Musoma: Polisi waenda kukagua nyumbani kwa mfanyabiashara maarufu na kada wa CCM, Peter Zakaria

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,552
Muda mfupi baada ya mfanyabiashara Peter Zakaria kufikishwa mahakamani na kusomewa mashtaka ya kujaribu kuua, Jeshi la Polisi limewasilisha na kupata kibali cha kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake mjini Tarime.

Waandishi wa Mwananchi waliopiga kambi katika viunga vya Mahakama ya Hakimu mkazi mjini Musoma wameshuhudia mfanyabiashara huyo tajiri akipandishwa ndani ya gari aina ya Land-cruiser tayari kwa safari ya kwenda nyumbani kwake mjini Tarime kwa ajili ya upekuzi.

Mjini Tarime, Waandishi wengine wa Mwananchi wameshuhudia mfanyabiashara huyo akiingizwa nyumbani kwake Barabara ya Nyamwaga akiwa ndani ya gari iliyokuwa ikisindikizwa na magari kadhaa yakiwemo mawili yaliyojaa askari Polisi wa Kikosi cha Kutuliza ghasia (FFU), waliojihami kwa silaha na zana za kiulinzi.

Mapema leo asubuhi Julai 5, Zakaria alifikishwa mahakamani na kusomewa mashtaka mawili ya kujaribu kuua.

ukaguzi%2Bpic.jpg
 
Hawachelewi kumuonyesha anamiliki misokoto ya bangi...
Hawa jamaa hawa wasikie tu.

Ila all in all acha jamaa naye aonje joto ya jiwe, mikono yake imelowa sana damu zisizo na hatia.

Aishie kwa risasi, atakufa kwa risasi.
Amwagaye damu ya mtu, damu yake naye itamwagwa na mtu.
 
hakuna kpnd nainjoy siasa za nchi hii zilivyo kama kpnd hk, ni mwendo wa drama asubh mchana jion. Nakuambia hv: ukiichukulia siasa serious na wakat wenzako wanaigza utapata tabu sana, yan n sawa unavyoangalia mieleka/movie ukachukulia serious wakat wenzako wanaigza utaishia kujiumiza. Drama goes with dramas. Na raha ya movie uiangalie ila ukijila ukaingia kuicheza basi watazamaji tutakuinjoy wewe. I real enjoy the seasons and its episodes if not parts
 
hakuna kpnd nainjoy siasa za nchi hii zilivyo kama kpnd hk, ni mwendo wa drama asubh mchana jion. Nakuambia hv: ukiichukulia siasa serious na wakat wenzako wanaigza utapata tabu sana, yan n sawa unavyoangalia mieleka/movie ukachukulia serious wakat wenzako wanaigza utaishia kujiumiza. Drama goes with dramas. I real enjoy the seasons and its episodes if not parts
mi hadi nimesahau ni episode ya ngap hii
 
Back
Top Bottom