Mungu ni dhana, hayupo.
Ni dhana kwamba kuna anayeweza yote, anayejua yote na mwenye upendo wote ambaye ameumba ulimwengu huu.
Ni dhana tu na hayupo kwa sababu dhana yenyewe inajipinga.
Dhana inajipinga kwa sababu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote asingeumba ulimwengu wenye kuruhusu maovu kama huu. Hii ni contradiction. Ni kama useme pembetatu haiwezi kuwa duara na duara haiwezi kuwa pembetatu, halafu useme kuna pembetatu ambayo hapo hapo ni duara.
Haiyumkiniki.
Mungu hayupo, ni kitu kinaitwa "imagined reality".
Hili si jambo baya by default. Kuna watu wanatetea dhana ya kuwepo Mungu hata baada ya kujua hayupo kwa sababu wanasema ni njia nzuri ya kuwafanya watu waishi kwa order.
Lakini hilo halifanyi Mungu awe yupo kama vile mstari wa Greenwhich unaopita Accra na London, ambao unatumika kama katikati ya dunia katika kupima masaa, usivyo katikati ya dunia.