Mume anahitajika 36+

Inaonekana wanywa pombe wengi sana ehhh, na wanapata shida mno, ouk, dada umeweka uzi wako, nimeupenda sana, nina uhakika kuna siku utarudi humu na kushukur kwamba umepata mume Jf, kama ni Mkristo mwwnye imani, nina uhakika kilio chako kakisikia Mungu, na atajibu, ila majibu ya Mungu anaweza akakupa nje na hayo uliyomention, kaa kujiandaa ktk hilo, Mungu anasema tunayowaza sisi, yeye anakuwa tofauti na mawazo yetu, anaweza kukuletea hata mvuta bangi lkn akaifaa sana familia hyo,ningekuwa sijaoa ningekutafuta, japo mm 32 but umri sio kitu kwangu, kilichonivutia sana ni hao watoto wawili Wadada, hapo ndo nazimia kabisa, napenda sana watoto hasa wa kike, kwahyo ningekupendea kupitia watoto wako.
Nashangaa wanaokimbia kulea watoto, hao ni baraka sana ktk maisha. Mungu akutafutue wa haja yako.
Asante dear
 
Ungemvumilia tu mwenzio maana mapungufu ni ya wanadam. Chamsingi ni kukomaa tu na hali yako. Maana hata huyo unayemtafuta anaweza akafanya cha juu zaidi ya huyo uliye mwacha. ILA kama huwezi kuvumilia basi ni bora uishi peke yako tu. Ushauri tu.
 
Habari wana JF,

Natafuta mume aliye tayari kuwa nami katika hali zote, mimi nina umri wa miaka 34, mwalimu wa shule moja ya sec mjini Mwanza.

Nilibahatika kuolewa lakini bahati mbaya nilitendwa vibaya na nikaamua kuachia ngazi, nina watoto wawili wa kike na ni mkristo.

Mume nimtakaye awe na sifa zifuatazo awe na miaka 36+, rangi yoyote, kabila lolote, dini mkristo, asiwe mnywa pombe wala mvuta sigara, ajue thamani ya mke na awe tayari kulea watoto wangu.

Mwenye uhitaji kama wangu karibu PM tuyajenge, astalavista..
Nyie si Hua mna ndoa moja unataka mume gani tena na mtafunga ndoa wapi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom