Mungu anajibu maombi

Mungu anajibu maombi

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
61,201
Reaction score
99,936
Inapokuja suala la imani hegeuka na kuwa kitu kigumu sana! Niliajiriwa kwenye International NGO, ilionekana nafasi nzuri kwa baadhi ya watu lakini kwangu mimi ilikua ni post yenye changamoto sana.

Baada ya kupata post ile ghafla sana mambo yaligeuka, Boss wangu ambaye alikua si Mtanzania alianza kunichukia sana sana. Ikafika kipindi hata kwenda kazini kwangu ikawa kama vile nakwenda kituo cha Polisi. Yaani ikifika saa kumi na moja asubuhi nakosa usingizi kabisa. Kwa ukweli hakua na sababu yoyote ya msingi ya kunichukia.

Nilianza kusali na kumuomba MUNGU sana kwamba kama kweli kuna jambo baya nimemtendea huyu Mama basi MUNGU anisamehe lakini pia niliomba sana AMANI na huyu Boss wangu, niliomba upatanisho, sikutaka kuweka visasi.

Nilijitahidi sana kufanya kazi kwa bidii na kwa ufanisi, baada ya miaka mitatu ya maumivu makali hatimae Boss wangu huyu alipandishwa cheo na kupelekwa Marekani yalipo Makao Makuu ya NGO.

Mwaka mmoja baadae aliachishwa kazi ghafla sana, tena akiwa kwenye Mkutano tu, lakini kitu cha kushangza siku moja nikiwa nyumbani nilipokea text kwenye namba yangu ya Whatsapp, sikuifahamu ile namba kwakua ni ya Marekani na kwenye Profile ilionekana picha ya Binti, nikaijibu tu lakini sikuhangaika kujua ni nani. Week mbili baadae nilipokea text nyingine kwenye namba ile ile ikinisalimia! Kucheki kwenye Profile Photo nikakuta ni yule Mama.

Nilimjibu na nikamwambia nimefurahi kusikia tena toka kwake. Kilichofuata baada ya hapo aliniomba kama nitasikia Opportunity yoyote hapa Tanzania nimshikirikishe! Nikamjibu nikamwambia sawa!

Nimeandika hivi kuonyesha kuwa ile miaka ya maumivu yote nimefurahi imekwisha, niliomba AMANI na hakika tumepatana! Moja ya mistari kwenye text yake aliandika hivi Get Ride of Bitterness!! Nikajua amejua ukweli kuwa sikuwahi kumtendea baya! Tafuteni kuwa na AMANI na Watu wote......Waebrania 12:14

SIKUOMBA AFUKUZWE NA SIKUFURAHISHWA NA KITENDO CHA KUFUKUZWA NILIOMBA NIPATE KUWA ANA AMANI NAYE. NA SASA TUNAONGEA NA SASA ANAWEZA KUNIOMBA NIMTAFUTIE FURSA HAPA BONGO. NAAMINI NIMEELEWEKA.

 
ubarikiwe, siku zote mungu anajibu. AMINI acha kujichelewesha hata katika mambo mengine muombe mungu anjibu.
 
dah ni ngumu kidogo, kwaio njia ya wewe kuwa na amani ni bosi wako kuhamishwa na baadae kufukuzwa kazi
 
Mpwa wangu Elli kuna msemo usemao muomba Mungu hakosi nafikiri umetimia.
 
Last edited by a moderator:
Unataka kutuambia kuwa kwa kusali kwako ndio kulisababisha huyo boss wako afukuzwe kazi? Kama jibu ni ndiyo,hizo sala bado unaziona kuwa ni kimbilio kwa watu wote wenye kuamini?
 
Hujamuelewa vizuri kawoli,amani kwake ni kuwa sasa yuko vizuri na aliyekuwa bosi wake,they are getting along well now.God bless you eli.
 
Last edited by a moderator:
Imani ni kitu comlicated sana, hapa kuna ujumbe nimeupata na pia kuna jambo limenichananya.

Umefurahia mbaya wako kuwa chini yako sasa? Sijaelewa kwenye part ya kufukuzwa part na kuja kwako kutafuta kazi.
 
Ndio changamoto za dunia mkuu,ila sijakuelewa uliposema Mungu kajibu Maombi. Unamaanisha ulikuwa ukiomba huyo bosi wako afukuzwe kazi ama?
 
Maombi mazuri sana hayo, hata mimi niko namwomba Mungu nikifanya MAOMBI ya kusaka AMANI. nimekataa kufanya maombi ya kulipiza kisasi yaani maombi ya kuombeana mabaya.
Kama wabongo wengi walivyo. AMANI kwanza.
 
kimsingi kuna mashaka juu ya uwepo wa mungu!

hiki unachokishangilia kweli wewe unadhani ni uwepo wa mungu? mungu gani huyo uliye naye ambaye unashangilia eti mwenzako kafukuzwa kazi? na haya ndiyo watu wanashuhudia makanisani eti mungu kanitendea muujiza.

leo hii ukibishana na mtu kuhusu mambo ya imani anasema subiri na katika kusema subiri mungu atajidhihirisha anategemea upate matatizo na ndio uje kutambua uwepo wa mungu.

tunaamini mungu ni the creator of everything sasa nguvu ya creation umewahi kuiona wapi? yaani kiumbe aliyetengeneza ulimwengu huu au viumbe vyote leo hii anakuja kumfukuzisha kazi bosi wako anayekuchukia bila wewe kujua sababu? huko ni kusema kiumbe huyo amefilisika. lakini wewe unayeshangilia kufukuzwa kwa mwenzako je atakuacha huru?

