Mume kutandika kitanda.

Mume kutandika kitanda.

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,707
Reaction score
1,729
Siku moja tulikuwa tukijadiliana na mama mmoja (mke wa mtu), mfanyakazi mwenzangu, masuala ya jamii na alishangazwa kusikia jamaa yetu mmoja akisema yeye huwa akitandika kitanda takriban siku zote anapoamka wa mwisho. Je wana JF wenzangu hii mnaonaje?
 
Anapoamuka wa mwisho, huenda mke amekwisha ondoka kwenda kibaruani ama sehemu yoyote ya kutafuta riziki ya kila siku, what wrong then
 
ameshasema anatandika akiwa wa mwisho kuamka,sioni tatizo hapo
 
Me nahisi kuna watu mnawahi/miliwahi kuoa kwa sababu zisizo za msingi.

mtu akichoka kufanya yafuatayo ndio husema anataka kuoa.
  • kufua nguo
  • Kuosha vyombo
  • kusafisha nyumba
  • kutandika kitanda n.k

Najiuliza tu,mnaoa ili wake zenu wawe working machines au?
Binafsi sipendi kufua,sipendi kuosha vyombo,lakini hizo sio
sababu za kunifanya niwahi kuoa.

Kuona kwako ni ajabu kwa jamaa kutandika kitanda nahisi mkeo
ana taabu kweli kweli,sidhani hata kama BOXER YAKO UNAIFUA.
 
Kilichonistaajabisha ni yule mama kushangaa kusikia mume akitandika kitanda!!!!!!!

huyo atakuwa ni wa kizazi cha enzi za Mama wa taifa,kama anatandika kiroho safi bila kushurutishwa ni mwanaume wa kipekee anaehitaji kuthaminiwa kwani ni among very few!!!!!!!mke sio punda bali msaidizi bhana.
 
Me nahisi kuna watu mnawahi/miliwahi kuoa kwa sababu zisizo za msingi.

mtu akichoka kufanya yafuatayo ndio husema anataka kuoa.
  • kufua nguo
  • Kuosha vyombo
  • kusafisha nyumba
  • kutandika kitanda n.k

Najiuliza tu,mnaoa ili wake zenu wawe working machines au?
Binafsi sipendi kufua,sipendi kuosha vyombo,lakini hizo sio
sababu za kunifanya niwahi kuoa.

Kuona kwako ni ajabu kwa jamaa kutandika kitanda nahisi mkeo
ana taabu kweli kweli,sidhani hata kama BOXER YAKO UNAIFUA.
Mkuu mie hufanya takriban kila kitu pale nyumbani, ila kilichotustaajabisha ni huyo mama kumsikia mmoja wetu akitandika kitanda. Yawezekana mila zake zinamkataza. Mama yule ni wa kanda ya ziwa.
 
huyo atakuwa ni wa kizazi cha enzi za Mama wa taifa,kama anatandika kiroho safi bila kushurutishwa ni mwanaume wa kipekee anaehitaji kuthaminiwa kwani ni among very few!!!!!!!mke sio punda bali msaidizi bhana.
Mkuu, mila zetu je?
 
Me nahisi kuna watu mnawahi/miliwahi kuoa kwa sababu zisizo za msingi.

mtu akichoka kufanya yafuatayo ndio husema anataka kuoa.
  • kufua nguo
  • Kuosha vyombo
  • kusafisha nyumba
  • kutandika kitanda n.k

Najiuliza tu,mnaoa ili wake zenu wawe working machines au?
Binafsi sipendi kufua,sipendi kuosha vyombo,lakini hizo sio
sababu za kunifanya niwahi kuoa.

Kuona kwako ni ajabu kwa jamaa kutandika kitanda nahisi mkeo
ana taabu kweli kweli,sidhani hata kama BOXER YAKO UNAIFUA.


uko sahihi kabisa...ndo maana ndoa za siku hizi hazidumu
 
kutandika kitanda hakuna ubaya wowote ila sema watanzania tulishakariri kuwa kutandika kitanda ni mwanamke
 
Hiyo imetulia mkuu,siku hizi kila kitu ni kusaidiana na ndivyo maisha yanavyotakiwa yaende isipokuwa kusaidiana kunyonyesha tu ndo haikubaliki.Thanks@
 
Hata akitandika kila siku poa tu.. As long as anapenda na yuko comfortable.



Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom