Mtu na mzazi mwenzie

Mtu na mzazi mwenzie

otimbiotimbi

Senior Member
Joined
Dec 12, 2019
Posts
136
Reaction score
235
Wadau poleni sana na tozo na mambo mengine kadha wa kadha. Iko hivi, nimekuwa kwenye mahusiano na mwanamke fulani kwa muda wa miaka mitatu sasa unaenda mwaka wa 4.

Hii ni nyumba ndogo(mchepuko), sasa mchepuko huyu kuna mwamba kazaa nae mtoto wao ana miaka 5 kwasasa, na mwamba hawajajibiki kwa lolote hasa matunzo ya mtoto kwa mujibu wa maelezo ya mama mtoto.

Upande wangu mi nimeoa, tena ndoa ya kanisani kabisa nina mke na watoto wa 3. Sasa kuna kipindi katikati hapo tulitengana kidogo na mke wangu kwa mambo ya hapa na pale(wanandoa mnaelewa), akaamua kuondoka kwenda kwao akakaa kama miezi miwili hivi.

Wakati wote wife hayupo nikahamia nyumba ndogo, nikaendelea kumuomba mke wangu msamaha kwa mawasiliano ya siri nikiwa huku nyumba ndogo.

Baadae mke wangu akakubali kunisamehe na kurudi nyumbani, siku yake nikazuga naenda safari mahali mara moja(namna nilivyoaga huku nyumba ndogo) ili mradi nipate mpenyo nirudi home kwa wife.

Nilipotoka nilienda na nikafanikiwa kuonana na wife pale nyumbani vizuri kabisa. Sasa kule upande wa pili si niliaga nasafiri, ikabidi nirudi safari yangu sasa. Ile narudi nimefika tu, nikaenda kuoga narudi mtu anasema naomba simu yako(nyumba ndogo).

Ile kuchukua simu akakuta picha zangu na mke wangu na watoto wangu! Akaanza kuniuliza we kumbe na mkeo mmerudiana, nikamwambia ndio. Japo tangu tunaanza mahusiano alikuwa anajua kwamba nimeoa na nina familia yangu!

Baada ya kuona zile picha akasema mimi na wewe sasa basi! Upande wake na huyo mzazi mwenzie wanawasiliana, japo kwa siri akiwasiliana naye anafuta call history, kama ni whatsapp anafuta charts zao .

Sasa siku nikakuta picha ya matokeo ya mtoto wake ya shuleni kwenye whatsapp sent image, namuuliza anasema nampangia kwa kutuma matokeo ya mwanaye?

Baadae akasema mdogo wake alipiga picha akamtumia baba mtoto wake(Shemeji mtu). Kifupi mi nimechanganyikiwa tu, sijui nimfanyeje huyu mwanamke mana nimemgharamia .
 
Sasa hiyo si both teams to score wajameni? Nyie wote n wezi af mnawekeana mipaka? Mpe uhuru na we chukua uhuru. Mkikutana n kazi kazi baaas.

Shida n hiyo we umeenda kwa mchepuko badala ya kuwrka mguu ndani mguu nje, umevua nguo zote ukaamua kuogelea mazima.

Kwanza tabia gani ya kumueleza mchepuko kuhusu wife wako? Senzi sana we jamaa!
 
Mchome na gunia la mkaa!
Halafu akamatwe atupwe jela maisha tu maana siyo kwa upimbi huu.

Yaani wewe mleta mada huna faida kwa familia yako wala jamii nzima ya wanaume timamu wenye akili zao yaani unathubutu kulia hapa eti umemgharamikia malaya?kwa hiyo na mtoto wa watu ukalipia ada huku wako wakiwa kwa Bibi yao kijijini na mama yao?

Hovyo kabisa.
 
Kinachofuata hapo ni kwenda jela, hospitali au kabulini kama tu haujachukua hatua za kumuacha aende
 
Wadau poleni sana na tozo na mambo mengine kadha wa kadha. Iko hivi, nimekuwa kwenye mahusiano na mwanamke fulani kwa muda wa miaka mitatu sasa unaenda mwaka wa 4...
Ila Sijui tuna Nini? Most of the time wanaume tunajitakia matatizo wenyewe, yaani ukiona tu Kuna ka Amani Fulani Kuna ka roho kanaanza kukushawishi.
 
Kama una mashamba mawili, Moja Lina minazi mitatu uliyopanda mwenyewe na lingine la pili Lina Mnazi mmoja, Tena umeukuta tu hapo Shambani!

