Muundo na maana ya Hadithi fupi

Muundo na maana ya Hadithi fupi

Kasomi

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2014
Posts
11,027
Reaction score
20,413
HADITHI FUPI -ni historia fupi fupi zinazoelezea wazo kuu moja au tukio koja na wahusika wake huwa ni wachache.

SIFA ZA HADITHI FUPI

1 ) Ni fupi

2) Huelezea kitu kimoja au tukio moja.

3)wahusika wake ni wachache ambao hawakuzwi kwq kina.

4)Huanza karibu na mwisho.

5)Haina maelezo mengi ya ufumbuzi

6) Ni masimulizi ya kinathari

7)Haina uchangamano.

MUUNDO WA HADITHI FUPI

1Mwanzo

2Kati na

3Mwisho

Mwanzo wa hadithi

Huelekeza moja kwa moja kwenye msuko wa hadithi,mwandishi aweze kuiskuka vyema hadithi hio ili kuchangia kuleta umoja wa hadithi moja. Aseme yale yanayohitajika tu katika sentensi zake.

Kati kati ya hadithi

Baada ya utangulizi, hadithi inapaswa kuendelezwa ni katika sehem ya katikati ya hadithi ambapo dhamira ya hadithi inapaswa kuendelezwa.

Mwisho wa Hadithi

Mwisho wa hadithi fupi ni sehem muhim sana ni katika sehemu hii mwandishi hudhihirisha waziwazi funzk la hadithi. Ni suluhisho na utatuzi wa mgogoro, Mwisho wa hadithi unaweza kuashiriwa kwa

a) Utatuzi wa tatizo

b) Uhitimishaji wa kawaida kama vile kifo au kupotea

C) Ukamilishaji wa kitanakuzi yaani hali ya kupingana bajna ya mwanzo na mwisho.

d)Udhihirishaji wa funzo

e)Muhtasari wa mada.

f)Mbinu fikirishi

HISTORIA YA HADITHI FUPI

Chimbuko la hadithi fupi ni hadithi simulizi na andishi ambazo zinapatikana katika fasihi ya lugha nyingu duniani

Fani maarufu zinazotajwa kusimuliwa kama hadithi fupi ni kama vile NGANO, HEKAYA, RARA, UFENDI, RIWAYA CHUKU na Hurafa.
 
Emma umetisha! Au umeutoa stoo?

By the way,andiko lako ni zuri. Kura yangu moja umepata. Sijui mfumo wa upigaji kura uko namna gani.
 
Emma umetisha! Au umeutoa stoo?

By the way,andiko lako ni zuri. Kura yangu moja umepata. Sijui mfumo wa upigaji kura uko namna gani.
🙏🙏🙏 Shukurani mkuu kwakua pamoja nami tupo pamoja sana
 
Back
Top Bottom