Mzawa_G

JF-Expert Member
Feb 27, 2014
667
1,467
Muonekano wa mwezi ukionekana na mashimo katika maeneo yake mbalimbali hata ukiwa huku duniani pia unaweza ukayashuhudia haya mashimo kama siku mwezi ukionekana wote (Full moon) na anga likiwa limetulia.

Mashimo hayo yamesababishwa na asteroidi na vimondo mbalimbali vilivyoweza kuushambulia mwezi wetu na vinavyoendelea kuushambulia mwezi wetu kila siku kila baada ya muda.

kwakuwa mwezi wetu hauna anga hewa (atmosphere) au tuseme kwakuwa mwezi wetu hauna uwezo wa kushika anga hewa kutokana na uwezo mdogo wa kani yake ya uvutano (gravity), ambayo kwa kawaida husaidia kushikilia matabaka mbalimbali kuendelea kubaki katika gimba na kuzunguka gimba lote kwa ujumla.

Sasa kwenye mwezi wetu kitu hicho hakuna kabisa na hupelekea vinasaba vyote vya anga hewa kupotelea angani. Anga hewa hucheza katika nafasi ya ulinzi wa vitu mbalimbali vinavyoweza kushambulia gimba.

Sasa kama gimba litakuwa na wingi wa anga hewa mbalimbali au matabaka ya anga hewa mazito basi ndipo ulinzi wa gimba unavyokuwa mkubwa kwakuwa vitu vyote huunguzwa na wakati mwengine husambaratishwa kabisa katika kipindi cha kuingia kwenye magimba yenye matabaka ya anga hewa mazito.

Kama mwezi wetu ungelikuwa unauwezo.wa kushika matabaka ya anga hewa mazito na mengi basi kusingekuwa na mashambulizi mengi ya vimondo na mawe makubwa ya astreroid.

Moudyswema Tanzaniascienceyetu AstronomyKiswahili
FB_IMG_1674671930595.jpg
 
Popoma wewe

Umbali gani uliopo kati ya kamera iliyopiga picha hiyo na hicho kitu kilichopigwa picha?

Sijasoma thread ila kulingana na hii comment

Inaonekana jamaa kaupiga mwezi picha toka vingunguti machinjioni alafu umetoka kama zile pic za Nasa

Conclusion
Asituone watoto
Wabongo ndio tunapofeli hapa. Mada imeletwa ni ya kitaalamu mtu hata hujaisoma unaanza kejeli wakati imeelezwa vizuri kabisa kwa fact za kisayansi.
 
Kabla cjaweka uzi wowote humu jf huwa najua wapo wenye maswali mazur, ya kipuuzi, yasioelweka na wafia dini uchwara
Thus why huwa cjibu maswali ambayo hayaeleweki ...
 
Tuliwahi kusikia kuwa kuna jiwe kubwa lilikuwa likielekea usawa wa dunia na hivyo lingeigonga dunia kwa kishindo kikuu! Hii ilileta hofu kubwa miongoni mwa mataifa makubwa (mataifa yaliyoendelea), kwani ilionekana kuwa impact ya jiwe hilo kubwa ingesababisha myumbisho au hata kuitoa kabisa katika njia (orbit) yake kulizunguja jua! Hapo wakaja na utaalamu wao kwa kupeleka chombo kilicholipiga jiwe hilo na kulielekeza usawa mwingine kutoka ule wa dunia. Swali langu ni kuwa: hayo mawe yanayopiga mwezi hayauondoi (deflect) kutoka kwenye njia (orbit) yake? Hilo shimo lililotokea hapo kwenye picha linaonyesha kuwa impact ilikuwa kubwa sana, na inaonyesha kuwa mawe (au vimondo) mengi yameupiga mwezi katika maeneo yake tofauti tofauti, je njia ya mwezi haijabadilika kwa miaka yote ukiwa unaizunguka dunia?
 
Tuliwahi kusikia kuwa kuna jiwe kubwa lilikuwa likielekea usawa wa dunia na hivyo lingeigonga dunia kwa kishindo kikuu! Hii ilileta hofu kubwa miongoni mwa mataifa makubwa (mataifa yaliyoendelea), kwani ilionekana kuwa impact ya jiwe hilo kubwa ingesababisha myumbisho au hata kuitoa kabisa katika njia (orbit) yake kulizunguja jua! Hapo wakaja na utaalamu wao kwa kupeleka chombo kilicholipiga jiwe hilo na kulielekeza usawa mwingine kutoka ule wa dunia. Swali langu ni kuwa: hayo mawe yanayopiga mwezi hayauondoi (deflect) kutoka kwenye njia (orbit) yake? Hilo shimo lililotokea hapo kwenye picha linaonyesha kuwa impact ilikuwa kubwa sana, na inaonyesha kuwa mawe (au vimondo) mengi yameupiga mwezi katika maeneo yake tofauti tofauti, je njia ya mwezi haijabadilika kwa miaka yote ukiwa unaizunguka dunia?
@stars hapana kaka hakukuwa na jiwe kubwa ambalo lingeweza kuwa na impact ya kutoa dunia katika njia yake

kaka unless lingekuwa na ukubwa unaokaribiana na duniani yetu

nasa walifanya majaribisho tu ya kuangalia njia kadhaa ambazo kwa baadae wanaweza kuzitumia kujilinda na mawe makubwa kama yatakuwa yanataka kuigonga dunia yetu
 
Back
Top Bottom