Mtumishi anadai: "Nalipwa mshahara bila kufanya kazi kwasababu ya Maige"

Huyu kijana mdogo ametokea kwenye ubunge na kuwa waziri ndani ya miaka miwili tu ameshakua tajiri na utajiri unaokimbizana na wale mafisadi kina Lowasa na kina Chenge! hii haiwezekani lazima achukuliwe hatua kali kwa mujibu wa sheria ikiambatana na viboko 12 siku anaingia jela na siku anatoka jela anapata viboko 12 akamwadisie mkewe!
 
Huyu kijana mdogo ametokea kwenye ubunge na kuwa waziri ndani ya miaka miwili tu ameshakua tajiri na utajiri unaokimbizana na wale mafisadi kina Lowasa na kina Chenge! hii haiwezekani lazima achukuliwe hatua kali kwa mujibu wa sheria ikiambatana na viboko 12 siku anaingia jela na siku anatoka jela anapata viboko 12 akamwadisie mkewe!

Watakuwa wanaumuonea tu, mbona mawaziri wengine hawakuchukuliwa hatua ? wamuche tu asepe na wengine watakaokuja pia watachukuwa chao mapema watasepa ! hii TAnzania bhana ! SHAMBA LA BIBI ! kila atakae kuja kula na aje ! Rukhsa ! mradi usivunje sharia angala waweza KUZIPINDA !
 
Pole sana kwa kupata likizo yenye malipo,vp ulikuwa kimya mpaka ripoti ya kamati ya bunge imnase maige?na vp? Dili za wanyama pori washkaji wanakushirikisha au likizo mpaka huko?
 
kwa hiyo unataka usilipwe mshahara?



Ooppph kuhusu kuvuna hata ukiwa msituni wakiamua kuvuna watavuna tu........
 
Pole sana kwa kupata likizo yenye malipo,vp ulikuwa kimya mpaka ripoti ya kamati ya bunge imnase maige?na vp? Dili za wanyama pori washkaji wanakushirikisha au likizo mpaka huko?

ahahahah! Hakuna kama wabongo.
 
Maige kazi anayo. itabidi awe smart kubaki salama kwenye hii political system ya Tanzania
 
Ndugu Mwenyekiti wa jukwaa hili,

Mimi naitwa Toto M. Kassi, Afisa Misitu Wilaya ya Same. Tarehe 23.12.2010 Mheshimiwa Waziri Ezekiel Maige, tukiwa kwenye Msitu wa Hifadhi Asilia ( Nature Reserve) wa Serikali Kuu wa Chome Wilayani Same, bila kujali misingi ya utawala bora, Waziri Maige alinisimamisha kufanya kazi za misitu na Mkurugenzi wa Misitu akaniandikia barua tarehe 07.01.2011 kutekeleza amri ya Waziri Maige.

Hivyo basi, kuanzia tarehe 07.01.2011 hadi hii leo naendelea kulipwa mshahara bila kufanya kazi. Msituni. watu wanaofanya uharibifu ikiwamo uvunaji haramu wa misitu ya asili bado wanaendelea na vitendo vyao hivyo. Sababu ya kusimamishwa kazi kwangu ni kwamba
nimezuia wavunaji misitu na wachimbaji madini ambao wana maslahi na Mkuu wa Wilaya ya Same na Mheshimiwa Maige mwenyewe.

Mimi sio mtumishi wa Wizara yake. Nipo Tamisemi ingawa kitaaluma ni Afisa Misitu. Ukweli ajira yangu haiko kwake, Waziri
amekurupuka kwa nia mbaya. Labda kosa langu ni kutetea rasilimali za umma zisihujumiwe. Vinginevyo sina kosa lolote na ndio maana mpaka sasa kujua nini iwe hatma yangu kiajira mbali ya kunilipa mshahara kila mwezi bila kufanya kazi. Nimefika Wizarani mara mbili. Ukweli pale Wizarani wanamwogopa sana Maige. Kila mtu anaogopa kushughulikia malalamiko yangu. Waziri anawatisha na wengine
kuwasimamisha kazi hovyo kwa maslahi yake.

Ndugu Mwenyekiti, Malalamiko yangu yako Tamisemi na Idara Kuu ya Utumishi. Tume ya Utumishi wa Umma na wizarani kwenyewe. Sijui hatima yangu, lakini ukweli mpaka sasa nalipwa mshahara bure, bila ya kufanya kazi. Ni mimi, Toto Kassi Mjumbe aliyewekwa
kijiweni na Waziri Maige ( Niko tayari kutoa ushahidi wa niliyoyaeleza hapa;

0784 715977)

Inatisha!
 
Ulicho fanya ndio ujasiri tunaokosa Watanzania wengi. Tunaogopa kufa, na kusahau kuwa hakuna njia kila nafsi itaonja mauti. Dawa yao ni kujitoa na kusema dhahiri. Hapa naona ni vema ukaweka pia maelezo yako polisi, ili likitokea lolote la kutokea umma utawahukumu. Usiogope maana Mungu ya pamoja nawe.

