Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,192
- 10,926
Hii hadithi ni ndefu sana.Lakini tutaileta hapa kwa ufupi.Najua kuna wataalamu wataiendeleza.
Kwa ufupi dunia tangu kuumbwa Mwenyezi Mungu (Allah) ameleta umma nyingi kabla ya umma huu.Wakileta jeruri huwa anawaangamiza na kuleta wengine.
Karibuni waliletwa bani Israel.Walipoanza kujisahau wakapewa nabii Mussa a.s awazindue na kuwaongoza.Walipofanya ufedhuli nabii Mussa a.s na watu wema wakaokolewa na waliobaki wakagharikishwa na wengine waliofuata mafunzo yale potofu na wanaoendelea kuyafuata wakalaaniwa..Hao ndio hawa mayahudi waliojikushanya kwenye ardhi za wapalestina.
Ama kwa waarabu baada ya kuwa walikuwa wapotofu sana,Allah akawapa heshima ya kuwatolea mtume miongoni mwao ambaye ni Muhammad s.a.w ili waongoze umma wa mwisho unaotakiwa wote uwe chini yake kwa imani ya kiislamu ile ile iliyokuwa dini ya mitume wote tangu Adam a.s
Baada ya kupewa heshima hiyo waarabu wakapewa muongozo tena katika maandishi ili wasitoke nje ya mstari.Muongozo huo ni kitabu cha Qur'an kisichokuwa na shaka ndani yake na ambacho hakiwezi kuingizwa maneno ya watu.
Miongoni mwa mafunzo ya kitabu hicho ambacho kiko katika lugha ya kiarabu ambayo ni lugha wanayoilewa vyema waarabu,ni kuhurumiana na kuacha kushirikiana na watu waliolaaniwa.
Ili kuwapa nguvu waarabu kusimamia mafunzo ya Qur'an na uislamu ubaki ndio imani ya wanadamu wote mpaka siku ya mwisho,waarabu wakapewa mali nyingi kwenye maeneo yao na wao pamoja na wengine walioukubali uislamu kuwekwa kwenye maeneo ya kistratejia kwa dunia nzima.
Kitu ambacho ni jeuri na kujisahau kwa waarabu ni kuacha mafunzo ya uislamu na kuacha watu waliolaaniwaa wafanye kama wanavyotaka kwa binaadamu wenzao na kwa ndugu zao.Zaidi ni kuacha kuwaunga mkono wale wanaopigana na maadui wa Allah kwa ajili ya kusimamia mafunzo na kulinda ishara za utukufu wake Allah (s.w).jIshara ya utukufu ni kama vile masjidul aLaqswa.
Kwa kipimo cha mafunzo ya uislamu,isingetarajiwa kuona waislamu 2.3 mil na wengine 4.7 milioni upande wa pili wakipigwa na kugaragazwa na mayahudi mbele ya macho yao.
Tofauti na hapo zamani,shida na mauwaji yanayofanywa na mayahudi yanatangazwa mubashara.Bado katika hali kama hiyo nchi zinazopakana na Gaza na Palestina kwa ujumla kila siku zinavyosogea na wao ndio wanazidisha ukimya.Mfano halisi ni Jordan,Misri na Saudi Arabia.
Allah s.w ni mwingi wa huruma lakini pia ni mwingi wa hasira na hua hana haraka wala papara katika maamuzi yake.Allah vile vile hana ushirika na viumbe vyake kwamba kundi fulani ni wateule wake.
Huwa anatoa fursa za kutosha za watu kushuhudia,kujitathmini na kujipanga kuchukua maamuzi.Kibianadamu muda huo huwa unaumiza sana lakini kwa vile ni fursa na yeye haathiriwi na maumivu ya kibinadamu basi muda huwa unaweza kurefuka.
Mwisho wa yote kuna ahadi ndani ya Qur'an kwamba iwapo watu waliopewa kheri watajisahau na kuipuuza basi anaweza akawanyang'anya watu kheri hizo na wakapewa watu wengine na hakuna atakayeweza kuzuia.
