Mungu Haishi. Maana Si Kiumbe

Majibu mepesi kama haya ndio yanafunga akili za watu. Ujiulizi kwanini kizazi kimoja kina pewa vitabu na kingine hakipewi.
 
Tatizo lako unadhani huo mwili wako ndiyo wewe.
Usijikane Jinsi ulivyo wewe una Mwili na Ndio ulivyo na Mungu ndio kakuumba Hivyi hivyo


Utakesha unamtafuta Mungu na hautamwona kamwe.

Sasa Kwani Nimekuambia Namtafuta Ndugu yangu. Anayemtafuta ni yule asiyejua ukweli. Ndio maana Mnaenda Kanisani na Misikitini kumtafuta Mungu maana Bado hamjui ukweli mngekuwa mnaujua Ukweli msingeenda Kwenye Nyumba hizo kumtafuta. Mpaka Inafikia Hatua Kuna Makanisa yanaandika MUNGU YUPO HAPA mbele ya Madhabahu zao. Haya yote ni kwa sababu hakuna Ukweli ndani Yenu

Hakuna Aliyewahi kumuona Mungu ndio maana Hata Yesu alipoulizwa Na Wanafunzi wake Tuonyeshe Mungu hakuwaonyesha Wanafunzi wake
 
Kama imani ya mtu ina nguvu kiasi hiki Mungu wa nini sasa.
😄😄😄😄😄 Daah

Kwa hiyo chombo kama chombo unaweza kukila bila msosi ndani yake? Imani na chombo ni sawa. Chombo kidogo msosi kidogo, chombo kikubwa msosi mwingi. Hakuna chombo hakuna msosi.

Imani.
 
Mkuu napenda sana watu wanaofikiri Kwa akili huru, Mimi nishaanza kuamini shetani kwa maana ya kiumbe hayupo, ila mambo yote negative ie wizi, uzinzi, uuaji, matusi etc ndo shetani, yaani shetani ni vitendo na sio kiumbe. Kwasabu nafikiria Yana Lucifer (shetani) kaumbwa na Mungu (kama tunavyofundishwa) alafu baada ya kumuasi, Mungu anapigana vita na yeye. Yani Mungu anapigana vita na kiumbe chake??? Je malaika Michael, au Gabriel naye akiasi itatokea Tena vita huko mbinguni, je wakipigwa wataenda kuungana na Lucifer (shetani tunayehadithiwa) au watantengeneza nao ufalme wao??
 
Daah

Kwa hiyo chombo kama chombo unaweza kukila bila msosi ndani yake? Imani na chombo ni sawa. Chombo kidogo msosi kidogo, chombo kikubwa msosi mwingi. Hakuna chombo hakuna msosi.

Imani.
Kwahiyo kuwa na Imani ni lazima umjue Mungu?
 
Kwenye vitabu husika.
Kitabu kilichoandikwa na Binadamu au Mungu!

Na je kabla ya Kitabu hicho ulikuwa unajua kuna Mungu? Maana kitabu hivyo unavyoviamini ni vya Juzi tu. Maana Wengine mmejua kwamba Kulikuwa na Gharika Baada ya Kitabu kuja Kwenu. Hata Babu yako Inawezekana hajui kama Kulikuwa na Magharika
 
Kwahiyo wewe akili inakwambia Mbingu ipo juu ya mawingu??
 
Shida inakuja miungu haujawahi sema chochote kile. Zaidi ya wakoloni kutuletea vitabu wakidai miungu inataka nini. Lakini miungu yenyewe haijawahi kusema kitu.
 
Usijikane Jinsi ulivyo wewe una Mwili na Ndio ulivyo na Mungu ndio kakuumba Hivyi hivyo

Ukisema nina mwili ni sahihi lakini mimi sio huo mwili. Huo mwili ni wangu nimepewa na hili silikatai japo unaniwekea maandishi ya kujikana.

Nina mwili ndio.
 
Mungu kama hana sifa ya kuishi basi hayupo, ili awepo lazima awe na sifa ya kuishi. Na kuhusu kutokuwa na sifa ya uhai. Embu tuambie uhai ni nini? Na kinyume cha neno uhai ni nini? Kama Mungu hana uhai atakuwa ni mfu
 
Mungu hafanani na kitu chochote alafu hapo Mungu kaumba mtu kwa mfano wake. Inafikirisha sana
 
Hata malaika na Majini yanazaliana kama Wewe na Mimi Mkuu ingawa Wewe huyaoni kwa Macho.

Mungu ameweka Mifumo yake Ya Uzalianaji hata Binadamu wa kwanza Kuumbwa Waliumbwa wakiwa na Vizazi ili wazae na Wakawekwa Duniani

MALAIKA nao hivyo hivyo Wakawekwa sehemu yao
Majini hivyo hivyo Wakawekwa sehemu yao

Hamaanishi kwa Vile wewe una Uhai basi na Mungu awe na Uhai. Jiwe halina Uhai ila Limeumbwa. Kwa Mantiki yako inatakiwa yule aliyeliumba Jiwe lazima asiwe Hai ili aweze umba Jiwe
 
Kabla ya shule ulikuwa unajua kuna herufi A?

Maswali mengine ujijibu mwenyewe.
 
Rudi kwenye post yangu hapo juu nilipoelekeza imani inavyofanya kazi.
Ndio maana nakwambia imani ni kitu binafsi hakitegemei Mungu maana hata wasio amini Mungu wana imani na zinafanya kazi.
 
Ndio maana nakwambia imani ni kitu binafsi hakitegemei Mungu maana hata wasio amini Mungu wana imani na zinafanya kazi.
Hayo yote nimeelezea kwenye post yangu ya imani. Rudi ukasome vizuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…