Muono wangu 2020

Muono wangu 2020

neba

Senior Member
Joined
Nov 19, 2008
Posts
173
Reaction score
139
Nawasalimu wana JamiiForums.

Jana nilikuwa nyumbani, nikapata wasaa wa kukumbuka nyimbo zetu (sisi wahenga), nikasikiliza wimbo wa Ndalla Kasheba, Dunia msongamano.

Wimbo huo niliusikia tokea ulivyotolewa, lakini jana ulinipa mtazamo tofauti. Kuna kipande cha wimbo huo kinasema "Naelekea uzeeni sasa, lazima niwe na utulivu. Sababu kuishi kwingi ni kuona mengi, kuelimisha wanaobaki, waishi kwa heshima".

Nilijiunga rasmi na JamiiForums mwaka 2008. Kabla ya hapo nilikuwa naingia na kutoka. Tangu mwaka huo nimekuwa na posti chache mno.( Mimi mhenga, sipendi matusi na kejeli). Ila kwa siku naweza kuingia zaidi ya mara nne.

Nimesoma posti za mabigwa wengi mno, na zipo ambazo zilikuwa nzuri mno. Za kufundisha na kuelimisha. Baadhi ya memba waliokuwa wakiposti sasa, siwaoni katika majukwaa mbalimbali humu.

Wapo ambao wapo sasa, wanaposti mada fikirishi. Kaka Mshana jr najaribu kuelewa mada zako, japo ni ngumu mno na pia yupo Habibu Hanga (Bold) kwa kweli akiandika naelewa mno.

Kuna wanaoposti ili wapate likes. Lakini posti zao, ni tatanishi mno. Nakumbuka kuna waliokuwa wanatambiana kupigana. Hayo mambo ya ajabu mno kwa kizazi kipya.

Kuna ambao hueneza uvumi, uongo na uchonganishi na kudharau, mpaka Utaifa wao. Hawa ndio wanaomtesa Maxence Mello na wenzake. JamiiForums inateseka na habari ambazo hazina vyanzo vya kuaminika.

Nimekuta mijadala humu ndani, na nje. Moja iliyowahi kunishangaza sana, ni ile ya ulinzi wa sehemu nyeti, kuwa chini ya wageni. Ina maana kizazi hiki hakijui kuwa nchi yetu ni waalimu (trainers)?

Je hawajui kuwa tunafundisha watu toka nje ya mipaka yetu? Hawajui kuwa tuna waaminifu, watiifu na wa kweli wengi tu?Hawajui pia kwamba kuna watu wenye weledi wa juu mno?

Niliwahi pia kukuta mada nyingine mahali. Kuna kiongozi wa Taifa kubwa, alitembelea Tanzania. Watu walidai kuwa kiongozi huyo analindwa na robot. Kwa kweli nilisikitika mno.

Ukiachia hayo, napenda kuwaomba wana forum, waposti kwa akili. Nawakumbusha wakati sio milele. Kikubwa mno, nawakumbusha tena methali ya kiswahili isemayo, mchuma janga hula na wakwao.

Wakati wa tatizo la kweli, utashangaa, hakuna like wala nini. Watu watajificha.

Nasomaga pia 'research' mbalimbali.Niliona mbili zilizonichekesha mno. Ya kwanza ilisema Watanzania ni watu wasio na furaha kabisa duniani. Nikaona wengi wamesapoti hilo. Nikajiuliza, hivi hatutembei hata kwa jirani zetu tu tuone? Nchi ambazo huruhusiwi kuongea kitu kuhusu viongozi? Nchi ambazo kila leo wafungwa wanauawa rumande?

Nikaona tafiti ya pili humu ndani. Tanzania ni ya 14 kwa uchawi duniani. Nikashangaa mno. Nikasema labda hii tumependekeza wenyewe. Najua mpaka sasa kuna idadi kubwa ya Watanzania, hawatambiki, wala hawarogi. Humtegemea Mungu tu.

Umezaliwa Tanzania, u Mtanzania, hata ufanyeje, hata uikane nchi yako, historia itabaki hivyo.

Nawatakia Mema yote 2020

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesoma uzi mzima lakini sijafahamu lengo lake, Kweli kuelekea utuuzima unataka utulivu.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Nimejaribu kusoma nielewa nimeshindwa ,nisaidieni waelewa ,ila asante kwa kuandika jina la the bold nilikuwa natafuta jina lake ili niende kucheki mabandiko yake

Sent using Jamii Forums mobile app
Anajalibu kuwakumbusha vijana kuacha majivuni, dharau na mengine ya kufanana na hayo

Pia anawakumbusha vijana kwamba wakati si milele (huwezi kudumu katika Hali uliyinayo kwa maisha yote kua Kuna mda mambo yatabadilika kama una nguvu hizo nguvu haziwezi kudumu milele

Kama wewe ni kijana huwezi kua kijana milele

Kama unaishi kwa wazazi huwezi kuishi kwao milele

Kama una mamlaka hayo mamlaka hayawezi kudumu milele

Kama afya yako ni imara huwezi kua na afya imara milele

Hata Kama Kuna watu unawapenda wawe karibu yako hawawezi kua karibu yako milele Kuna muda wataondoka either kwa kwenda mahala pengine au kufa


Kwa ujumla hakuna kinachodumu kwa sisi wanadamu


Pia mwandishi anajaribu kuawakumbusha hasa vijana kwamba mchuma janga hula na wakwao kwa maana ya kwamba Kama Kuna mtu anafanya mambo yasiyompasa kufanya basi matokeo ya mambo yake yakitokea atakua yeye na ndugu zake

Mfano kwa wanafunzi wakifanya mgomo kwa sababu yoyote ile na yakitokea madhara ya mgomo yatakua Yana mwathiri mwanafunzi mmoja mmoja na ndugu zake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
a45, Nenda kwa Mangi mwambie akupe Pepsi kubwa nakuja kulipa...huu Uzi sijasoma ila asante kwa kunitafunia na kunimezeshea mdomoni
 
  • Thanks
Reactions: a45
Ndio nimeiona hii post leo baada ya kutafuta utulivu... Nashukuru mno kwa kutambua MCHANGO wangu hapa JF.. Natambua umekuwa kaka na rafiki mwema kwangu nje na ndani ya JF.. Ukinionya na kunishauri katika mengi.. Daima kwangu utakuwa zaidi ya kaka na rafiki

Umeandika kwa hekima na lugha tulivu... Katikati ya mistari hii ndio kuna ujumbe uliofichama.. Wengi hawajauona na kuuelewa
Maandishi yetu huongea na kututambulisha katika uhalisia wa ajabu sana.. Hatupaswi kujiandikia tu kama chizi mwokota makopo... Kuna maisha baada ya maandiko yetu nje ya JF na huu ndio UJUMBE mkuu na MUHIMU SANA...
Tunaishi katika nyakati ambazo maandishi yako yanaweza kuwa ndio kiama chako.. Na kiama kikifika wale waliokushangilia na kukusifu hutowaona popote pale... Watapotea kama hawajawahi kuwepo....

Tunao wenzetu ambao sasa makazi yao yamekuwa ni nyuma ya vyuma na milango ya chuma.... MAANDISHI yamewaponza... TUMAKINIKE... ... Ili siku tukiwa peke yetu na chatu...


Jr
 
Muono wako uko wapi sasa? Mhenga vipi wewe!
 
Back
Top Bottom