Mufti Simba awasha moto

Status
Not open for further replies.

Mzito Kabwela

JF-Expert Member
Nov 28, 2009
18,857
7,618
Mufti Simba awasha moto
Tangu September 20, 2013, na | Imesomwa
mara 278 | Haina maoni
*Amvaa Sheikh Kilemile, amwambia afuate
sheria
Na Eben-Ezery Mende
MUFTI wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania
(Bakwata), Issa Shaban bin Simba amesema
yeye si msanii kama anavyoshutumiwa na
Mwenyekiti wa Kamati ndogo ya Mazungumzo
kati ya Waislamu na Serikali, Sheikh Suleiman
Kilemile.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu
jana, Mufti Simba alisema shutuma
anazotupiwa zinatokana na malalamiko yake
kwa Serikali kuhusu kupuuzia suala la
Mahakama ya Kadhi.
Kutokana na hali hiyo, Mufti Simba alisema
yeye yupo sahihi na kwamba anayemshutumu
atumie sheria badala ya kulalamika kwenye
vyombo vya habari.
Simba alisema anachofahamu ni kwamba
kupatikana kwa Kadhi hakuhitaji ushirikishwaji
wa taasisi zote za Kiislamu na kubainisha kuwa
kama kuna kosa lililofanyika sheria ndiyo
itatengua kitendawili hicho na si malalamiko.
“Huyo Sheikh Kilemile kama anadhani
kulalamika ni dawa waulizwe Waislamu kuhusu
Mahakama ya Kadhi na mimi sitaki kuendeleza
mvutano kwenye vyombo vya habari,” aling’aka
Mufti Simba.
Kauli ya Simba imekuja baada ya Sheikh
Kilemile kudai kuwa Mufti huyo ni msanii katika
kupata Mahakama ya Kadhi.
Sheikh Kilemile alidai hatua ya kumuona Mufti
Simba msanii imekuja baada ya kujitokeza
akiilaumu Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa
kupuuza maoni ya Waislamu ya kutaka
kuanzishwa kwa mahakama hiyo.
Alisema lawama zilizotolewa na Mufti Simba
zinashangaza kwa sababu zaidi ya miaka mitatu
iliyopita, Rais Jakaya Kikwete alimuagiza Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda awasiliane na Bakwata ili
kumtaka Simba aunde jopo la masheikh kutoka
taasisi mbalimbali za Kiislamu ili liwe chombo
cha kuwakilisha Waislamu wote nchini.
Sheikh Kilemile alifafanua kuwa baada ya
kufanyika kwa vikao vingi chini ya uenyekiti wa
Mufti na vingine na Pinda mchakato huo
ulionesha kufikia hatua nzuri.
Alisema kikao cha mwisho cha jopo hilo chini ya
waziri mkuu kilihudhuriwa na baadhi ya
watendaji wa Serikali na mawaziri kadhaa
wakiwemo Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias
Chikawe, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina
Kombani, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais
(Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira, Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na
Bunge) William Lukuvi na Mwanasheria Mkuu
wa Serikali, Jaji Frederick Werema. “Kwa vile
mahakama za kadhi zinapatikana pia katika nchi
nyingine za kisekyula kama Uingereza, India,
Kenya na hata Zanzibar, Wasira alimshauri
waziri mkuu upatikane ujumbe utakaokwenda
kutembelea nchi hizo na utakaokusanya
wajumbe kutoka serikalini na jopo la masheikh
kujionea taratibu za uendeshaji wa mahakama
za kadhi katika nchi hizo ili utakaporudi nchini
uweze kuelekeza jinsi ya kuziendesha
mahakama hizo hapa nchini.
“Pinda alikubali na kuibariki rai hiyo. Aliamuru
upande wa jopo la masheikh utoe wajumbe
watatu na upande wa Serikali wajumbe wawili.
Ilikubaliwa kuwa gharama za kupeleka ujumbe
huo Uingereza, India, Kenya na Zanzibar zilipwe
na Ofisi ya Waziri Mkuu. Ujumbe huo ulitakiwa
uwe umekamilisha ziara hizo kabla ya Aprili,
2013,” alisema.
Sheikh Kilemile alidai kabla ya kufanikisha
hayo, Mufti Simba alipuuza yale maazimio ya
kikao hicho na badala yake aliamua kuitisha
mkutano wa viongozi wa Bakwata mjini
Dodoma na kutangaza jina la kadhi wake mkuu
pamoja na wasaidizi wake bila kushauriana na
jopo la masheikh lililoteuliwa kushughulikia
mchakato mzima wa kupatikana Mahakama ya
Kadhi.


