Mume, mipaka yake kwa mkewe mwisho wapi

Mume, mipaka yake kwa mkewe mwisho wapi

Suprise

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2012
Posts
2,696
Reaction score
1,063
Morning MMU,
Naombeni mawazo yenu kuhusu binamu yangu, kaolewa 6 yrs iliyopita,
Hapo wanzo 2 yrs , shem alikua mkarimu , ana mapenzi na ndugu, anshiriki kwenyeshida na raha, after some time akabadika cjui ni ubize, ikitokea ishu ya mkusanyiko, anshiriki mkewe peke yake, mkewe anamwambika kaniwakilishe asi hadi misibani anaka kuwailishwa, hali imekua mbaya now, sasa hataki mkewe atoke tena, iktokea ni msba basi awe blood sis or bro ndo aruhusu na akisafiri hata kuzika basi ageuze kesho yake mapema,vinginevyo anaambiwa abaki hukohuko.

Majuz ulitokea msiba wa mtoto wa babaake mkubwa mwanza, basi akagomewa kwend mbaya zaid mkewe akaomba kaka yake amuombee ruhusa mmewe katoa maneno machafu eti mbali mkewe hawez kwenda.

Bi dada kafosi kaenda, msbani wamumuwekea kikao abaki na mumewe asiwashirikishe kwa lolote na wao hawatamsumbua.Kurudi mume kamwambia last warning akienda tena atachagua.

Hakuna msaada wowote toka ka wake, mama mkwe kamwambia umeolewa mskilize mume, tumshauri jamani
 
Inaonekana mume ana wivu sana, ndio ameolewa lakini anapaswa pia kushiriki mambo ya Familia. Mume hajawahi kufiwa huyo, ngoja afiwe yeye....
 
Spiritually; huyo ni shetani anataka kuharibu ndoa yao. Hivyo ni vyema wakaenda kwa viongozi wa dini wakaombewa.


Kwa hali ya kawaida; kuna mawili:-

1. Chanzo yaweza kua huyo Dada; i mean, kuna vitabia vichafu kavionyesha kwa mumewe: huyo dada huenda alimuonyesha mumewe matendo sio ya kiaminifu.

-Wanamme wako sensitive sana; Kwa anayejua maana ya ndoa, anaweza kukuonya na kukutaka uache tabia hizo. Na hapo ndio hua ni mtihani mkubwa pindi mwanamke akianza tabia chafu.Kozi hua inachukua hata miaka zaidi ya 10

-Ukiwachunguza kwa ukaribu utakuta kuna mambo mengi machafu sana yanaendelea ndani. No peace...kutokuelewana etc

Pili: Huenda tatizo likawa kwa mwanamme; Mambo ya michepuko kama mnavyosema. Au tu, frustration za maisha na kama mwanamke anamdomo ndio mambo yanakua ovyo kabisa.

#Ushauri hapo juu utasaidia. Bado mapema sana kukata tamaa.

Mwanamke awe mpole...wote wawe wapole; Instead ya kutafuta pesa...watafute suruhisho la amani ya ndoa yao na wamweke Yesu awe mchungaji wao katika ndoa yao.
 
Nianze na suala na uhuru wa mwanandoa

Kimsingi ndoa ni makubaliano ya watu wawili na hata huo uhuru unapoanzia na kuishia ni kutegemea na wao wamekubaliana vipi kwa ni sio uniform,jambo moja linaweza kuwa ni lazima wanandoa fulani washirikiane lakini jambo lilelile kwa wanandoa wengine hawashirikiani

Hivyo kwenye suala hilo ni kutegemea na mlivyokubaliana lakini kuolewa au kuoa sio mwisho wa kufanya mambo yako binafsi au kutokuwa na "praivesi"

Nikija kwenye situation ya huyo rafiki yako ni kwamba huenda huyo jamaa kuna jambo limemfanya abadilike au halivyokuwa zamani ilikuwa ni acting tu kama vile ambavyo wengi wanafanya siku hizi ili wawanase watu wanaotaka kuwanasa kwenye mahusiano

Inaweza kuwa amegundua mkewe tabia yake sio nzuri na huko misibani na kwenye vikao ndiko anakpoatia mwanya wa kufanya mambo yake na njia aliyotumia ni kumzuia kwenda huko kwani kawaida watu tunatofautiana namna ya kulitatua tatizo na wengine wanatatua jambo kwa njia za ajabu sana na mojawapo ni hii,huyo shemeji yako huenda hiyo njia ndiyo aliyoiona njema kutatua tatizo hili [kama ni hilo]