Akitaka atakuondoeni, enyi watu! Na awalete wengineo. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa hayo. (QUR 4:133)
Kwa ufupi dunia tangu kuumbwa Mwenyezi Mungu (Allah) ameleta umma nyingi kabla ya umma huu.Wakileta jeruri huwa anawaangamiza na kuleta wengine.
Karibuni waliletwa bani Israel.Walipoanza kujisahau wakapewa nabii Mussa a.s awazindue na kuwaongoza.Walipofanya ufedhuli nabii Mussa a.s na watu wema wakaokolewa na waliobaki wakagharikishwa na wengine waliofuata mafunzo yale potofu na wanaoendelea kuyafuata wakalaaniwa..Hao ndio hawa mayahudi waliojikushanya kwenye ardhi za wapalestina.
Ama kwa waarabu baada ya kuwa walikuwa wapotofu sana,Allah akawapa heshima ya kuwatolea mtume miongoni mwao ambaye ni Muhammad s.a.w ili waongoze umma wa mwisho unaotakiwa wote uwe chini yake kwa imani ya kiislamu ile ile iliyokuwa dini ya mitume wote tangu Adam a.s
Baada ya kupewa heshima hiyo waarabu wakapewa muongozo tena katika maandishi ili wasitoke nje ya mstari.Muongozo huo ni kitabu cha Qur'an kisichokuwa na shaka ndani yake na ambacho hakiwezi kuingizwa maneno ya watu.
Miongoni mwa mafunzo ya kitabu hicho ambacho kiko katika lugha ya kiarabu ambayo ni lugha wanayoilewa vyema waarabu,ni kuhurumiana na kuacha kushirikiana na watu waliolaaniwa.
Ili kuwapa nguvu waarabu kusimamia mafunzo ya Qur'an na uislamu ubaki ndio imani ya wanadamu wote mpaka siku ya mwisho,waarabu wakapewa mali nyingi kwenye maeneo yao na wao pamoja na wengine walioukubali uislamu kuwekwa kwenye maeneo ya kistratejia kwa dunia nzima.
Kitu ambacho ni jeuri na kujisahau kwa waarabu ni kuacha mafunzo ya uislamu na kuacha watu waliolaaniwaa wafanye kama wanavyotaka kwa binaadamu wenzao na kwa ndugu zao.Zaidi ni kuacha kuwaunga mkono wale wanaopigana na maadui wa Allah kwa ajili ya kusimamia mafunzo na kulinda ishara za utukufu wake Allah (s.w).jIshara ya utukufu ni kama vile masjidul aLaqswa.
Kwa kipimo cha mafunzo ya uislamu,isingetarajiwa kuona waislamu 2.3 mil na wengine 4.7 milioni upande wa pili wakipigwa na kugaragazwa na mayahudi mbele ya macho yao.
Tofauti na hapo zamani,shida na mauwaji yanayofanywa na mayahudi yanatangazwa mubashara.Bado katika hali kama hiyo nchi zinazopakana na Gaza na Palestina kwa ujumla kila siku zinavyosogea na wao ndio wanazidisha ukimya.Mfano halisi ni Jordan,Misri na Saudi Arabia.
Allah s.w ni mwingi wa huruma lakini pia ni mwingi wa hasira na hua hana haraka wala papara katika maamuzi yake.Allah vile vile hana ushirika na viumbe vyake kwamba kundi fulani ni wateule wake.
Huwa anatoa fursa za kutosha za watu kushuhudia,kujitathmini na kujipanga kuchukua maamuzi.Kibianadamu muda huo huwa unaumiza sana lakini kwa vile ni fursa na yeye haathiriwi na maumivu ya kibinadamu basi muda huwa unaweza kurefuka.
Mwisho wa yote kuna ahadi ndani ya Qur'an kwamba iwapo watu waliopewa kheri watajisahau na kuipuuza basi anaweza akawanyang'anya watu kheri hizo na wakapewa watu wengine na hakuna atakayeweza kuzuia.
Akitaka atakuondoeni, enyi watu! Na awalete wengineo. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa hayo. (QUR 4:133)