Source: Jamba Leo
 
bakwata ni tawi la ccm lilianzishwa lengo kuwakandamiza waslamu wasiwe na maendeleo waslamu maendeleo awana sababu ya bakwata angalia wa kristo wana vyuo vingi ,shule nyingi,mahospitali mengi kwa waslam ivi vitu very few
 
bakwata ni tawi la ccm lilianzishwa lengo kuwakandamiza waslamu wasiwe na maendeleo waslamu maendeleo awana sababu ya bakwata angalia wa kristo wana vyuo vingi ,shule nyingi,mahospitali mengi kwa waslam ivi vitu very few

Hebu acha kutania Bakwata wewe..Bakwata ina shule,hospitali n.k Hebu tutajie shule na hospital answar sunna wamejenga.Misikiti tu kujenga shida kazi kutaka kuipora iliyopo ya BAKWATA KILA WAKATI WANAPANDA JUU YA MAPAA NA VISUARLI VYAO VIFUPI kutaka kupora misikiti.u-maamuma ulio nao wewe hata imamu atoke Maka hawezi kukusaidia wewe.
 
Hebu acha kutania Bakwata wewe..Bakwata ina shule,hospitali n.k Hebu tutajie shule na hospital answar sunna wamejenga.Misikiti tu kujenga shida kazi kutaka kuipora iliyopo ya BAKWATA KILA WAKATI WANAPANDA JUU YA MAPAA NA VISUARLI VYAO VIFUPI kutaka kupora misikiti.u-maamuma ulio nao wewe hata imamu atoke Maka hawezi kukusaidia wewe.
Ndugu yangu katika imani tafadhali rejea uzi humu jamvini ulioletwa na Mohamed Said "KWA NINI HATUITAKI BAKWATA" kabla ya ku~comment
 
Ndugu yangu katika imani tafadhali rejea uzi humu jamvini ulioletwa na Mohamed Said "KWA NINI HATUITAKI BAKWATA" kabla ya ku~comment

Hicho kitabu nilishakisoma ni cha historia.Kinaongelea mambo yaliyopita .History is the study of past events) na mimi si mtumwa wa historia tofauti na nyie mnaopigia kelele BAKWATA kwa kuwa bado ni watumwa wa historia.Hayo yalishapita tugange yajayo saa hizi kila taasisi iko huru kujenga shule hospitali n.k jengeni si wakati wa kupigia kelele taasisi ingine kwa yaliyopita.Kwanza hakuna anayelazimisha waislamu wawe chini ya taasisi moja.Hata wakristo wana mabaraza kibao yenye imani tofauti lakini hayagombani.Shida iko kwenye mabaraza ya kiislamu kutwa kutukana BAKWATA si mtulie mpange mambo yenu huko kwenye mabaraza yenu.

