Mume wangu hanifikishi kileleni : Ushauri

majibu mepesi kwa maswali magumu sana. Hapa suluhisho haliwezi kupatikana kama chanzo cha tatizo hakijulikani. Saa nyingine hata huyo mwanaume hajui shida ni nini. Inawezekana kuna mambo yanaendelea kwenye ubongo wake uliolala bila yeye kujua - inawezekana akiwa mtoto alishaambiwa ngono ni kitu kibaya kichafu sana, sasa ukubwani huku bila yeye kujua anafanya chap chap ili aondokane na uchafu. Labda kuna kitu dhamira yake inamshitaki, labda msisimko wa mahusiano umezimia, labda ana mchepuko kwa hiyo kwa mkewe anatimiza wajibu, labda kabla hajaoa alikuwa na addiction ya ngono na sasa imeisha, labda msongo wa mawazo, labda nguvu tu zimepotea akila vizuri zitarudi, labda alibakwa na hausigeli utotoni, labda, labda,,,,,,,,,,,,,,,,,,,, All in all tumia busara usimlalamikie, ila akikataa kutoa ushirikiano katika kutatua tatizo fanya uamuzi utakaokufeva.
 
Back
Top Bottom