Kuna mshikaji wangu miaka ya nyuma baada ya kumaliza chuo wakati sisi tuko kitaa na bahasha Kusaka kazi yeye brother wake akamuunganisha mchongo kwenye NGO flani. Kazi ya kwanza wakaenda field kufanya tafiti for three months, na wakaja wazungu watatu (mmoja dada mkalii) wakaungana na staff wengine ikawa timu ya watu nane. Wakaenda field huko Kilwa na Liwale mkoani Lindi. Huko porini walikuwa na mahema but jamaa anasema yule dada wa kizungu akawa ameanza kumzoea jamaa mpaka ikawa muda wote yuko kwenye hema la mshikaji, sometimes na kipensi na tisheti tuu.... Ikaendaa hivyo mpaka jamaa akaanza kuona mzungu kampenda. Weekend moja wakatoka porini kwenda town (wilayani) kupata good time kidogo. Wakiwa town baada ya kupata lager na Konyagi za Kutosha wakaenda guest Kutafuta room, jamaa kuingia kwa room si akaomba mchezo huku anaanza kumvua nguo demu wa kizungu... Aisee mzungu alichange ghafla na kuwa mwekundu kwa hasira, akamsukuma jamaa huko Akafungua mlango na kwenda kutafuta another guest. Jamaa pombe ikakata na usiku mzima hakulala akifikiria kesho aibu yake ataificha wapi.
Sent using
Jamii Forums mobile app