Muhimu: CHADEMA WAWEKEZE KWENYE NGOME ZAO

mozze

Senior Member
Aug 27, 2010
185
28
Kwa kufuatilia matukio tu nadhani CDM waanze kufikiria kuwa na Makao makuu au Kuamishia shughuli za Chama katika mikoa ambayo ni Ngome. Kikubwa waangalie influence ya hayo maeneo...Mkoa kama Mwanza, Mbeya, Shinyanga Arusha nadhani ni strategic kuliko kung'ang'ania Dar es slaam.
Kwa sababu ni gharama sana kuwafikia wananchi ya mikoani kutoka Dar, ni vyema CDM wafikirie kuweka shughuli za kichama karibu na ngome zao, hii itarahisisha sana Harakati za kukiimarisha chama.
Naamini kutoka mkoani ni rahisi kuiteka Dar es salaam mana ni mji ulio na mchanganyiko sana...kama CDM itakubalika na watu wa kanda ya Ziwa, hawa watu wapo Dar es salaam pia so ni rahisi kuingia, lakini watu wa mkoani wakifikiri CDM na viongozi wao wanakimbilia Dar wataona sio chama cha kuwatetea mana viongozi wanajilimbikiza Dar.
Hii ni strategy ambayo nadhani itakuwa ngumu kwa vyama vingi kufuata....na tukubali kuwa kwenye mfumo wa vyama vingi kila chama kina ngome yake.....so CDM wasijisahaukuwekeza kwenye ngome yao....

Alternative kwa vile CDM sera yao ni ya majimbo basi waanze sasa kubadili mfumo wa chama na kuwe na CDM kila kanda ambayo shughuli zake za kisiasa zitakuwa huru bila kuingiliwa na makao makuu....so tuwe na CDM nyanda za juu, CDM kanda ya Ziwa etc.....hii pia itasaidia kuwafanya wananchi wa maeneo hayo wajisikie kuimiliki na kumiliki sera kuliko maamuzi yote kufanyika Dar na kutumwa mikoani....
 
Unajua 2015 inaweza kuonekana mbali lakini ni very soon, ili kuweza kuhakikisha chama hakiingii gharama kubwa wakati wa uchaguzi ni lazima wajipange fresh. Kipindi hiki hakuna pressure sana so ni wakati muafaka kujichimbia kwa supporters.
Kutengeneza loyalty na supporters ndio njia pekee itakayoingiza CDM Ikulu....
kwenye business strategy kuna term muhimu... organization must identify and go for strategies that can give it sustainable competitiveness. Na ili uwe na hiyo nguvu hutakiwi kuwa vuguvugu, you must choose your extreme which you can perform better than competitor .... ukifuata strategy ya mshindani wako utaishia kuwa follower tu na it is unlikely ku-overtake.
So CDM go a step further...msiishie kuelimisha umma, bali pia wekezeni kwenye mbinu (strategy).
 
Chadema kuwa na ngome imara DAr ni ndoto kwa sababu ya udini wao, hata wao wanalijua hili ndo maana hata nguvu yao ni yakusuasua dara. wazo lakuwa ngome kwenye majimbo ni zuri ila hili unalosema kila jimbo liwe na mamlaka yao ni sawa na kukiua chama kwani ni rahisi kupoteza mwelekeo ikiwa baadhi ya majimbo, viongozi wao hawana msimamo, ie ni rahisi kununulika au kuwa na makundi katika chama kitu ambacho kwa mtazamo wangu nakiona kama hatari. Ila kwa mengi big YES.
 
Chadema kuwa na ngome imara DAr ni ndoto kwa sababu ya udini wao, hata wao wanalijua hili ndo maana hata nguvu yao ni yakusuasua dara. wazo lakuwa ngome kwenye majimbo ni zuri ila hili unalosema kila jimbo liwe na mamlaka yao ni sawa na kukiua chama kwani ni rahisi kupoteza mwelekeo ikiwa baadhi ya majimbo, viongozi wao hawana msimamo, ie ni rahisi kununulika au kuwa na makundi katika chama kitu ambacho kwa mtazamo wangu nakiona kama hatari. Ila kwa mengi big YES.
Huo udini mnauna nyie tu na Dar siyo mji wa watu wa dini moja tu
 
Back
Top Bottom