Utaing`ang`ania historia ikufunge hadi lini? mwandika kitabu huyo alishakufa ,wengi aliowataja humo ndani wawe akina nyerere na wengineo waislamu na wakristo waliotajwa humo ni marehemu walishajifia miaka wewe bado tu umeng`ang`ana.WEWE ni mtumwa wa historia cha kufanya chukua hicho kitabu cha mohamed Said KICHOME MOTO halafu kaa na wenzio muongee future yenu mnaanzaje kuijenga kuanzia hapo.Vinginevyo utabakia kusema mohamed Said aliandika aliandika? una-quote maandiko yake utafikiri ni QURAN hiyo ni shirki katika uislamu.Watoto wengi wa kiislamu wanaharibiwa kwa kufunzwa kuwa watumwa wa historia wakati wakristo hawahangaiki na kuwa watumwa wa historia wanasonga mbele kutafuta maendeleo_Ondoka kwenye kijiwe cha historia tafuta maendeleo.
 
Ndomana kila baada ya muda huwa mnabadilisha agano ili kwenda na wakati au yesu kila kipindi huleta muongozo mwengine tafauti na waawali
 
Hebu acha kutania Bakwata wewe..Bakwata ina shule,hospitali n.k Hebu tutajie shule na hospital answar sunna wamejenga.Misikiti tu kujenga shida kazi kutaka kuipora iliyopo ya BAKWATA KILA WAKATI WANAPANDA JUU YA MAPAA NA VISUARLI VYAO VIFUPI kutaka kupora misikiti.u-maamuma ulio nao wewe hata imamu atoke Maka hawezi kukusaidia wewe.

Takbir!! Takbir!!
FaizaFoxy, Ritz, kahtaan, Boko haram
 
Last edited by a moderator:
Hicho kitabu nilishakisoma ni cha historia.Kinaongelea mambo yaliyopita .History is the study of past events) na mimi si mtumwa wa historia tofauti na nyie mnaopigia kelele BAKWATA kwa kuwa bado ni watumwa wa historia.Hayo yalishapita tugange yajayo saa hizi kila taasisi iko huru kujenga shule hospitali n.k jengeni si wakati wa kupigia kelele taasisi ingine kwa yaliyopita.Kwanza hakuna anayelazimisha waislamu wawe chini ya taasisi moja.Hata wakristo wana mabaraza kibao yenye imani tofauti lakini hayagombani.Shida iko kwenye mabaraza ya kiislamu kutwa kutukana BAKWATA si mtulie mpange mambo yenu huko kwenye mabaraza yenu.

Utaing`ang`ania historia ikufunge hadi lini? mwandika kitabu huyo alishakufa ,wengi aliowataja humo ndani wawe akina nyerere na wengineo waislamu na wakristo waliotajwa humo ni marehemu walishajifia miaka wewe bado tu umeng`ang`ana.WEWE ni mtumwa wa historia cha kufanya chukua hicho kitabu cha mohamed Said KICHOME MOTO halafu kaa na wenzio muongee future yenu mnaanzaje kuijenga kuanzia hapo.Vinginevyo utabakia kusema mohamed Said aliandika aliandika? una-quote maandiko yake utafikiri ni QURAN hiyo ni shirki katika uislamu.Watoto wengi wa kiislamu wanaharibiwa kwa kufunzwa kuwa watumwa wa historia wakati wakristo hawahangaiki na kuwa watumwa wa historia wanasonga mbele kutafuta maendeleo_Ondoka kwenye kijiwe cha historia tafuta maendeleo.

Mkuu umemaliza!
 
Hicho kitabu nilishakisoma ni cha historia.Kinaongelea mambo yaliyopita .History is the study of past events) na mimi si mtumwa wa historia tofauti na nyie mnaopigia kelele BAKWATA kwa kuwa bado ni watumwa wa historia.Hayo yalishapita tugange yajayo saa hizi kila taasisi iko huru kujenga shule hospitali n.k jengeni si wakati wa kupigia kelele taasisi ingine kwa yaliyopita.Kwanza hakuna anayelazimisha waislamu wawe chini ya taasisi moja.Hata wakristo wana mabaraza kibao yenye imani tofauti lakini hayagombani.Shida iko kwenye mabaraza ya kiislamu kutwa kutukana BAKWATA si mtulie mpange mambo yenu huko kwenye mabaraza yenu.

