Mume wangu kantongoza


Pole sana umejiharibia menyewe umepoteza uwaminifu kwa mumeo, hapo alipo hakuamin hata chembe anakuona wewe ni kiruka njia anais kipindi yuko nje ya nchi ulimsaliti, ulichotaiwkukifanya ni kumweleza day one ile msg ilipoingia tu ungemshirikisha sasa hadi umfika pahali mmepangana mihadi unakuja kuomba ushauri hapa kwani wakati unatoka ulimuagaje ulimwambia unakwenda wapi.
 

Mie nlienda kwa sababu nilihisi kuna mchezo unachezwa hapo, na nilitaka kujiaminsha kama ninachokihisi ni kweli, and it turned out to be true
 
mwanamke wa kuitwa kwa sm na kufunga safari kwenda pasipo kujua nani kamwita ni m.a.l.a.y.a tu!

Hapo ndipo wengi tunapokosea, mimi huwa naamini katika kumjua mbaya wangu ni nani, kwani kama asingekuwa mume wangu ningemjua pia ni nani na hapo ndo ningejua ni hatua gani niichukue. Hata hivyo haya ni maoni huru na yamepokelewa kama mengine tuu. Asante kwa kuchangia
 

Najua sikutake precautions on that, lakini pia lengo langu halikuwa kuflirt na huyo mtu, lakini kwa kuwa nilianza kuhisi kuchezewa akili, nami ni mtu mzima maamuzi yangu tu ndo yalinisukuma kuonana naye. Asante kwa ushauri, nimeshajifunza sidhani kama ntarudia kosa kama hili
 
Eeh! We kaka/dada ukicheche wangu ni upi hapo jamani? Mie nlitamani tu kumjua huyo anaenitongoza kwa kudai kuwa mie ni mpenz wake. Na mind you huyu mtu alionekana kunifahamu vizuri. Sasa sijui kwa nini umenihukumu hivyo
Yani ukafunga safari mpaka Bustani ya Rose kwenda kumfahamu tu...? The intention was clearly there bana! ulitakiwa umpe mumeo hiyo number ili yeye ndio ampigie huyo mtongozaji
 
Yani kama me ndio mumeo nakumwaga mazima unaonekana ni kicheche.
Ukweli ndo huo huyu mwanamke ni kicheche kwani kama alitaka kukamata mwizi angemtonya mumewe wakamvizie huyu jamaa lakini yeye kaondoka kimya kimya na angekuta ni sio mumewe angejirusha.
 

Nilimshirikisha kabla hata ya kuonana naye, just at the beginning ya move yenyewe. Then nlipoanza kushtukia kuwa huenda ni yeye, nkamuuliza kama an line ya tigo akakataaa kabisa kuwa hana. Nkamwonesha na ile namba akasema haijui. Na baada ya hapo sms zikaendelea, nami nkasema huyo mtu ni lazima nimjue kwa sura. Hico ndicho kilisababisha niitikie mwito huo wa kukutana naye. Sasa sijui yeye afikiria nini kwa sababu hajasema anafikiria nini, ila alidai kuwa alitaka kunionesha jinsi wanawake wa mjini wanavyolaghaiwa
 
Yani ukafunga safari mpaka Bustani ya Rose kwenda kumfahamu tu...? The intention was clearly there bana! ulitakiwa umpe mumeo hiyo number ili yeye ndio ampigie huyo mtongozaji

Nimeshasema huko mwanzo kuwa Hiyo Garden iko jirani na ninapofanyia kazi. Na mume wangu nilimshirikisha toka awali akanpotezea, so mie ningefanyaje?
 
Ukweli ndo huo huyu mwanamke ni kicheche kwani kama alitaka kukamata mwizi angemtonya mumewe wakamvizie huyu jamaa lakini yeye kaondoka kimya kimya na angekuta ni sio mumewe angejirusha.

Na kama mume wangu ndo jamaa mwenyewe unadhani angekubali kukamatwa?
 
Nimeshasema huko mwanzo kuwa Hiyo Garden iko jirani na ninapofanyia kazi. Na mume wangu nilimshirikisha toka awali akanpotezea, so mie ningefanyaje?