Kwa hawa ambao wanadhulumu mali zetu kwa kiasi hiki, tusipowashitaki, tusipowafilisi, tusipowakalia kooni hadi watapike walichomeza itakuwa ni aibu yetu na laana yetu.

Katiba yetu iweke dhahiri kipengele cha kuwashtaki na kuwafilisi viongozi wote wenye madaraka ya umma pindi wataposhindwa kuthibitisha wapatavyo mali zao. Maige ikiwa haya yana ukweli, basi ninatamka bila hofu wala huruma juu yako * Laana na iwe juu yako na watoto wako, na watoto wa watoto wako* kwa kuibia wanyonge na kudhulumu wasio na nafasi.
 
Mkuu wa wilaya ya Same yaani Ibrahim Marwa au? Naye anavuna misitu asili! Tutafika ila tukiwa tumevimba mitoki!
 
Waziri wala mkurugenzi wa misitu hana mamlaka ya kumsimamisha mtumishi wa local govt. Non of them is a disciplinary authority. Kwa case he DED ndiye disciplinary authority.
Barua ya kukusimamisha kazi ni sawa na barua toka mtani wako au girl friend. Endelea na kazi kabla ded hajakufukuza.
 
Serikali ya kihuni,kitapeli nk hii,eti waziri anamuhonga mhudumu wa ndege $3000 ili apate kukubaliwa kimapenzi tu!mkuu si kua watufafanulie tu walipataje hizo mali bali walitakiwa kufikishwa mahakamani kama kina mramba,kufungwa na kutaifishwa pia!ila kwa kua hawa ni washkaji wa mzee wa visasi basi tusitarajie ilo

ndio faida ya kuchagua wazinzi! tukome sasa
 
. . . Mimi naitwa Toto M. Kassi, Afisa Misitu Wilaya ya Same. Tarehe 23.12.2010 Mheshimiwa Waziri Ezekiel Maige, tukiwa kwenye Msitu wa Hifadhi Asilia ( Nature Reserve) wa Serikali Kuu wa Chome Wilayani Same, bila kujali misingi ya utawala bora, Waziri Maige alinisimamisha kufanya kazi za misitu na Mkurugenzi wa Misitu akaniandikia barua tarehe 07.01.2011 kutekeleza amri ya Waziri Maige.

Hivyo basi, kuanzia tarehe 07.01.2011 hadi hii leo naendelea kulipwa mshahara bila kufanya kazi. Msituni. watu wanaofanya uharibifu ikiwamo uvunaji haramu wa misitu ya asili bado wanaendelea na vitendo vyao hivyo. Sababu ya kusimamishwa kazi kwangu ni kwamba nimezuia wavunaji misitu na wachimbaji madini ambao wana maslahi na Mkuu wa Wilaya ya Same na Mheshimiwa Maige mwenyewe. Mimi sio mtumishi wa Wizara yake.

Nipo Tamisemi ingawa kitaaluma ni Afisa Misitu. Ukweli ajira yangu haiko kwake, Waziri amekurupuka kwa nia mbaya. Labda kosa langu ni kutetea rasilimali za umma zisihujumiwe. Vinginevyo sina kosa lolote na ndio maana mpaka sasa kujua nini iwe hatma yangu kiajira mbali ya kunilipa mshahara kila mwezi bila kufanya kazi. Nimefika Wizarani mara mbili. Ukweli pale Wizarani wanamwogopa sana Maige. Kila mtu anaogopa kushughulikia malalamiko yangu.

Waziri anawatisha na wengine kuwasimamisha kazi hovyo kwa maslahi yake. Ndugu Mwenyekiti, Malalamiko yangu yako Tamisemi Idara Kuu ya Utumishi. Tume ya Utumishi wa Umma na wizarani kwenyewe. Sijui hatima yangu, lakini ukweli mpaka sasa nalipwa mshahara bure, bila ya kufanya kazi. Ni mimi, Toto Kassi Mjumbe aliyewekwa kijiweni na Waziri Maige ( Niko tayari kutoa ushahidi wa niliyoyaeleza hapa; 0784 715977
 
Kwenye barua ya kusimamishwa umeandikwa charge zipi ambazo ndo basis ya kusimamishwa? Lakini kama mwajiri wako umesema ni tamisemi inakuaje mkurugenzi wa misitu ambaye yupo wizara ya malialisi awe na mamlaka ya kukusimmisha? Je mwajiri wako alisemaje? Kama vipi tuwekee madocument hapa tuyaone.
 
daaah kashfa nyingine hii...sasa nenda ITV au gazeti la mwananchi kaseme haya kama UNAUSHAIDI NA UNAYO SEMA. mkuu wa wilaya ya same alieshirikiana na maige kukunyanyasa bado ni mkuu wa wilaya same?
 
Kwenye barua ya kusimamishwa umeandikwa charge zipi ambazo ndo basis ya kusimamishwa? Lakini kama mwajiri wako umesema ni tamisemi inakuaje mkurugenzi wa misitu ambaye yupo wizara ya malialisi awe na mamlaka ya kukusimmisha? Je mwajiri wako alisemaje? Kama vipi tuwekee madocument hapa tuyaone.
namba ya simu hiyo hapo, nenda hewani kama unataka details zaidi.
 
Back
Top Bottom