Akitokea MTU akikutaka uachie shamba Moja wapo kati ya Shamba lenye minazi mitatu uliyopanda mwenyewe vs shamba la Mnazi mmoja Tena uliopandwa na mtu mwingine, utachagua kupoteza Shamba lipi? Usinijibu! Mshukuru Mungu
 
sijui kama sijakuelewa hivi, yaani mchepuko alianza kuona picha za wewe na full wife, akasema iwe basi muachane halafu baada ya siku na wewe ukaona picha ya matokeo yakitumwa kwa kaka yako yaani aliyeanza kumpeleka leba.

natafuta ukweli wa story yako.. yaani mmeshaachana ila bado uliona picha kwenye simu yake?
au ni chai hii nayo
 
Wadau poleni sana na tozo na mambo mengine kadha wa kadha. Iko hivi, nimekuwa kwenye mahusiano na mwanamke fulani kwa muda wa miaka mitatu sasa unaenda mwaka wa 4.

Hii ni nyumba ndogo(mchepuko), sasa mchepuko huyu kuna mwamba kazaa nae mtoto wao ana miaka 5 kwasasa, na mwamba hawajajibiki kwa lolote hasa matunzo ya mtoto kwa mujibu wa maelezo ya mama mtoto.

Upande wangu mi nimeoa, tena ndoa ya kanisani kabisa nina mke na watoto wa 3. Sasa kuna kipindi katikati hapo tulitengana kidogo na mke wangu kwa mambo ya hapa na pale(wanandoa mnaelewa), akaamua kuondoka kwenda kwao akakaa kama miezi miwili hivi.

Wakati wote wife hayupo nikahamia nyumba ndogo, nikaendelea kumuomba mke wangu msamaha kwa mawasiliano ya siri nikiwa huku nyumba ndogo.

Baadae mke wangu akakubali kunisamehe na kurudi nyumbani, siku yake nikazuga naenda safari mahali mara moja(namna nilivyoaga huku nyumba ndogo) ili mradi nipate mpenyo nirudi home kwa wife.

Nilipotoka nilienda na nikafanikiwa kuonana na wife pale nyumbani vizuri kabisa. Sasa kule upande wa pili si niliaga nasafiri, ikabidi nirudi safari yangu sasa. Ile narudi nimefika tu, nikaenda kuoga narudi mtu anasema naomba simu yako(nyumba ndogo).

Ile kuchukua simu akakuta picha zangu na mke wangu na watoto wangu! Akaanza kuniuliza we kumbe na mkeo mmerudiana, nikamwambia ndio. Japo tangu tunaanza mahusiano alikuwa anajua kwamba nimeoa na nina familia yangu!

Baada ya kuona zile picha akasema mimi na wewe sasa basi! Upande wake na huyo mzazi mwenzie wanawasiliana, japo kwa siri akiwasiliana naye anafuta call history, kama ni whatsapp anafuta charts zao .

Sasa siku nikakuta picha ya matokeo ya mtoto wake ya shuleni kwenye whatsapp sent image, namuuliza anasema nampangia kwa kutuma matokeo ya mwanaye?

Baadae akasema mdogo wake alipiga picha akamtumia baba mtoto wake(Shemeji mtu). Kifupi mi nimechanganyikiwa tu, sijui nimfanyeje huyu mwanamke mana nimemgharamia .
Uliingia mazima kwa mchepuko. Pumba wewe. Pole yako. Mwache kama ulivyomkuta.

Kuna dalili kuwa huyo ni bidada wa mjini. Ukithubutu kumfanyia mbaya, utaumia.
 
Kabla hujafikilia cha kufanya unganinisha hizo bullet uone chain inafika wap
Mkei,wewe,mchepuko wako (nyumba ndigo), mchepuko wa nyumba ndogo yako, mchepuko wa mchepuko wa wa nyumba ndogo yako,,,,,
Kwa kuwa tuna mheshim mkeo tusizungmzie chain yake akiwa likizo tuassume alikua sterile
Ushaur wangu kwa kuwa una familia try not to be narcissistic jari maisha yako for the sake of your child
 
Hatuwezi kumlaum single mother wa watu
Bali wewe mwenyewe
Sababu wewe una mke na yeye anajua
Sasa ulitaka atulie?
Wewe unapokua na mkeo yeye afanyaje?


Sisisotenibinadamubwaba
 
Back
Top Bottom