Ok, asante kwa ufafanuzi ila binafsi sidhani kama ulifanya uamuzi wa busara kuitikia wito wa kwenda RG! though mumeo nae ana wivu na mitego ya kijinga

Dunia ya leo tukiachunguzana kihivyo unaweza pata vichomi tu
 
Ok, asante kwa ufafanuzi ila binafsi sidhani kama ulifanya uamuzi wa busara kuitikia wito wa kwenda RG! though mumeo nae ana wivu na mitego ya kijinga

Dunia ya leo tukiachunguzana kihivyo unaweza pata vichomi tu

Asante kwa kunielewa samora10. Unajua kila mwanadamu ana instincts zake, sasa inategemea weweumeumbwaje, mimi nikiwa na doubts na kitu huwa napenda nii clear kabisa. Na hapo ndo udhaifu wangu ulipo, huwa siifikirii hatari iliyo mbele hadi ninapokutana nayo. Anyways nshajifunza kutokana na makosa
 
Last edited by a moderator:
Na kama mume wangu ndo jamaa mwenyewe unadhani angekubali kukamatwa?

Hilo lisingehitajika maana ungeshamjibu kwamba "akukome huna muda na wapuuzi". Sasa we umeendekeza mpaka kufikoa kukubali miadi na bado unataka mumeo tu ndo aonekane mbaya.

Kaaazi kweli kweli.
 
Alitaka kuona kama wakati akiwa masomoni ulikuwa na mwingine; na hapo hata kama ulikuwa mkali mimi nimebaini kuwa kuwa ulikuwa na mtu. Kama huku na mtu kwa nini ukakubali kwenda Rose Garden kuonana na mtu usiyemfahamu ? Kwa nini hukumwambia .....samahani, naona wrong number.........?
 
Hilo lisingehitajika maana ungeshamjibu kwamba "akukome huna muda na wapuuzi". Sasa we umeendekeza mpaka kufikoa kukubali miadi na bado unataka mumeo tu ndo aonekane mbaya.

Kaaazi kweli kweli.

Hayo yote niliyafanya mpenzi Lizzy lakini kwa kuwa alikomaa nami, nami nkasema lazima nimfahamu ni nani. Na uzuri nlimuuliza husband kama namba hiyo anaijua na nikamweleza wazi kuwa kuna mtu anantumia sms za aina fulani, yeye akapotezea. Nkaona ngoja nideal nalo mwenyewe.

Na NOTE ME: sijataka mume wangu aonekane mbaya, bali nimeelezea kisa kilichonikuta. Hapa najibu kulingana na comment za watu, na kila mtu ana maoni na mafikirio yake tofauti na mwenzake, nawe mchango wako ni wa muhimu. Unakuwa my dear haya yatakukuta nawe utadeal nayo kwa jinsi yako
 
Nilimshirikisha kabla hata ya kuonana naye, just at the beginning ya move yenyewe. Then nlipoanza kushtukia kuwa huenda ni yeye, nkamuuliza kama an line ya tigo akakataaa kabisa kuwa hana. Nkamwonesha na ile namba akasema haijui

okay, kwa maelezo haya ya ziada it looks like ulijitahidi kuplay your part

alidai kuwa alitaka kunionesha jinsi wanawake wa mjini wanavyolaghaiwa

na yeye huwa anawalaghai kwa njia hiyo? otherwise alijuaje?
 
bombu hapa sasa nimekuelewa vizuri zaidi. Nilidhani hukumshirikisha kabisa, kumbe alikuwa anajua kinachoendelea. Mumeo naye namlaumu kwa mtego aliotumia, kwani ungeweza kumuumiza hata yeye mwenyewe pia. Kuaminiana ndani ya ndoa ni jambo la muhimu sana. Vinginevyo mnaweza kujikuta mnapoteza muda kwa mambo yasiyo na tija. Kama ilivyotokea hiyo siku, mliacha shughuli zenu kwenda kushughulikia jambo ambalo lingeweza kuzua ugomvi na pengine kusambaratisha nyumba. Kwa mara nyingine nakupa pole kwa uchungu ulio nao, I know how it feels. Unatamani afungue moyo wako asome mwenyewe jinsi ulivyo mwaminifu kwake. Vumilia tu, baada ya muda uchungu utakwisha, itabaki historia. Hata hivyo, kama ulivyosema, jitahidi kufuta doubts alizonazo kwako. Kwa jinsi anavyokupenda (nimemsoma from your story) atakuamini na hatokutega tena. Mwombe sana Mungu akuvushe salama kwenye machungu uliyonayo. Najua umejifunza kitu kikubwa sana kutokana na tukio hilo. Nakutakia furaha, amani na upendo wa kudumu katika ndoa yako. Barikiwa!
 
Last edited by a moderator:


Asante dada Maamuma, you are a true friend. Ujue hata mie nligundua kosa baada ya kuwa mambo yamekwisha. Ndo maana nkaamua niisimulie hii story kwani kuna watu wengine watajifunza humu. Asante kwa ushauri wako na busara zako, I am inspired. Ubarikiwe
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…