ninachotaka kukueleza kuna uwezekano wa imani kutokutoka unakokudhani na kule imani zinakotoka wanatake advantage ya matukio au kuchochea baadhi ya matukio alafu unaletewa mawazo mungu kafanya kazi. kwa logic ya kawaida mungu hawezi kufanya hilo unalolishangilia ila kitu kinaweza kujifanya mungu kikafanya upumbavu ukashangilia na chenyewe kikabaki kinakucheka. kama wengine wanavyodanganywa kuwa ukichinja albino utapata mali basi wanachinja na kinachowadanganya kinabaki kuwacheka.
Elli
 
Last edited by a moderator:
dah ni ngumu kidogo, kwaio njia ya wewe kuwa na amani ni bosi wako kuhamishwa na baadae kufukuzwa kazi
sikuomba afukuzwe na sikufurahishwa na kitendo cha kufukuzwa niliomba nipate kuwa ana amani naye. Na sasa tunaongea na sasa anaweza kuniomba nimtafutie fursa hapa bongo. Naamini nimeeleweka.
 
jAMANI WAZEE NA VIJANA WENZANGU, TUJIFUNZE KUSOMA NA KUELEWA, HAKUNA MAHALI NIEMADNIKA KUWA NIMEFURAHI KUWA AMEFUKUZWA KAZI, NIMESEMA HATIMAE TUMEWEZA KUONGEA! HATIMAE AMENIONA NA MIMI KUWA MTU. Tujifunze kusoma kabla ya kukimbilia ku-comment
kimsingi kuna mashaka juu ya uwepo wa mungu!

hiki unachokishangilia kweli wewe unadhani ni uwepo wa mungu? mungu gani huyo uliye naye ambaye unashangilia eti mwenzako kafukuzwa kazi? na haya ndiyo watu wanashuhudia makanisani eti mungu kanitendea muujiza.

leo hii ukibishana na mtu kuhusu mambo ya imani anasema subiri na katika kusema subiri mungu atajidhihirisha anategemea upate matatizo na ndio uje kutambua uwepo wa mungu.

tunaamini mungu ni the creator of everything sasa nguvu ya creation umewahi kuiona wapi? yaani kiumbe aliyetengeneza ulimwengu huu au viumbe vyote leo hii anakuja kumfukuzisha kazi bosi wako anayekuchukia bila wewe kujua sababu? huko ni kusema kiumbe huyo amefilisika. lakini wewe unayeshangilia kufukuzwa kwa mwenzako je atakuacha huru?

ninachotaka kukueleza kuna uwezekano wa imani kutokutoka unakokudhani na kule imani zinakotoka wanatake advantage ya matukio au kuchochea baadhi ya matukio alafu unaletewa mawazo mungu kafanya kazi. kwa logic ya kawaida mungu hawezi kufanya hilo unalolishangilia ila kitu kinaweza kujifanya mungu kikafanya upumbavu ukashangilia na chenyewe kikabaki kinakucheka. kama wengine wanavyodanganywa kuwa ukichinja albino utapata mali basi wanachinja na kinachowadanganya kinabaki kuwacheka.
 
kimsingi kuna mashaka juu ya uwepo wa mungu!

hiki unachokishangilia kweli wewe unadhani ni uwepo wa mungu? mungu gani huyo uliye naye ambaye unashangilia eti mwenzako kafukuzwa kazi? na haya ndiyo watu wanashuhudia makanisani eti mungu kanitendea muujiza.

leo hii ukibishana na mtu kuhusu mambo ya imani anasema subiri na katika kusema subiri mungu atajidhihirisha anategemea upate matatizo na ndio uje kutambua uwepo wa mungu.

tunaamini mungu ni the creator of everything sasa nguvu ya creation umewahi kuiona wapi? yaani kiumbe aliyetengeneza ulimwengu huu au viumbe vyote leo hii anakuja kumfukuzisha kazi bosi wako anayekuchukia bila wewe kujua sababu? huko ni kusema kiumbe huyo amefilisika. lakini wewe unayeshangilia kufukuzwa kwa mwenzako je atakuacha huru?

ninachotaka kukueleza kuna uwezekano wa imani kutokutoka unakokudhani na kule imani zinakotoka wanatake advantage ya matukio au kuchochea baadhi ya matukio alafu unaletewa mawazo mungu kafanya kazi. kwa logic ya kawaida mungu hawezi kufanya hilo unalolishangilia ila kitu kinaweza kujifanya mungu kikafanya upumbavu ukashangilia na chenyewe kikabaki kinakucheka. kama wengine wanavyodanganywa kuwa ukichinja albino utapata mali basi wanachinja na kinachowadanganya kinabaki kuwacheka.

naondoka online kdg....ningekua na angalau dk. 5 nadhan tungeeleweshana......kijana mtoa mada barikiwa sana kwa moyo wako wenye uvumilivu mwingi na upendo......my GOD bless you..
 
Maombi mazuri sana hayo, hata mimi niko namwomba Mungu nikifanya MAOMBI ya kusaka AMANI. nimekataa kufanya maombi ya kulipiza kisasi yaani maombi ya kuombeana mabaya.
Kama wabongo wengi walivyo. AMANI kwanza.

Hujatendewa ubaya mkuu
 
Back
Top Bottom