Mungu hayupo? Atheist njooni mthibitishe

Mungu hayupo? Atheist njooni mthibitishe

JumaKilumbi

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2022
Posts
432
Reaction score
507
Dini zilikuwepo tangu enzi na enzi, jamii za wanaadamu zimekuwa zikiabudu vile wanavyoviita Mungu kwa miaka mingi sana hili halina ubishi.

Uwepo wake miaka mingi haina maana ni sahihi kuwepo wake maana hata uongo usipodhihirika huonekana ukweli miaka yote mpaka ukweli utakapofahamika.

Ila kuna sehemu ya watu kwenye jamii wamekuwa wakitilia mashaka na kukosoa wazo lenyewe la kuwepo kwa huyo anaeitwa Mungu. Wanaoamini (imani yoyote tu ‘as long as’ wanamuabudu wanachokiita Mungu) wanasistiza kuwa yupo na uwezo wake ni Mkuu sana.

Hoja za waumini nazifahamu baadhi, ila hoja za Atheist sijazielewa.

Ningependa kuwaelewa zaidi Atheists, Karibuni hapa Atheist walau mthibitishe (kama mtaweza) kuwa huyo wa kuitwa Mungu hayupo.

Lakini kwanza ni lazima tufafanue nini maana ya MUNGU, kwa maana kukurupuka kujibu swali ilhali hatujui maana ya dhana ya msingi wa swali itakuwa ni uhayewani wa kiwango cha juu sana.

Karibuni sana!
FB02F851-AFA5-4F45-B078-2F153A980D10.jpeg
 
Dini zilikuwepo tangu enzi na enzi, jamii za wanaadamu zimekuwa zikiabudu vile wanavyoviita Mungu kwa miaka mingi sana hili halina ubishi.

Uwepo wake miaka mingi haina maana ni sahihi kuwepo wake maana hata uongo usipodhihirika huonekana ukweli miaka yote mpaka ukweli utakapofahamika.

Ila kuna sehemu ya watu kwenye jamii wamekuwa wakitilia mashaka na kukosoa wazo lenyewe la kuwepo kwa huyo anaeitwa Mungu. Wanaoamini (imani yoyote tu ‘as long as’ wanamuabudu wanachokiita Mungu) wanasistiza kuwa yupo na uwezo wake ni Mkuu sana.

Hoja za waumini nazifahamu baadhi, ila hoja za Atheist sijazielewa.

Ningependa kuwaelewa zaidi Atheists, Karibuni hapa Atheist walau mthibitishe (kama mtaweza) kuwa huyo wa kuitwa Mungu hayupo.

Lakini kwanza ni lazima tufafanue nini maana ya MUNGU, kwa maana kukurupuka kujibu swali ilhali hatujui maana ya dhana ya msingi wa swali itakuwa ni uhayewani wa kiwango cha juu sana.

Karibuni sana!
View attachment 2355249
wakija kudhibitisha ni kutaka kujengea watu imani flani tu bila udhibitisho unaoingia akilin , hyo imani ya kuamn Mungu hayupo haina tofauti na iman ya din flan tu, waulize ni nguvu gani ilipangilia mifumo mbalimbali kiustadi bila kuathiri viumbe hai , wanasema wanaamni sayansi waulize sayansi inaweza simama bila kutegemea rawmaterial iliyokuwepo tu bila ufundi kutoka kwa binadamu?

waulize ni nguvu gani na intelligence ipi inayofanya kazi ndani sperm kuunda kiumbe kilicho na mifumo na mipangilio maalumu ? ni kitu gan kiliweka sukari ndan ya muwa na kwa dhumuni lipi je ilitokea tu bila nguvu na inteligence yoyote?
 
Yani wewe uanzishe mada, alaf utake watu waje wathibitishe?

Nadhan ilifaa wewe uweke facts zako kwa upana, then opposers waje na reasons zao, ila sio kutaka waje wapinge kauli ambayo haijashiba maelezo
Hutapanga nini nifanye ama nini nisifanye.

Kama unaona kufanya hivyo ni sahihi fungua mada kisha weka ‘facts’ then “opposers waje na reasons zao”
 
Wakija kudhibitisha ni kutaka kujengea watu imani flani tu bila udhibitisho unaoingia akilin , hyo imani ya kuamn Mungu hayupo haina tofauti na iman ya din flan tu, waulize ni nguvu gani ilipangilia mifumo mbalimbali kiustadi bila kuathiri viumbe hai , wanasema wanaamni sayansi waulize sayansi inaweza simama bila kutegemea rawmaterial iliyokuwepo tu bila ufundi kutoka kwa binadamu? waulize ni nguvu gani na intelligence ipi inayofanya kazi ndani sperm kuunda kiumbe kilicho na mifumo na mipangilio maalumu ? ni kitu gan kiliweka sukari ndan ya muwa na kwa dhumuni lipi je ilitokea tu bila nguvu na inteligence yoyote?
Wakija kusema hao ni alliance waliunda vyote hivyo ( annunaki ) basi waambie kama ni wao sisi tumeamua kuwaita Mungu kwa sababu wametuumba , hatuna uwezo juu yao na ndo Mungu ni taofauti ya majina tu.
 
