Muafaka unaokuja Zanzibar ni mwendelezo wa ulaghai

Muafaka unaokuja Zanzibar ni mwendelezo wa ulaghai

Mpita Njia

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2008
Posts
6,999
Reaction score
1,187
Upo msemo wa Kiingereza ambao tafsiri yake inasema; “kurudia kufanya jambo lile lile, kwa namna ile ile, huku ukitarajia matokeo tofauti, ni uendawazimu.”

Sitaki kusema kuwa Zanzibar imefikia hatua hiyo linapokuja suala la muafaka. Lakini imefika wakati sasa tujiulize hii miafaka (sijui kama huo ndio wingi wa neno muafaka) ambayo imekuwa ikijirudia muda mfupi kila baada ya uchaguzi mkuu haiashirii huu msemo wa Kiingereza niliounukuu?

Inashangaza kuwa kila baada ya uchaguzi kunakuwa na mgogoro wa kisiasa Zanzibar unaotokana na malalamiko kuhusu uchaguzi. Siku zote malalamiko yanatolewa na vyama vya upinzani kuwa uchaguzi haukuwa huru na wa haki. Hapa, vyama hivyo vya upinzani (kilianza CUF na sasa kuna ACT Wazalendo) vinatishia kususia Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK).

Kila mara, mgogoro huo unafuatiwa na vikao baina ya Chama Cha Mapinduzi (ambacho ndicho kinalalamikiwa) na chama cha upinzani. Kila mara mazungumzo haya huzaa makubaliano (yaite muafaka) na baada ya hapo chama cha upinzani hurudi kujiunga kwenye SUK.

Lakini mara tu baada ya kujiunga, malalamiko hutolewa tena na chama hicho cha upinzani kikieleza kasoro kadhaa katika uendeshaji wa SUK.

Unapokaribia uchaguzi, chama hicho cha upinzani kinaweza kuja na tishio la kususia uchaguzi lakini suluhu hutafutwa na hatimaye kinashiriki uchaguzi.

Wakati wa kampeni kunawezaa kuwa na malalamiko kutoka chama hicho cha upinzani kuhusiana na kutotendewa haki na na Tume ya Uchaguzi (ZEC). Lakini hatimaye chama hushiriki uchaguzi.

Mara tu baada ya uchaguzi, malalamiko ya chama cha upinzani kuhusu kutotendewa haki katika uchaguzi huibuka na mzunguko wa majadiliano, makubaliano, malalamiko mapya, majadiliano tena, makubaliano hujirudia mpaka unapofika uchaguzi mwingine.

Kila mara chama cha upinzani Zanzibar hutoa malalamiko na madai yale yale. Kila mara suluhu hutafutwa kwa njia ile ile. Kila mara Suluhu huwa ni ile ile.

Kila mara tunashuhudia mzunguko huu ukijirudia huku wahusika wakuu, walalamikaji na wanaolalamikiwa wakifanya yale yale lakini wakiueleza umma kuwa wanatarajia kuwa wakati huo kutakuwa na matokeo tofauti.

Nadhani sasa umefika wakati wanasiasa wa Zanzibar watupumzishe kidogo. Huu mtindo wao wa kufanya mambo yale yale, kwa namna ile ile na kutuahidi kuwa kutakuwa na matokeo tofauti, unapaswa kufika mwisho.

Inashangaza sana kuwa watu wazima, ambao wanaaminiwa na wananchi wengi, wanatufanyia mambo haya mchana kweupe.

Hapa majuzi tumesikia tena kuwa baada ya ACT Wazalendo kususia kujiunga kwenye SUK baada ya kulalamikia uchaguzi w mwaka jana, yamefanyika mazungumzo na sasa suluhu inakaribia kupatikana na kama inavyotarajiwa ACT kitajiunga kwenye SUK.

ACT Wazalendo kinasisitiza kuwa mufaka utakaopatikana utaweka mbele maslahi ya Zanzibar. Hii nayo si kauli mpya. Kila mara vyama vya upinzani vilipolalamika na muafaka kufikiwa tuliambiwa kuwa muafaka huo ni kwa maslahi ya Zanzibar.

Kama ni hivyo, inashangaza sana kuwa maslahi ya Zanzibar ni kuendeleza mzunguko wa malalamiko – majadiliano - makubaliano na kurudi tena kwenye malalamiko!
 
Wanaotaka Muafaka ni ACT Wazalendo kwasbabu moja kubwa, kuficha nyuso zao
Kumekuwa na 'miafaka' mingi ikiwemo uliozaa Marekebisho ya Katiba ya Zanzibar 2010 , kuundwa kwa SUK
Kabla ya hapo kulikuwa na muafaka uliozaa Tume ya uchaguzi huru wakiwemo CUF a.k.a ACT

ACT walishindwa chaguzi ikiwemo iliyobaragazwa na Salimu Jecha kwa kutumia vyombo vya Dola
Ni wazi, katika vyama vya Upinzani CUF ambayo ni ACT kwa sehemu kubwa wana uzoefu mkubwa wa kuteswa

CHADEMA waliwashsuri kutoshiriki Tume ya Mkandara ili kuzidisha shinikizo la Katiba. ACT kwasababu za ''kijamii'' wakashirikia. Matokeo yake suala la Katiba likapoteza nguvu. ACT walijua huruma na hisani itawabeba mbeleni

2025 ACT waliambiwa katika mazingira yaliyopo ni ndoto kushinda kwa kuzingatia yaliyotokea 2020 na 2015. Kwamba hakukuwa na uchaguzi hata CCM wanakiri. ACT wakapuuzia wakiweka matumaini ya hisani na fadhila

ACT waliamini viongozi kutoka Bara wanawakandamiza ili kuitawala Zanzibar, hivyo 2025 hakukuwa na kikwazo.
Historia ni mwalimu mzuri, hakuna kilichobadilika, ACT wamepigwa vibaya Zanzibar !

Aibu inawakumba ACT! Watawaambia nini Wanachama wao kwamba wamepigwa!!
Kwanini hawakuwasikiliza CHADEMA kudai mabadiliko ya jumla? Kwanini hawakujifunza kutoka yaliyopita?

Katika kuficha aibu, ACT wakataka muafaka wakati Wawakilishi wao wapo ndani ya Baraza la wawakilishi
Hakuna muafaka ni namna ya kutoka katika lindi la aibu! wanatafuta pakutokea kwa lugha ya mjini

Kinachoendelea ni namna ya kupewa nusu mkate ambayo ACT wamezoea, a.k.a SUK na kufungua makongamano, kuwakilisha mazishi n.k
 
Back
Top Bottom