Al Watani
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 20,489
- 30,520
Yule jamaa hakuwa mtu wa kawaida aiseeBila kusahau kuliua jiji la DSM ambalo ndilo kubwa lao la Upinzani. Hakika ndugu yule alikuwa mtu wa chuki na visasi. Hivi kwa maendeleo ya mkoa wa DSM na uchangiaji wake kwenye pato la Taifa unaweza kulivunja? Jiji la miaka nenda Rudi? Jiji la historia? Akaacha Ilala iwe jiji kwa kuwa Ikulu iko Manispaa ya Ilala. Maeneo ya Kinondoni, Ubungo, Kawe, Kibamba kote ni Fire. Kigamboni alimanusura. Mimi ni .CCM lakini kwa kuwa tuliruhusu upinzani sioni sababu ya kuwachukia maana hata ndugu zetu na majirani wapo ambao ni Wapinzani. Je tutawachukia na kuwatenga? Muhimu huwa tunapingana kwa hoja tukikutana na hatujawahi kuwa maadui. Nimefurahi kuwa Mh. Rais sasa watakaa meza moja na wenzetu Wapinzani. Mwisho wa siku sote ni Watanzania.