Lakini pia huenda amegundua kuwa kuna watu wanamfukuzia mkewe na njia aliyochagua ni kumzuia nyumbani kwa sababu kitendo cha kujua hayo kimemfanya akose kujiamini kabisa

Lakini lililo kubwa sana na ninalodhani ndilo tatizo lake ni kuwa ana tabia ile ya mfumo dume na ubabe ambayo wanayo wanaume wengi kidogo,wanataka kuonesha Uanaume wao kwa ubabe zaidi kuliko uwajibikaji kwenye familia wanataka mkewe asiende mahali bila ruhusa yao,kwa kifupi asifanye chochote bila ruhusa yake,wanataka wake zao wawe kama wale mbuzi wanaofugwa,hawawezi kwenda popote bila uangalizi
Hao wana tatizo la kimalezi na ili kuwaondoa hapo ni hadi wapate ushauri wa kisaikolojia.Kitu kingine cha kustaajabisa ni kuwa wanakuwa wanajua kabisa tabia hiyo sio nzuri na ndio maana wanaificha mwanzoni ili wawapate wanaowahitaji na wakisha wapata huact kwa muda kisha wanarudia halizao za zamani na hapo ndoa huwa chungu sana,watu hawa hua ni mafundi wakubwa wa ku act na mhusia ni vigumu sana kuwajua

Huyo dada anatakiwa aoneshe msimamo na ajisimamie maana huyo jamaa atamfanya kabati au stuli ya kukaa ndani tu,amwambie namna tabia hiyo asivyoipenda na ikiwezekana atafute mtu ambae huyo mumewe anamuheshimu na ajaribu kumshirikisha kumshauri mumewe

Maisha hayawezi kwenda kwa aina hiyo!
 
Huyo mwanaume tabia yake ni hiyohiyo hata kama anekuwa hajaoa so ndoa isionekane ni mkosi hakuna kitu inanipa raha na furaha kama ndoa!unakuwa na mtu anakuona kama baba wewe ndo kila kitu halafu na wewe unampenda kuliko hata nafsi yako.....hongereni sana wana ndoa wenzagu.....si vizuri mtu aishi peke yake nitamtafutia msaidizi wa kufanana naye.
 
hizo ndoa za kubembelezana kwenye upuuzi me ndo siziwezi kabisa na nashukuru Mungu nae alinipa mwanaume wa kwendana na mimi, sasa mume gani huyo? hiyo ndoa au kibarua, manake mwanaume huyo ana masharti ya kibosi na si kindoa, me ningekuwa yeye ningefanya yooooote yanipasayo kijamii na kibinafsi alimradi sivunji sheria wala simkosei heshima alafu yeye mume aamue KUSUKA au KUNYOA. Yani nikisiaga ndoa za namna hiyo huwa nahisi hasira sana
 
SCOAN
awe mpole, nini suluhisho la ndoa yake, au mahusiano na nduguze
 
Asante mkuu Eiyer, ila huyo shem kadekezwa sana kwao mpaka mamaake hawez mwambia chochote
 
Suprise: Suluhisho ya yote uliyoniuliza lipo katika maaumuzi yao ya dhati. Kuamua kujikabidhi kwa Yesu, wakabidhi ndoa yao kwa Yesu na kumfanya awe Mwokozi wa maisha yao.


-Pili: Upendo wa kweli utawaweka Huru!


#Love is the greatest weapon!
 
Last edited by a moderator:
Sio ushenzi. Unapochangia.....lazima ujue maana na tofauti katika NDOA NA UCHUMBA.

Hapa nitashangaa sana kuona mtu ambae anasikia sikia tu kuhusu ndoa na akachangia lolote.


#Ndoa ni kitu kizuri sana na kitakatifu; But shetani akikiingilia ni shidaaa
 
Mipaka ya mume ni kwenye chupi ya mkewe akishaivua tu badi mipaka inaishia hapo.nothing more period!!!
 
Mipaka ya mume ni kwenye chupi ya mkewe akishaivua tu badi mipaka inaishia hapo.nothing more period!!!

kama mpaka upo kwenye chupi tu, kuna tofauti gani na michepuko sasa
 
Back
Top Bottom