Mtifuano mkali; Nini kinaendelea Kanisa la Tanzania?

MTAZAMO

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
19,643
33,432
Wakuu,

Nahisi wengi hawajafuatilia kwa karibu "vita" inayoendelea kwenye makanisa ya kiroho. Hivi karibuni Askofu Kakobe, Mtume Fenenard (yule wa Agape) na Askofu Gamanywa waliunda umoja wao na kuuita Jukwaa la kumuhubiri Kristo na siku ya uzinduzi waliponda mno huduma za sasa hasa manabii ikiwemo kuuzwa kwa mafuta na maji ya upako.

Kakobe alifikia hatua kuitaka serikali kukusanya kodi kwa manabii wanaouza maji na mafuta ya upako maana ni biashara kabisa na kinyume cha maandiko

Nimefatilia matamko ya hilo jukwaa la kumuhubiri Kristo nikaona video ambayo walikuwa wakifafanua kusudi la jukwaa hilo na pia waliweka sauti za watu walioibuka kuwajibu na kujibu hoja zao (nenda YouTube utakuta mengi zaidi).

Leo nimeona limeitishwa kongamano la huduma zote tano likiongozwa na akina Askofu Gwajima, Mwingira na wahudhuriaji wengi akiwemo akina Mwamposa n.k

Hili kongamano lilishasemwa kuandaliwa kuwajibu akina Kakobe ( ukisikiliza majibu ya akina Kakobe) na kweli limefanyika.

Ni dhahiri kuna mgawanyiko mkubwa, si kawaida kuona mtu kama Askofu Gwajima akiwa kinyume na mtu anayemwita baba yake kiroho yaani Kakobe.

Kwanza kama Roho ni yule yule hawezi kufunulia watu wake mafunuo yanayopingana. Huku kupingana ni dalili dhahiri ya kazi ya yule mwovu.

Mimi ni Mkatoliki na sipo hapa kupinga imani za wengine zaidi nawaombea umoja kama jinsi kila misa lazima tuombee umoja wa kanisa. Umoja wa Kanisa ni moja ya sala ambayo Kristo aliombea kanisa lake.

Maandiko yanasema nyinyi ni chumvi na chumvi ikiishiwa utamu itakolezwa na nini? Kama mnashindwa kuambiana ukweli kama Paulo alivyomkosoa Petro wazi nani awasuluhishe? Kiburi cha kiroho?

Itakuwa aibu mtapokuja kusuluhishwa na wanasiasa, tumieni umoja wenu rasmi unaotambuliwa na serikali kuainisha ukweli juu ya huduma zenye utata na mueleze ukweli ili watu wataoamua kwenda huko waende wakijua kweli.

Hizi link zitawasaidia wanaotaka kufatilia zaidi huu mtifuano mkali.






 
Wakuu,

Nahisi wengi hawajafuatilia kwa karibu "vita" inayoendelea kwenye makanisa ya kiroho. Hivi karibuni Askofu Kakobe, Mtume Fenenard (yule wa Agape) na Askofu Gamanywa waliunda umoja wao na kuuita Jukwaa la kumuhubiri Kristo na siku ya uzinduzi waliponda mno huduma za sasa hasa manabii ikiwemo kuuzwa kwa mafuta na maji ya upako.

Kakobe alifikia hatua kuitaka serikali kukusanya kodi kwa manabii wanaouza maji na mafuta ya upako maana ni biashara kabisa na kinyume cha maandiko

Nimefatilia matamko ya hilo jukwaa la kumuhubiri Kristo nikaona video ambayo walikuwa wakifafanua kusudi la jukwaa hilo na pia waliweka sauti za watu walioibuka kuwajibu na kujibu hoja zao (nenda YouTube utakuta mengi zaidi).

Leo nimeona limeitishwa kongamano la huduma zote tano likiongozwa na akina Askofu Gwajima, Mwingira na wahudhuriaji wengi akiwemo akina Mwamposa n.k

Hili kongamano lilishasemwa kuandaliwa kuwajibu akina Kakobe ( ukisikiliza majibu ya akina Kakobe) na kweli limefanyika.

Ni dhahiri kuna mgawanyiko mkubwa, si kawaida kuona mtu kama Askofu Gwajima akiwa kinyume na mtu anayemwita baba yake kiroho yaani Kakobe.

Kwanza kama Roho ni yule yule hawezi kufunulia watu wake mafunuo yanayopingana. Huku kupingana ni dalili dhahiri ya kazi ya yule mwovu.

Mimi ni Mkatoliki na sipo hapa kupinga imani za wengine zaidi nawaombea umoja kama jinsi kila misa lazima tuombee umoja wa kanisa. Umoja wa Kanisa ni moja ya sala ambayo Kristo aliombea kanisa lake.

Maandiko yanasema nyinyi ni chumvi na chumvi ikiishiwa utamu itakolezwa na nini? Kama mnashindwa kuambiana ukweli kama Paulo alivyomkosoa Petro wazi nani awasuluhishe? Kiburi cha kiroho?

Itakuwa aibu mtapokuja kusuluhishwa na wanasiasa, tumieni umoja wenu rasmi unaotambuliwa na serikali kuainisha ukweli juu ya huduma zenye utata na mueleze ukweli ili watu wataoamua kwenda huko waende wakijua kweli.

