( Madai haya yamefikishwa na mtumishi wa umma kwenye http://mjengwablog.com)
Ndugu Mwenyekiti wa jukwaa hili,
Mimi naitwa Toto M. Kassi, Afisa Misitu Wilaya ya Same.
Tarehe 23.12.2010 Mheshimiwa Waziri Ezekiel Maige, tukiwa kwenye Msitu wa Hifadhi Asilia ( Nature Reserve) wa Serikali Kuu wa Chome Wilayani Same, bila kujali misingi ya utawala bora, Waziri Maige alinisimamisha kufanya kazi za misitu na Mkurugenzi wa Misitu akaniandikia barua tarehe 07.01.2011 kutekeleza amri ya Waziri Maige.
Hivyo basi, kuanzia tarehe 07.01.2011 hadi hii leo naendelea kulipwa mshahara bila kufanya kazi. Msituni. watu wanaofanya uharibifu ikiwamo uvunaji haramu wa misitu ya asili bado wanaendelea na vitendo vyao hivyo.
Sababu ya kusimamishwa kazi kwangu ni kwamba nimezuia wavunaji misitu na wachimbaji madini ambao wana maslahi na Mkuu wa Wilaya ya Same na Mheshimiwa Maige mwenyewe.
Mimi sio mtumishi wa Wizara yake. Nipo Tamisemi ingawa kitaaluma ni Afisa Misitu. Ukweli ajira yangu haiko kwake, Waziri amekurupuka kwa nia mbaya. Labda kosa langu ni kutetea rasilimali za umma zisihujumiwe. Vinginevyo sina kosa lolote na ndio maana mpaka sasa kujua nini iwe hatma yangu kiajira mbali ya kunilipa mshahara kila mwezi bila kufanya kazi.
Nimefika Wizarani mara mbili. Ukweli pale Wizarani wanamwogopa sana Maige. Kila mtu anaogopa kushughulikia malalamiko yangu. Waziri anawatisha na wengine kuwasimamisha kazi hovyo kwa maslahi yake.
Ndugu Mwenyekiti,
Malalamiko yangu yako Tamisemi Idara Kuu ya Utumishi. Tume ya Utumishi wa Umma na wizarani kwenyewe. Sijui hatima yangu, lakini ukweli mpaka sasa nalipwa mshahara bure, bila ya kufanya kazi.
Ni mimi, Toto Kassi
Mjumbe aliyewekwa kijiweni na Waziri Maige
( Niko tayari kutoa ushahidi wa niliyoyaeleza hapa; 0784 715977)
Ndugu Mwenyekiti wa jukwaa hili,
Mimi naitwa Toto M. Kassi, Afisa Misitu Wilaya ya Same.
Tarehe 23.12.2010 Mheshimiwa Waziri Ezekiel Maige, tukiwa kwenye Msitu wa Hifadhi Asilia ( Nature Reserve) wa Serikali Kuu wa Chome Wilayani Same, bila kujali misingi ya utawala bora, Waziri Maige alinisimamisha kufanya kazi za misitu na Mkurugenzi wa Misitu akaniandikia barua tarehe 07.01.2011 kutekeleza amri ya Waziri Maige.
Hivyo basi, kuanzia tarehe 07.01.2011 hadi hii leo naendelea kulipwa mshahara bila kufanya kazi. Msituni. watu wanaofanya uharibifu ikiwamo uvunaji haramu wa misitu ya asili bado wanaendelea na vitendo vyao hivyo.
Sababu ya kusimamishwa kazi kwangu ni kwamba nimezuia wavunaji misitu na wachimbaji madini ambao wana maslahi na Mkuu wa Wilaya ya Same na Mheshimiwa Maige mwenyewe.
Mimi sio mtumishi wa Wizara yake. Nipo Tamisemi ingawa kitaaluma ni Afisa Misitu. Ukweli ajira yangu haiko kwake, Waziri amekurupuka kwa nia mbaya. Labda kosa langu ni kutetea rasilimali za umma zisihujumiwe. Vinginevyo sina kosa lolote na ndio maana mpaka sasa kujua nini iwe hatma yangu kiajira mbali ya kunilipa mshahara kila mwezi bila kufanya kazi.
Nimefika Wizarani mara mbili. Ukweli pale Wizarani wanamwogopa sana Maige. Kila mtu anaogopa kushughulikia malalamiko yangu. Waziri anawatisha na wengine kuwasimamisha kazi hovyo kwa maslahi yake.
Ndugu Mwenyekiti,
Malalamiko yangu yako Tamisemi Idara Kuu ya Utumishi. Tume ya Utumishi wa Umma na wizarani kwenyewe. Sijui hatima yangu, lakini ukweli mpaka sasa nalipwa mshahara bure, bila ya kufanya kazi.
Ni mimi, Toto Kassi
Mjumbe aliyewekwa kijiweni na Waziri Maige
( Niko tayari kutoa ushahidi wa niliyoyaeleza hapa; 0784 715977)