Mtu anayekaa katikati ya Barabara pale Victoria

Mtu anayekaa katikati ya Barabara pale Victoria

chukua hatua mkuu! unaweza kushuka siku moja ukamwonda na kumeelimisha hatari ya kuomba barabarani

Kuna ndugu yake mmoja kila wakati alikuwa anakuja kumtoa kwa bakora pale. Naona atakuwa kashachoka. Ule uchizi utakuwa umesababishwa na bange au sembe. Sio wa kuzaliwa nao ule.
 
Dawa yake ni siku moja gari ikifunga breki miguuni mwake. Kama si chizi ataacha.
 
Wakati naanza kusoma ujumbe huu kuna kiswahili cha sasa hivi ukisoma kinakereketa sana nilidhani ni mwanafunzi wa shule ya msingi kumbe ni "Mzazi" ajirekebishe kiswahili chake katika maandishi mekundu niliyoya ahinisha, isimaanishe mimi najua sana kiswahili la hasha tunaelekezana tu. Samahani lakini

'kama ni kuelekezana basi ngoja tukuelekeze ndugu yangu huwezi kusema ajirekebishe kiswahili chake labda kama ungeweka koma baada ya neno ajirekebishe halaf ungeendelea na sentensi yako,na kamwe haiwezi kusemwa akirekebishe kwa sababu -ki- itasimama kwa kitu ambacho kinaonekana ila kwa kiswahili fasaha ulitakiwa kusema arekebishe kiswahili chake hivi ndivyo ilivyopaswa kuandikwa ndugu na pili umesema niliyoya ahinisha cha kwanza kabisa hukutakiwa kuachanisha hapo ni ungesema kwa mfano niliyoyazungumza huwezi kuachanisha yakawa maneno mawili ni neno moja tu hilo lakini bado kuna ukoseaji wa silabi ulitakiwa kusema ainisha na wala sio ahinisha ndugu yetu kabla ya kutoa kibanzi kwenye jicho la mwenzako ulitakiwa kutoa boriti kwanza kwenye jicho lako,tunaelekezana tu'
 
'kama ni kuelekezana basi ngoja tukuelekeze ndugu yangu huwezi kusema ajirekebishe kiswahili chake labda kama ungeweka koma baada ya neno ajirekebishe halaf ungeendelea na sentensi yako,na kamwe haiwezi kusemwa akirekebishe kwa sababu -ki- itasimama kwa kitu ambacho kinaonekana ila kwa kiswahili fasaha ulitakiwa kusema [COLOR]arekebishe kiswahili chake[/COLOR] hivi ndivyo ilivyopaswa kuandikwa ndugu,tunaelekazana tu'

Nakushukuru sana kwa ufafanuzi huo nimefurahi kwamba sasa tutaanza kufundishana kiswahili kwa ufasaha.
 
Habari zenu wakuu!huwa nasikitika sana kila wakati nikiwa napita hapa maeneo ya Victoria unamkuta mtu kakaa katikati ya barabara huku akiomba na pia inaonekana ana matatizo ya akili.
Je hakuna mamlaka zinazousika kuakikisha usalama wake !na waendesha Magari!
Mimi kama mzazi kama kuna wahusika basi wasaidie kumwondoa huyu mtu ili kutoatarisha maisha yake na watu wengine.Ni hayo tu


Hilo ndio swali ninalo jiuliza kila siku. Hiviii! hii Wizara ya Ustawi wa Jamii inafanya kazi gani nchiii hiii?
 
Hilo ndio swali ninalo jiuliza kila siku. Hiviii! hii Wizara ya Ustawi wa Jamii inafanya kazi gani nchiii hiii?
Siyo ustawi wa jamii tu hata polisi unamkuta mita chache anaongoza magari kwa nini wasiwe wanamfukuza!au kumwondoa na kumpleleka kunakostahili?
 
Natamani hata hawa Clouds FM kupitia kipindi chao cha PB.Mtu mwenye number zao watusaidie jamini.
 
Siyo ustawi wa jamii tu hata polisi unamkuta mita chache anaongoza magari kwa nini wasiwe wanamfukuza!au kumwondoa na kumpleleka kunakostahili?

Nakumpa Msaada anao stahili.
 
Duh bado yupo tuuu! Nilianza kumuona hapo 2011...........Aiseeeee!
 
Wote mnaompita na kumdhiaki pasipo kumsaidia Mungu anawaona adhabu kubwa juu yenu
 
Anabwia unga pale Mwananyamala A karibu na ofisi ya mtendaji.. maranyingi kuanzia asubuhi yupo na mateja papa wanatmia mlizo mgaia kuvuta bange na unga... jioni anakuja hapo kuweka kambi tena
 
Back
Top Bottom