Ndugu wanajukwaa, Waswahili husema kwamba Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni. Kumbe ni kweli! Sikuwahi kujua kuwa Hospitali ya Agha Khan ni bora kuliko ile ya Taifa, Muhimbili. Kitendo cha kumhamisha DCI Manumba kutoka katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwenda Agha Khan kimenifanya niamini kuwa hali ya Muhimbili kihuduma ni mbaya sana. Madaktari walipogoma miezi michache iliyopita, moja ya madai yao ilikuwa ni kudai mazingira bora ya kazi kama vile kuwa na vifaatiba vya kisasa. Reaction ya serikali ilikuwa ni kupuuza madai yao. Je, kwa nini serikali haitaki kuboresha huduma za afya nchini? Kwa uelewa wangu, napata majibu haya: kukosekana kwa uzalendo miongoni mwa viongozi wetu, kuwepo kwa ufisadi, na kwamba hospitali zetu ni kwa ajili ya walalahoi kama mimi, kwa sababu wao wana uwezo wa kwenda kutibiwa katika hospitali kama Agha Khan na nchi za nje. Au taifa letu ni maskini kama wanavyosema wao? Kama ni kweli, mbona tuna rasilimali lukuki nchini? Iweje Hospitali ya Agha Khan (hospitali binafsi) iwe na huduma bora kuliko ile ya Taifa inayomilikiwa na serikali? Ipi iliyo na nguvu, taasisi binafsi au serikali? Kama taasisi ina nguvu kuliko serikali, hivi Watanzania tunaweza kujivuna kuwa tuna serikali makini? Naomba majibu yenu, siasa tuweke pembeni! Waingereza husema, 'One finger can not crush a louse'. Katika nchi yetu, mambo ni kinyume kabisa. Serikali inakusanya kodi nyingi sana, lakini hali si shwari kabisa. Tafadhali, naomba mawazo yenu!