Mtoto wa Mke wangu: Sheria inasemaje?

Mtoto wa Mke wangu: Sheria inasemaje?

Wa Mjengoni

JF-Expert Member
Joined
May 4, 2010
Posts
480
Reaction score
128
Napenda wenye ufahamu wanisaidie kuhusu hili.
Nina mke wangu wa ndoa ambaye kabla sijamuoa nilimkuta na mtoto wa kiume wa miaka mitatu, mtoto huyo sasa hivi mkubwa na ameingia form one sekondari.
Mtoto huyu ana baba yake ambaye ni mtu mwenye uwezo mkubwa tu, lakini kutokana na jeuri ya mama yake (mke wangu) hataki kumshirikisha mtoto upande wa babake kwa jambo lolote, yaani hataki hata mtoto ajue kuna babake. Ada ya shule silipi mimi ila mjomba wa mtoto yaani kaka wa mke wangu.
Chakula, mavazi, uniform, nauli ya kwenda shule ya boarding na matumizi ya shule vyote natoa mimi.
Katika kukorofishana baada ya yeye kukataa kunipigia pasi nguo zangu kwa madai kupiga pasi ni option tu hufanyika akipenda yeye sio lazima na mimi nikamjibu ku supply education materials kwa mwanao ni option tu sio lazima kwani mtoto huyo ana baba yake aliye hai , labda asingekuwa naye (amekufa) ndo ingekuwa lazima!
Niliongeza kuwa wajibu wangu kwa mtoto wake huyo ni kumpa chakula ale na kumpa malazi alale tu na sio vitu vingine.
Swali langu sheria inasemaje kuhusu wajibu wetu kwetu sisi akina baba wenye watoto wa aina hii?
 
Umejichanganya mkuu km mkeo hajapiga pasi ni kosa lake usitake kuhusisha uhusiano wako ww , mkeo na mtoto utahatarisha ndoa yako km ulikuwa hutaki kumlea mtoto ungekuwa wazi mapema ss tangu 3yrs mpaka seköndary! Ongea na mkeo atimize wajibu wake na ww ufanye kazi na kutimiza wajibu wako then mshirikishe mkeo kuhusu haki za mtoto , mtoto anapaswa kuwajua biological parents hata km ni vichaa si ndo wazazi wake!
 
Kwanini mkeo hataki mwanae aende kwa baba yake?????

Kama ishu ya kupiga pasi nguo inaleta matatizo yanayomgusa mtoto asiye na hatia, najaribu kutafakari siku atakapogoma kukupashia moto kiporo. Zawadi alizopewa baba mkwe zitahusika walahi.
 
Kuna wanawake wengine sijui huwa hata wanawaza nini!!??Sasa kama huyu akipatikana anaejua kutumia fursa, eti nae alalamike!!!!Ila za uso ulizompa nina imani zilimchoma ili ajue wajibu ni nini.Ngoja wajuzi wa sheria waje watiririke.
 
Kuna wanawake wengine sijui huwa hata wanawaza nini!!??Sasa kama huyu akipatikana anaejua kutumia fursa, eti nae alalamike!!!!Ila za uso ulizompa nina imani zilimchoma ili ajue wajibu ni nini.Ngoja wajuzi wa sheria waje watiririke.

Never ever trust a woman, ukipata fursa itumie chapchap sana.
 
"Kupasi nguo ni option siyo lazima?" huyo mwanamke wkt unamuoa hakupewa hata kitchen party ni bora hata angeomba umsaidie hata angesingizia kuwa hajisikii vizuri kuliko kuongea huo utumbo..........mtoto anapaswa amjue baba yake,mwambie akamtambulishe mtoto kwa baba yake huyo form 1 akili imeanza kukomaa!
 
Kwanza lazima nikiri wewe ni moja ya wanaume wenye moyo sana. Wanaume wengi hilo la kulea mtoto wa kiume toka 3yrs to Sec school ilihali baba mtoto yupo na anauwezo lahitaji moyo sana tu.

Tatizo ni pale ambapo wewe ulifanya hivo ukidhani mkeo atakuwa 'Yes boss' kwa kila hitaji lako. Haiwi hivo all the time my brother! Hata kama umemtendea mengi mema mwenzio, hutokea wakati mkawa katika hali ya ugonvi au kutokuelewana na hiyo ya pasi ikawa kama kukuadhibu fulani kwa kitu ambacho anadhani umemtendea sivo. Na hii haijalishi kama umemnunulia 'mbingu'!

Washirikishe wazee (me/ke) wenye busara ili huyo mtoto amjue baba yake mzazi, itapunguza mambo mengine mengi tu huko ukubwani kwake akifikia kutaka kuoa, nk.

You are a good husband, pasi isikukere sana!!

PP
 
According to dini ya kiislamu: Mtoto wa mkeo ni mtoto wako, na anastahili malezi yote kutoka kwako including mirathi.
Mtoto wa mumeo (kama wewe ni mwanamke) SIO mtoto wako na hatambuliki kisheria.
 
According to dini ya kiislamu: Mtoto wa mkeo ni mtoto wako, na anastahili malezi yote kutoka kwako including mirathi.
Mtoto wa mumeo (kama wewe ni mwanamke) SIO mtoto wako na hatambuliki kisheria.