MUNGU ni suala la kiimani na huwezi thibitisha suala la kiimani nje ya imani. Tunaamini MUNGU yupo sababu hakuna mbadala wa concept isiyo na shaka ya uwepo wa ulimwengu. Hii imani ni zao la kutokewepo kwa facts zisizo na shaka za sababu za uwepo wetu na vyote tuvionavyo. Ukisema tuachane na imani ya uwepo wa MUNGU njoo na hitimisho la yote tuliyoyakuta duniani.

Siku tukipata jibu kuwa ss ni nn na ulimwengu ni nn basi hiyo imani itafutika. Kwa sasa yoyote apingaye uwepo wa MUNGU bila ushahidi timilifu wa kutokuwepo kwake ni mfuasi wa adui wa MUNGU aitwaye shetani, ibilisi. Hii kutaka kubatilisha uwepo wa MUNGU kwa njia ya kushindwa kuthibitisha uwepo wake nje ya imani haipo sawa sababu imani ya uwepo wake ni matokeo ya uwepo wetu pasipo kuwa na ushahidi usio na shaka wa sababu za uwepo.

Hii sababu ya uwepo wetu tusiyoweza kuithibitisha ndiyo iliyozaa imani ya uwepo wa MUNGU.
 
MUNGU ni suala la kiimani. Tunaamini MUNGU yupo sababu hakuna mbadala wa concept isiyo na shaka ya uwepo wa ulimwengu. Hii imani ni zao la kutokewepo kwa facts zisizo na shaka za sababu za uwepo wetu na vyote tuvionavyo. Ukisema tuachane na imani ya uwepo wa MUNGU njoo na hitimisho la yote tuliyoyakuta duniani. Siku tukipata jibu kuwa ss ni nn na ulimwengu ni nn basi hiyo imani itafutika. Kwa sasa yoyote apingaye uwepo wa MUNGU bila ushahidi timilifu wa kutokuwepo kwake ni mfuasi wa adui wa MUNGU aitwaye shetani, ibilisi.
Ukiachana na iman ya uwepo wa Mungu utaingia kwenye imani mpya wa kutokuwepo kwa Mungu, ukitaka kushinda hlo iman isiwepo kabsa kitu ambacho ni uongo.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
ukiachana na iman ya uwepo wa Mungu utaingia kwenye imani mpya wa kutokuwepo kwa Mungu , ukitaka kushinda hlo iman isiwepo kabsa kitu ambacho ni uongo.
Mkuu, imani inazaliwa, inatunzwa, inakomaa kisha inarithishwa. Sisi ni vizazi tulivyorithi imani kutoka kwa mababu. Imani ya kutoamini uwepo wa MUNGU bila majibu kamili ya ulimwengu, maisha na kifo ni nn kwangu mm ni ujinga kama ujinga mwingine.

Imani ya kuamini uwepo wa MUNGU sababu hakuna majibu mbadala ya sababu za uwepo wa ulimwengu, maisha na kifo kwangu mm ni sahihi sana. Mtu akisema hakuna MUNGU anapaswa aseme sisi ni nn, kifo ni nn, yote tuyaonayo ni nn.

Tunasema MUNGU yupo sababu tupo ila hatujui sisi ni nn, maisha ni nn, kifo ni nn.
 
Mkuu, imani inazaliwa, inatunzwa, inakomaa kisha inarithishwa. Sisi ni vizazi tulivyorithi imani kutoka kwa mababu. Imani ya kutoamini uwepo wa MUNGU bila majibu kamili ya ulimwengu, maisha na kifo ni nn kwangu mm ni ujinga kama ujinga mwingine. Imani ya kuamini uwepo wa MUNGU sababu hakuna majibu mbadala ya sababu za uwepo wa ulimwengu, maisha na kifo kwangu mm ni sahihi sana. Mtu akisema hakuna MUNGU anapaswa aseme sisi ni nn, kifo ni nn, yote tuyaonayo ni nn. Tunasema MUNGU yupo sababu tupo ila hatujui sisi ni nn, maisha ni nn, kifo ni nn.
Mkuu imani ipo tu ata wasingeanzisha mababu, unapanda gari unaamini huyo dereva atakufikisha salma japo haujui kama jana alipata kichaa unaamni tu, unalala unaamn kesho utaamka, unaamni tu, unaamni tu binadamu ana akili ata haujawahi kuiona akili kimaumbile ya kimwili unaamin tu, unaamni tu kuna hewa, ila hauioni kwa macho unaamn tu, unaamn kuna joto na unalihisi ila haujawahi kuliona

KWAHIYO KUTOONA Jambo flani kwa macho hakumaanishi jambo hlo halipo, ila kuona matokeo tu au kuhisi nikidhibitsho tosha hlo jmbo lipo, kuna maumbile sio rahisi kuyaona kwa macho kwa sababu yapo kwenge enegry ya juu na frequence ya hali ya juu.
 
