otimbiotimbi
Senior Member
- Dec 12, 2019
- 136
- 235
Wadau poleni sana na tozo na mambo mengine kadha wa kadha. Iko hivi, nimekuwa kwenye mahusiano na mwanamke fulani kwa muda wa miaka mitatu sasa unaenda mwaka wa 4.
Hii ni nyumba ndogo(mchepuko), sasa mchepuko huyu kuna mwamba kazaa nae mtoto wao ana miaka 5 kwasasa, na mwamba hawajajibiki kwa lolote hasa matunzo ya mtoto kwa mujibu wa maelezo ya mama mtoto.
Upande wangu mi nimeoa, tena ndoa ya kanisani kabisa nina mke na watoto wa 3. Sasa kuna kipindi katikati hapo tulitengana kidogo na mke wangu kwa mambo ya hapa na pale(wanandoa mnaelewa), akaamua kuondoka kwenda kwao akakaa kama miezi miwili hivi.
Wakati wote wife hayupo nikahamia nyumba ndogo, nikaendelea kumuomba mke wangu msamaha kwa mawasiliano ya siri nikiwa huku nyumba ndogo.
Baadae mke wangu akakubali kunisamehe na kurudi nyumbani, siku yake nikazuga naenda safari mahali mara moja(namna nilivyoaga huku nyumba ndogo) ili mradi nipate mpenyo nirudi home kwa wife.
Nilipotoka nilienda na nikafanikiwa kuonana na wife pale nyumbani vizuri kabisa. Sasa kule upande wa pili si niliaga nasafiri, ikabidi nirudi safari yangu sasa. Ile narudi nimefika tu, nikaenda kuoga narudi mtu anasema naomba simu yako(nyumba ndogo).
Ile kuchukua simu akakuta picha zangu na mke wangu na watoto wangu! Akaanza kuniuliza we kumbe na mkeo mmerudiana, nikamwambia ndio. Japo tangu tunaanza mahusiano alikuwa anajua kwamba nimeoa na nina familia yangu!
Baada ya kuona zile picha akasema mimi na wewe sasa basi! Upande wake na huyo mzazi mwenzie wanawasiliana, japo kwa siri akiwasiliana naye anafuta call history, kama ni whatsapp anafuta charts zao
.
Sasa siku nikakuta picha ya matokeo ya mtoto wake ya shuleni kwenye whatsapp sent image, namuuliza anasema nampangia kwa kutuma matokeo ya mwanaye?
Baadae akasema mdogo wake alipiga picha akamtumia baba mtoto wake(Shemeji mtu). Kifupi mi nimechanganyikiwa tu, sijui nimfanyeje huyu mwanamke mana nimemgharamia


.
Hii ni nyumba ndogo(mchepuko), sasa mchepuko huyu kuna mwamba kazaa nae mtoto wao ana miaka 5 kwasasa, na mwamba hawajajibiki kwa lolote hasa matunzo ya mtoto kwa mujibu wa maelezo ya mama mtoto.
Upande wangu mi nimeoa, tena ndoa ya kanisani kabisa nina mke na watoto wa 3. Sasa kuna kipindi katikati hapo tulitengana kidogo na mke wangu kwa mambo ya hapa na pale(wanandoa mnaelewa), akaamua kuondoka kwenda kwao akakaa kama miezi miwili hivi.
Wakati wote wife hayupo nikahamia nyumba ndogo, nikaendelea kumuomba mke wangu msamaha kwa mawasiliano ya siri nikiwa huku nyumba ndogo.
Baadae mke wangu akakubali kunisamehe na kurudi nyumbani, siku yake nikazuga naenda safari mahali mara moja(namna nilivyoaga huku nyumba ndogo) ili mradi nipate mpenyo nirudi home kwa wife.
Nilipotoka nilienda na nikafanikiwa kuonana na wife pale nyumbani vizuri kabisa. Sasa kule upande wa pili si niliaga nasafiri, ikabidi nirudi safari yangu sasa. Ile narudi nimefika tu, nikaenda kuoga narudi mtu anasema naomba simu yako(nyumba ndogo).
Ile kuchukua simu akakuta picha zangu na mke wangu na watoto wangu! Akaanza kuniuliza we kumbe na mkeo mmerudiana, nikamwambia ndio. Japo tangu tunaanza mahusiano alikuwa anajua kwamba nimeoa na nina familia yangu!
Baada ya kuona zile picha akasema mimi na wewe sasa basi! Upande wake na huyo mzazi mwenzie wanawasiliana, japo kwa siri akiwasiliana naye anafuta call history, kama ni whatsapp anafuta charts zao
.Sasa siku nikakuta picha ya matokeo ya mtoto wake ya shuleni kwenye whatsapp sent image, namuuliza anasema nampangia kwa kutuma matokeo ya mwanaye?
Baadae akasema mdogo wake alipiga picha akamtumia baba mtoto wake(Shemeji mtu). Kifupi mi nimechanganyikiwa tu, sijui nimfanyeje huyu mwanamke mana nimemgharamia



.