Kwa nini wakati baba yake ni mume wangu
 
Mkuu hata tukikueleza kuhusu vifungu vya sheria je yafaa nini? (Vifungu vipo)

Maana sheria inapobainishwa maana yake inahitajika kitumika kwenye jukwaa la kisheria au kimaamuzi kama mahakama n.k

Kumtuza huyo mwanao wa kufikia au kutokumtunza inategemea na makubaliano yako ya awali na mkeo, pili inategemea na hulka na utashi wako wa kibinadamu.
 
jukumu lako kama baba kisheria liko juu ya mwanao wa kumzaa. Kwa mtoto wa mkeo ni utashi wako tu, hakuna sheria inayokulazmisha..
 
we bana hebu sovu issue zako na mkeo!
kama hukuwa tayari kulea huyo mtoto toka mwanzo ungesema abaki kwa mjomba wake we uchukue mke!


ulishindwa kuweka misingi y kunyooshewa nguo toka mnaoana leo uje kulalamika ?
kwa mfano mkeo akiwa anakunyooshea
-itaondoa ukweli kuwa baba wa huyo mtoto ana uwezo?
-itaondoa ukweli kuwa mkeo hataki kumtambulisha mtoto kwa babake?
-itaondoa ukweli kuwa mkeo ana kiburi(kwa tafsiri yako kutotaka mawasiliano na baba wa mtoto ni kburi?eheheh sijui kama unajua unachokiwish)


hebu fanya homework yako!
 
yan ningekuwa mimi nisingeongea chochote ningekuwa naondoka asbuhi cjanyoosha naingia kwenye gari naondoka na jion narud zmenyooka vzuri. Siku nikiona vp narud nimebadilisha nguo kabisa. Angepata adabu

Umekosea kumhusisha mtoto. Epuka kujibizana na mwanamke ndani ya ndoa. ukiona umemwambia hajakuelewa fanya kwa vitendo kimyakimya.
 
Mkuu kwanza nikupongeze kwa ujasiri wa kukubali kuoa mwanamke mwenye mtoto na bado mkeo asione kujitoa huko hadi akujibu kwa jeuri namna hiyo. Kukatisha huduma kwa mwanao wa hiari nadhani ni hasira tu, mtoto hana hatia, endelea kumhudumia inalipa sana, Mungu lazima anakuona na atakulipa wema wako, ila jitahidi mtoto amfahamu baba yake maana ni haki yake.
 
Kuna wanawake wengine sijui huwa hata wanawaza nini!!??Sasa kama huyu akipatikana anaejua kutumia fursa, eti nae alalamike!!!!Ila za uso ulizompa nina imani zilimchoma ili ajue wajibu ni nini.Ngoja wajuzi wa sheria waje watiririke.

maneno alomtolea ayahusiani na ugomvi walokuwa nao, kumlea mtoto aliamua mwenyewe ipo sku atahusisha na vitu alivyoweza kuvifanya kwao mwanamke km ndugu wa mwanamke wanaenda kuwatembelea na jamaa akasaidia sometimes nauli, atazisemea sku1 ktk ugomvi. Najiuliza ina faida gani yeye kutoa msaada kumbe inamuuma c angeacha tangia mwanzo? Msaada anaoutoa kwa mtoto havihusiani kabisa na ugomvi wa mke wake kutokuwajibika
 
It doesnt make sense to me kwamba mke kagoma kukupasia nguo then unahusishaje na hilo suala la mtoto? Nadhani uombe tu ushauri on how to handle hiyo situation ya mtoto! Kifupi tu mtoto atambulishwe kwa baba yake na ikibidi babayake abebe majukumu ya mwanae yote ikibidi hata aishi nae mana hapo kwako nahisi moshi unaanza kufuka usijemfanya vibaya mtoto wa watu bure!
 
Mimi kwanza nikushauri kuhusu ndoa yako. Kwenye ndoa kama ilivyo kwenye uhusiano wowote "Revenge" ni kitu kibaya na matunda yake ni lazima uhusiano uvunjike. Atakataa kukupigia pasi, utakataa kumpa mtoto pocket money, atakununia na wewe utamnunia, kisha atakunyima unyumba na wewe utatoka nje...ukitoka na yeye anatoka. Sasa huko nje kuna atakayerudi na mimba na mwingine hiv...Kuna atakayekolea hatimaye divorce proceedings zikaanza na mtatengeneza watoto wa kambo watakaoenda kusababisha majanga kwenye ndoa nyingine. Now tell me, Where r we heading?

Never ever ever think of doing something bad to a person to counter for something bad done to u unless u want an enemy out of them.

Kingine, Kama wewe ni baba wa ukweli kabisa. Huyo mtoto ulitakiwa uwapatanishe hao wazazi wake na mtoto akalelewe full na baba-haijalishi utatumia mbinu gani kufanikisha hilo. Baba yake akimkataa wewe kama kichwa cha nyumba unatakiwa kumchukua under ur wing. Anakuwa mwanao jukumu lako kabisa kama hao wengine.

Kataa kuwa baba wa kushikiza, mkeo anajifanyia tu maamuzi yake na mtoto analipiwa na ndugu za mkeo. Mwishowe mtoto akuletee dharau uone kama utaweza kuwa baba hapo nyumbani! Tena unamtumia kumtisha mkeo? Thats too low man!
 
Kutokupasi mkeo hakuhusiani na mtoto,ww shida zako na mkeo unamuingiza vp mtt?umelazimishwa kumuhudumia?huko ni kumnyanyapaa mtt,na unavyoonekana unataka mtt either apelekwe kwa baba ake au ahudumiwe na baba ake,hujui madhara ya mkeo kua na mawasiliano na mzazi mwenzie,shukuru mkeo hataki mawasiliano na huyo baba,ulipenda boga babu penda na ua lake,yako na mkeo hayamhusu mtt!
 
Back
Top Bottom