kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,224
- 1,685
Mwanamke mkazi wa kijiji cha Matui, Wilayani Kiteto, Mkoani Manyara ameponea chupuchupu kuuawa baada ya mume wake kumchoma na chuma cha moto sehemu zake za siri, kutokana na wivu wa mapenzi.
Mwanamke huyo alifanyiwa kitendo hicho juzi usiku kwenye kijiji hicho, baada ya mume wake kumtuhumu kuwa ana uhusiano wa mapenzi na msaidizi wao wa nyumbani.
Akizungumza kwenye Hospitali ya wilaya ya Kiteto juzi, wakati akipatiwa matibabu mwanamke huyo alisema hivi "kwa sasa anasikia maumivu makali sana".
Alisema alipofanyiwa kitendo hicho alipoteza fahamu kwa muda mrefu, kwani alitokwa na damu nyingi na alizinduka baada ya kufikishwa hospitalini hapo iliyopo umbali wa kilomita 32 kutoka nyumbani kwake.
Alongeza kuwa kabla ya kufanyiwa kitendo hicho, kila mara mume wake alikuwa anamweleza kuwa amesikia tetesi kuwa ana uhusiano wa mapenzi na msaidizi wa kazi hivyo atamfanyia kitu ambacho hatakisahau.
"Siku ya tukio hilo, alikoka moto akachukua nondo ya kuweka alama kwenye ng'ombe, akaniambia "ingia ndani mke mwenzako anakuita", nilipoingia ndani naye akaingia na kufunga mlango akaniingizia hiyo nondo ya moto", alisema.
Daktari wa hospitali hiyo Godfrey Mbise alisema mwanamke huyo amepata kilema cha maisha baada ya kufanyiwa kitendo hicho cha kikatili, kwani ameachiwa majeraha sehemu zake za siri, mapajani na mgongoni.
Hata hivyo, Diwani wa Kata ya Matui, Kidawa Athuman alisikitishwa na kitendo cha Polisi wa Kituo cha Matui kutochukua jambo hilo kwa uzito.
Athuman alisema askari hao wanashindwa kumchukulia hatua mwanaume aliyefanya kitendo hicho, kutokana na nguvu kubwa ya uchumi aliyonayo.
…Source by Mwananchi - Jumapili, Januari 13, 2013
Mwanamke huyo alifanyiwa kitendo hicho juzi usiku kwenye kijiji hicho, baada ya mume wake kumtuhumu kuwa ana uhusiano wa mapenzi na msaidizi wao wa nyumbani.
Akizungumza kwenye Hospitali ya wilaya ya Kiteto juzi, wakati akipatiwa matibabu mwanamke huyo alisema hivi "kwa sasa anasikia maumivu makali sana".
Alisema alipofanyiwa kitendo hicho alipoteza fahamu kwa muda mrefu, kwani alitokwa na damu nyingi na alizinduka baada ya kufikishwa hospitalini hapo iliyopo umbali wa kilomita 32 kutoka nyumbani kwake.
Alongeza kuwa kabla ya kufanyiwa kitendo hicho, kila mara mume wake alikuwa anamweleza kuwa amesikia tetesi kuwa ana uhusiano wa mapenzi na msaidizi wa kazi hivyo atamfanyia kitu ambacho hatakisahau.
"Siku ya tukio hilo, alikoka moto akachukua nondo ya kuweka alama kwenye ng'ombe, akaniambia "ingia ndani mke mwenzako anakuita", nilipoingia ndani naye akaingia na kufunga mlango akaniingizia hiyo nondo ya moto", alisema.
Daktari wa hospitali hiyo Godfrey Mbise alisema mwanamke huyo amepata kilema cha maisha baada ya kufanyiwa kitendo hicho cha kikatili, kwani ameachiwa majeraha sehemu zake za siri, mapajani na mgongoni.
Hata hivyo, Diwani wa Kata ya Matui, Kidawa Athuman alisikitishwa na kitendo cha Polisi wa Kituo cha Matui kutochukua jambo hilo kwa uzito.
Athuman alisema askari hao wanashindwa kumchukulia hatua mwanaume aliyefanya kitendo hicho, kutokana na nguvu kubwa ya uchumi aliyonayo.
…Source by Mwananchi - Jumapili, Januari 13, 2013