Mtoto wa miezi mitatu hakui

Kama ni mtoto wa kwanza wamama wengi huwa hatujui kunyonyesha vizuri watoto. Ila baadae nilipofundishwa wtt wangu walofata walikua wana gain haraka sana. Unachotakiwa kufanya usimnyonyeshe mtoto ziwa moja dkk chache mara ushamwamishia tena upande mwingine. Maziwa yamegawinyika mara mbili kama sikosei fore milk na maziwa yanayofata. Ya mbele yanajaa maji tuu hivyo ukimnyonyesha hayo ya mbele utaona kama ameshiba ila sio kushiba vzr amejaza tuu maji hayana virutubisho muhimu na sio mazito so hakikisha mtt ananyonya ziwa moja hata kwa dkk 15 mpk yale maziwa ya nyuma yaliyo mazito na yenye wingi wa protini yaishe. Hata kama akionekana ameshiba muache kidogo kama dkk tano then arudie ziwa lile lile mpk uone limenywea. Kama hili lingine litakua limevimba sana maziwa yamejaa sana unaweza anza kwa kuyakamulia nje then ndo umpe anyonye sasa ili asipaliwe na hayo maana hutoka kwa kasi. Jaribu hivyo kama hufanyi hivyo.
 
Bila shaka ni first born..wasiwasi kama wote kila kitu unachunguza

Ataongezeka tu dear..asije akatokea mtu akakwambia mlambishe viuji hashibi sijui nini itakula kwako.
 
Habari zenu.. natumain ni wazima wa afya na wale wagonjwa poleni Mungu atawaponya.

Nina mtoto wa miezi mitatu huyu mtoto shida yake kwenye ukuaji yaan haongezeki kilo..alipata shida kidogo wakati alipozaliwa alikua hataki kunyonya ila baada ya wiki moja mbele alianza kunyonya..kwa sasa ana kilo 4 tu.

Ushaur wenu nifanye nini ili mtoto huyu aongezeke na akue.

Asanten.

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
Mtoto huyu na akue ikiwa ni pamoja na kuwa na afya njema sana; kwa jina la YESU
 
Back
Top Bottom