mume mkopaji

mume mkopaji

nduu

Member
Joined
Aug 6, 2011
Posts
12
Reaction score
11
Nina jirani yangu kanijia kwa masikitiko kwamba mumewe amekuwa ni anayependa kukopa mno. Anadai kwamba tokea wakiwa wachumba amekuwa akimkopa yeye, akikopa kwenye makampuni ya wakopeshaji nk. Tabia hii haijabadilika hadi hivi leo wameoana zaidi ya muongo mmoja. Kinachomuumiza ni kwamba hajawahi kumrudishia hata centi moja. Hizo hela akikopa hata hajui anachofanyia manake mahitaji yote ya nyumba ni mama ndio anatimiza. wote wawili wana kazi na mshahara hautofautiani sana. je afanyeje kumsaidia huyu kidume na tabia yake ya ukopaji?
 
makubwa!wenye ndoa zao waje wajibu maana mimi nikisema naonekana mbaya bure
 
Huyu bwana ni NJEMBA SURUALI.....Kama wako pamoja zaidi ya MUONGO mmoja ina maana Mama kayazoea....Ndiyo style ya ndoa yao hao....
 
Unafiki wake tu mtu anapewa mkopo hadi na taasisi na hafanyi tangibles bado na yeye anaendelea kumpa tu pesa!!!!!

Mshauri ampe ATM card kabisa ili kuondoa udhia
 
Yani tokea wachumba alikuwa anaiyona hali hiyo na bado akang'ang'ania kuolewa? inamaana alishakubaliana na mwenendo wa huyo mume wake............. mimi nisingeweza kwenye mahusiano tu naachia ngazi.....
 
Mh! Kwani we nduu umetumwa utangaze? Au ndo umbea? Mambo yao we yanakuhusu nini?
 
Last edited by a moderator:
Hapo mkopo kwa collateral ya penzi aka ndoa! Hata aongeze interest mara 800 hakuna return hapo!

dawa ni ku quite tu hiyo biashara!
 
Anadai kwamba tokea wakiwa wachumba amekuwa akimkopa yeye, akikopa kwenye makampuni ya wakopeshaji nk.

Huu ndio ulikuwa wakati sahihi wa kujaribu kurekebisha tabia hiyo...

Kitendo cha kukubali kuolewa na mwanaume huyo binafsi nakitafsiri kuwa huyo mwanamke alikubali tabia na kasoro zote za mumewe...ikiwemo hii ya kupenda kukopa.
 
mama kazoea waache tu na maisha yao mwishowe ushauri uonekane mbaya. baba matumizi mabovo.
 
Mh! Kwani we nduu umetumwa utangaze? Au ndo umbea? Mambo yao we yanakuhusu nini?

Mimi nimeombwa ushauri, nikajua kuna ma-great thinkers watanisaidia kunipa mikoba ili nikamshauri huyu mama. au hapo kuna ubaya? Kumbuka hii ni ndoa, ni very sensitive issue. mwaga ushauri basi!
 
^^
Miaka kumi ndo anataka ushauri leo!! Fanya mambo yako,,ndoa ina mengi ni zaidi ya inavyoonekana.
Urefu wa kina cha maji aujuae chura.
^^
 
Mimi najua muongo mmoja ni sawa na miaka 18 au nimekosea? Nadhani matatizo yao watayamaliza wao ni watu wazima
 
Nina jirani yangu kanijia kwa masikitiko kwamba mumewe amekuwa ni anayependa kukopa mno. Anadai kwamba tokea wakiwa wachumba amekuwa akimkopa yeye, akikopa kwenye makampuni ya wakopeshaji nk. Tabia hii haijabadilika hadi hivi leo wameoana zaidi ya muongo mmoja. Kinachomuumiza ni kwamba hajawahi kumrudishia hata centi moja. Hizo hela akikopa hata hajui anachofanyia manake mahitaji yote ya nyumba ni mama ndio anatimiza. wote wawili wana kazi na mshahara hautofautiani sana. je afanyeje kumsaidia huyu kidume na tabia yake ya ukopaji?

Jamani kila siku jambo hili linaongelewa hapa, 'USIMKOPESHE BOYFRIEND/MUME hela' atakuona uko matawi ya juu, na majukumu yake yote anakuachia wewe. Hivi kwa nini tunawashobokea sana hawa watu? ndio MAPENZI au tuna shida sana ya kuolewa? Mpaka mtu unaamua KUMUHONGA mume hivi inakuwaje? embu nielewesheni labda mimi ndio nina matatizo!

Huyo mume/mchumba ANAHONGWA hela, anakuwa kafanya nini?
 
khaaa! siku akithubutu tu hata kuniomba hela nadai talaka, chake changu changu changu banaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom