Si unajua tena wadada mnapenda kutongozwa, kudanganywa, kupewa maneno matamu! Mi nnaona huyo alikuwa anaplay role yake kama mwanamke! As long as hakukubali, basi yupo kwenye safe side!Mbona yeye kakubali kutongozwa? Wote ni wale wale hivyo akubali tu.
Si unajua tena wadada mnapenda kutongozwa, kudanganywa, kupewa maneno matamu! Mi nnaona huyo alikuwa anaplay role yake kama mwanamke! As long as hakukubali, basi yupo kwenye safe side!
Lizzy, naona unajaribu kujitetea sana, yaeleka ushapigwa tukio kama hili..lol!
Karibu tena bombu, siku nyingi sijakusikia.
Kama ulifahamu kuwa kuna kamchezo, ingekuwa vizuri kama ungemshrikisha huyo mume wako cuz kama aliamua kukufanyia hivyo, basi ujeue hakuamini na kuvitu alitaka kuprove!
Yani kama me ndio mumeo nakumwaga mazima unaonekana ni kicheche.
Sasa ulighafilika nini? unajuwa maana ya kughafilika lakini au umeliweka tu hilo neno?
Kughafilika ni kusahau, sasa wewe hapo ulimaanisha ulighafilika (sahau) nini?
Sasa ulighafilika nini? unajuwa maana ya kughafilika lakini au umeliweka tu hilo neno?
Kughafilika ni kusahau, sasa wewe hapo ulimaanisha ulighafilika (sahau) nini?
Hii inasikitisha inaonekana na ww macho juu. Kama kweli mwaminifu utapangaje na mtu ambaye huna uhusiano naye na wala humjui? Cha kushangaza na ww umekwenda, ungekuta buzi kweli si ungeachia mchezo? usituzuge kwa kuwa umekuta mumeo ndiyo unajibalaguza.
Acha kabisa huo mchezo wewe ni mke wa wenyewe. Na nyumba hujengwa na heshima ya mke kama hujui.
Naombeni jamani tusaidiane hili. Mume wangu alikuwa masomoni nje ya nchi kwa muda wa miaka miwili, amerudi hivi karibuni. Aliporudi kanunua line ya Airtel ambayo ndio ninayoifahamu. Mie sikujua kumbe mwenzangu kanunua line ya tigo, ambayo hakunambia. Sasa siku moja usiku nashangaa msg inaingia:-
YEYE: Darling mambo vipi? Naona tangu jamaa yako arudi umenitosa
MIE: Mbona mie sikufahamu?
YEYE: Hee! kumbe tuko wengi tunaoiba? Njoo basi tukutane hapa Rose garden
Na mengine meeengiiiii.
Mie nkaushtukia mchezo hapo, ila nkasema wacha nione hii movie mwisho wake utakuwaje. Tukapanga hadi kukutana, bahati nzuri sikuwa na papara. ALHADULILAH! mara nafika eneo la tukio ni yeye huyooo!
Nilighafilika kwa kweli, ingawa hisia zangu zishantuma kuwa kama sio yeye basi ameweka watu wanitrace. Hivi ingekukuta wewe mwana JF mwenzangu, ungeliamuaje hili?
hakuamini hata kidogo! Sasa inabidi na wewe ujifanye kama mnaachana hivi??
Karibu tena bombu, siku nyingi sijakusikia.
Kama ulifahamu kuwa kuna kamchezo, ingekuwa vizuri kama ungemshrikisha huyo mume wako cuz kama aliamua kukufanyia hivyo, basi ujeue hakuamini na kuvitu alitaka kuprove!
kweli wewe ni bombu huoni hiyo ni bahati kuona mmeo anakupenda na chengine kwanini uende kwa mtu usiemjua au na wewe ni wale wale..
Bahati nzuri huyo mume wa bombu siyo mimi, Kama ni mimi Power angekuja eneo la tukio angefikia kipondo kikali sana ambacho asingekisahau maisha yake yote.Mwanamke mwaminifu kwenye ndoa yake hawezi kufanya mawasiliano ya namna hii mpaka anaenda eneo la tukio.Kuna wasiwasi wa uaminifu wako kwenye ndoa yako bombu!