Utaing`ang`ania historia ikufunge hadi lini? mwandika kitabu huyo alishakufa ,wengi aliowataja humo ndani wawe akina nyerere na wengineo waislamu na wakristo waliotajwa humo ni marehemu walishajifia miaka wewe bado tu umeng`ang`ana.WEWE ni mtumwa wa historia cha kufanya chukua hicho kitabu cha mohamed Said KICHOME MOTO halafu kaa na wenzio muongee future yenu mnaanzaje kuijenga kuanzia hapo.Vinginevyo utabakia kusema mohamed Said aliandika aliandika? una-quote maandiko yake utafikiri ni QURAN hiyo ni shirki katika uislamu.Watoto wengi wa kiislamu wanaharibiwa kwa kufunzwa kuwa watumwa wa historia wakati wakristo hawahangaiki na kuwa watumwa wa historia wanasonga mbele kutafuta maendeleo_Ondoka kwenye kijiwe cha historia tafuta maendeleo.

mkuu ungesema tu kitabu cha Mohamed Said kinawadhalilisha waislam, hiyo si defn ya History. Pongezi ewe muislam kwa kujitambua. Adui mkuu wa waislam ni waislam wenyewe
 
Last edited by a moderator:
bakwata ni tawi la ccm lilianzishwa lengo kuwakandamiza waslamu wasiwe na maendeleo waslamu maendeleo awana sababu ya bakwata angalia wa kristo wana vyuo vingi ,shule nyingi,mahospitali mengi kwa waslam ivi vitu very few

waislam jitambueni kuwa adui yenu ni shetani na si wakristo.
 
Hicho kitabu nilishakisoma ni cha historia.Kinaongelea mambo yaliyopita .History is the study of past events) na mimi si mtumwa wa historia tofauti na nyie mnaopigia kelele BAKWATA kwa kuwa bado ni watumwa wa historia.Hayo yalishapita tugange yajayo saa hizi kila taasisi iko huru kujenga shule hospitali n.k jengeni si wakati wa kupigia kelele taasisi ingine kwa yaliyopita.Kwanza hakuna anayelazimisha waislamu wawe chini ya taasisi moja.Hata wakristo wana mabaraza kibao yenye imani tofauti lakini hayagombani.Shida iko kwenye mabaraza ya kiislamu kutwa kutukana BAKWATA si mtulie mpange mambo yenu huko kwenye mabaraza yenu.

Utaing`ang`ania historia ikufunge hadi lini? mwandika kitabu huyo alishakufa ,wengi aliowataja humo ndani wawe akina nyerere na wengineo waislamu na wakristo waliotajwa humo ni marehemu walishajifia miaka wewe bado tu umeng`ang`ana.WEWE ni mtumwa wa historia cha kufanya chukua hicho kitabu cha mohamed Said KICHOME MOTO halafu kaa na wenzio muongee future yenu mnaanzaje kuijenga kuanzia hapo.Vinginevyo utabakia kusema mohamed Said aliandika aliandika? una-quote maandiko yake utafikiri ni QURAN hiyo ni shirki katika uislamu.Watoto wengi wa kiislamu wanaharibiwa kwa kufunzwa kuwa watumwa wa historia wakati wakristo hawahangaiki na kuwa watumwa wa historia wanasonga mbele kutafuta maendeleo_Ondoka kwenye kijiwe cha historia tafuta maendeleo.

Hakika haya maneno hayakutoka kwako ila kwa Roho wa Mungu aliyeko ndani yako! Na kama wewe ni Mwislamu na Mwenyezi akakujalia wewe na waislamu wenzio kuwaza hivi bila shaka Tanzania na dunia ingebaki kuwa kisiwa cha amani. Aione FaizaFoxy na washirika wake!
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom