Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,660
- 46,350
Ferdinand "Bongbong Marcos" Jr. ameshinda urais wa Philippines kwa zaidi ya asilimia 50 za kura huku mpinzani wake wa karibu akiwa na wastani wa 30%.
Baba yake Dikteta Ferdinand Marcos aliitawala Philipines kwa miaka 21, mwaka 1965 hadi 1986, chini ya utawala wa mkono wa chuma huku muda mrefu zaidi akiitawala kwa amri ya kijeshi" martial law" na amri za kawaida "decree" baada mahakama kumzuia kugombea kwa muhula wa tatu mwaka 1972.
Utawala wake ulikuwa muovu sana, wa kifisadi, wapinzani wake waliuwawa na kupotea. Hadi anaondolewa madarakani mwaka 1986 inakadiriwa alikuwa ameiba billion 10 dola za kimarekani. Mke wake alikuwa na hobby kubwa ya viatu, inakadiriwa alikuwa akimiliki pair 3000 za viatu hadi wakati wanaondolewa madarakani.
Hatimaye wapiga kura wa Philippines wameamua kuirudisha familia hiyo ya Marcos madarakani kupitia mtoto pekee wa familia hiyo. Marcos Jr. ataitawala nchi hiyo kwa kipindi cha muhula mmoja wa miaka 7 kama hatabadilisha katiba ya nchi hiyo.
Demokrasia wakati mwingine ina mitanziko na matokeo ya kushangaza.
Baba yake Dikteta Ferdinand Marcos aliitawala Philipines kwa miaka 21, mwaka 1965 hadi 1986, chini ya utawala wa mkono wa chuma huku muda mrefu zaidi akiitawala kwa amri ya kijeshi" martial law" na amri za kawaida "decree" baada mahakama kumzuia kugombea kwa muhula wa tatu mwaka 1972.
Utawala wake ulikuwa muovu sana, wa kifisadi, wapinzani wake waliuwawa na kupotea. Hadi anaondolewa madarakani mwaka 1986 inakadiriwa alikuwa ameiba billion 10 dola za kimarekani. Mke wake alikuwa na hobby kubwa ya viatu, inakadiriwa alikuwa akimiliki pair 3000 za viatu hadi wakati wanaondolewa madarakani.
Hatimaye wapiga kura wa Philippines wameamua kuirudisha familia hiyo ya Marcos madarakani kupitia mtoto pekee wa familia hiyo. Marcos Jr. ataitawala nchi hiyo kwa kipindi cha muhula mmoja wa miaka 7 kama hatabadilisha katiba ya nchi hiyo.
Demokrasia wakati mwingine ina mitanziko na matokeo ya kushangaza.