Mkuu, imani inazaliwa, inatunzwa, inakomaa kisha inarithishwa. Sisi ni vizazi tulivyorithi imani kutoka kwa mababu. Imani ya kutoamini uwepo wa MUNGU bila majibu kamili ya ulimwengu, maisha na kifo ni nn kwangu mm ni ujinga kama ujinga mwingine. Imani ya kuamini uwepo wa MUNGU sababu hakuna majibu mbadala ya sababu za uwepo wa ulimwengu, maisha na kifo kwangu mm ni sahihi sana. Mtu akisema hakuna MUNGU anapaswa aseme sisi ni nn, kifo ni nn, yote tuyaonayo ni nn. Tunasema MUNGU yupo sababu tupo ila hatujui sisi ni nn, maisha ni nn, kifo ni nn.
Sisi ni Mungu katika maumbile yakuonekana, maisha ni mchezo wa kuigiza, kifo ni badiliko la kiumbo tu kutoka maumbile ya ngaz ya chini kwenda ngazi ya juu zaidi, kma lilivyobadiliko la maji, mvuke barafu.
 
Mkuu imani ipo tu ata wasingeanzisha mababu , unapanda gari unaamini huyo dereva atakufikisha salma japo haujui kama jana alipata kichaa unaamni tu, unalala unaamn kesho utaamka , unaamni tu , unaamni tu binadamu ana akili ata haujawahi kuiona akili kimaumbile ya kimwili unaamin tu, unaamni tu kuna hewa , ila hauioni kwa macho unaamn tu , unaamn kuna joto na unalihisi ila haujawahi kuliona KWAHIYO KUTOONA Jambo flani kwa macho hakumaanishi jambo hlo halipo , ila kuona matokeo tu au kuhisi nikidhibitsho tosha hlo jmbo lipo , kuna maumbile sio rahisi kuyaona kwa macho kwa sababu yapo kwenge enegry ya juu na frequence ya hali ya juu.
Upo sawa boss
 
sisi ni Mungu katika maumbile yakuonekana , maisha ni mchezo wa kuigiza , kifo ni badiliko la kiumbo tu kutoka maumbile ya ngaz ya chini kwenda ngazi ya juu zaidi , kma lilivyobadilio la maji ,mvuke barafu.
Hii ni nadharia japo katika uhalisia inamake sense.
 
Jukumu la kutoa uthibitisho lipo kwa mtoa madai sio mpinga mdai. Mimi nimekwambia nimesoma harvard wewe umeangalia kwenye CV yangu ujaona popote ambapo panaonesha nimesoma harvard hapo ni mimi ndio nitapaswa kukuthibitishia nimesoma harvard kwa kukuonesha cheti nitaoneka wa ajabu nikitaka wewe ndo unithibitishie sijasoma harvard.

Ambao hawaamini uwepo wa Mungu hawakuja tu madai hayo, waliikuta iyo nadharia ya uwepo wa Mungu kwenye jamii walizoishi walifundishwa baada ya kuchanganya za kuambiwa na zao ndio wakaja na hitimisho hizi habari sio kweli.

Kwaiyo unaona hapo madai yalianza kutolewa wao ndio wakaja kuyapinga na moja ya vigezo vyao vya kupinga ni kukosekana kwa uthibitisho juu ya uwepo wa Mungu. waumini wengi wanapoombwa uthibitisho wa uwepo wa Mungu wanachukulia ufinyu wao wa maarifa kama uthibitisho wa uwepo wa Mungu kitu ambcho sio sahihi, ndipo wanakuja na maswali kama ulimwengu ulitokea wapi, pumzi unayovuta imetokea wapi n.k

Lazima tuelewe kwamba ulimwengu ulkwepo miaka mingi sana kama yetu binadamu kwaiyo hatuwezi kujua kila kitu kirahisi rahisi tu kuna mambo mengi hatuyajui kutokana na ugeni wetu kwenye huu ulimwengu na inawezekana kabisa hakuna kizazi kitakachokuja kuwa na majibu yote kuhusu ulimwengu kwaiyo pale ambapo maarifa yako yamefika mwisho ni vyema ukakiri haujui ukitaka kumweka Mungu katika iyo point ambayo maarifa yako yamefika mwisho basi onesha ushaidi wa kimahusiano kati ya Mungu na suala husika. Kwa msingi huo mimi nafikiri wanaoamini uwepo wa Mungu ndio wanapaswa kutoa uthibitisho wa uwepo wake
 
Back
Top Bottom