Hizi link zitawasaidia wanaotaka kufatilia zaidi huu mtifuano mkali.







Tuwekee habari za kongamano la akina Gwajima leo, kumezungumzwa nini?
 
Wakuu,

Nahisi wengi hawajafuatilia kwa karibu "vita" inayoendelea kwenye makanisa ya kiroho. Hivi karibuni Askofu Kakobe, Mtume Fenenard (yule wa Agape) na Askofu Gamanywa waliunda umoja wao na kuuita Jukwaa la kumuhubiri Kristo na siku ya uzinduzi waliponda mno huduma za sasa hasa manabii ikiwemo kuuzwa kwa mafuta na maji ya upako.

Kakobe alifikia hatua kuitaka serikali kukusanya kodi kwa manabii wanaouza maji na mafuta ya upako maana ni biashara kabisa na kinyume cha maandiko

Nimefatilia matamko ya hilo jukwaa la kumuhubiri Kristo nikaona video ambayo walikuwa wakifafanua kusudi la jukwaa hilo na pia waliweka sauti za watu walioibuka kuwajibu na kujibu hoja zao (nenda YouTube utakuta mengi zaidi).

Leo nimeona limeitishwa kongamano la huduma zote tano likiongozwa na akina Askofu Gwajima, Mwingira na wahudhuriaji wengi akiwemo akina Mwamposa n.k

Hili kongamano lilishasemwa kuandaliwa kuwajibu akina Kakobe ( ukisikiliza majibu ya akina Kakobe) na kweli limefanyika.

Ni dhahiri kuna mgawanyiko mkubwa, si kawaida kuona mtu kama Askofu Gwajima akiwa kinyume na mtu anayemwita baba yake kiroho yaani Kakobe.

Kwanza kama Roho ni yule yule hawezi kufunulia watu wake mafunuo yanayopingana. Huku kupingana ni dalili dhahiri ya kazi ya yule mwovu.

Mimi ni Mkatoliki na sipo hapa kupinga imani za wengine zaidi nawaombea umoja kama jinsi kila misa lazima tuombee umoja wa kanisa. Umoja wa Kanisa ni moja ya sala ambayo Kristo aliombea kanisa lake.

Maandiko yanasema nyinyi ni chumvi na chumvi ikiishiwa utamu itakolezwa na nini? Kama mnashindwa kuambiana ukweli kama Paulo alivyomkosoa Petro wazi nani awasuluhishe? Kiburi cha kiroho?

Itakuwa aibu mtapokuja kusuluhishwa na wanasiasa, tumieni umoja wenu rasmi unaotambuliwa na serikali kuainisha ukweli juu ya huduma zenye utata na mueleze ukweli ili watu wataoamua kwenda huko waende wakijua kweli.

Hizi link zitawasaidia wanaotaka kufatilia zaidi huu mtifuano mkali.







Waache wafu wazikane
 
Vitu kama hivi hapa JF ndio tunaweza kujadili bila kuwa biased. Media zote za dini zina upande, hata vipindi huru kama Chomoza haviwezi kuwa huru sababu hutegemea "baba" zao wapo upande gani ndio maana habari za Jukwaa la kumuhubiri Kristo hawakuzitangaza kabisa lakini hili kongamano wamelipa airtime! Ndio ukristo huo na "ulokole" wa siku hizi.
 
Dini inatumika vibaya, ukristo asilia ulilenga kuponya roho za wanadamu, ukristo wa sasa ni ukristo maslahi binafsi, viongozi wa dini wanawanyonya waumini na kujitajirisha wao, kama kweli maaskofu, wachungaji, makasisi na wengineo wana dhamira ya kweli ya kuokoa roho na miili ya watu, wafanye kama alivyofanya Yesu Kristo, awaponye na kuwahudumu waumini bila gharama wala ujanja ujanja.
 
Dini inatumika vibaya, ukristo asilia ulilenga kuponya roho za wanadamu, ukristo wa sasa ni ukristo maslahi binafsi, viongozi wa dini wanawanyonya waumini na kujitajirisha wao, kama kweli maaskofu, wachungaji, makasisi na wengineo wana dhamira ya kweli ya kuokoa roho na miili ya watu, wafanye kama alivyofanya Yesu Kristo, awaponye na kuwahudumu waumini bila gharama wala ujanja ujanja.
Kiukweli binafsi sioni ubaya waliosema akina Kakobe ila hofu yangu ni kuwa kuna vita nje ya kupingana ukweli juu ya hizi huduma! Mpaka limeundwa jukwaa la kumuhubiri Kristo bila akina Gwajima na hii ya leo maana yake haya ni matokeo tu lakini kuna kitu kikubwa nyuma ya haya.
 
Kama tuna nia ya kweli uwekwe mjadala wa wazi usio na mipaka ili facts ziwekwe wazi. Waitwe hadi mababa kutoka Kanisa Katoliki, Lutheran, Anglican n.k

Hakuna haja ya kiburi cha kiroho, Yapo makanisa yalikuwepo kabla ya yote haya ya sasa. Ipo miaka hakukuwa na huduma binafsi (kanisa binafsi). Warudi kwa hao waliopokea imani kwao. Kwani walijibatiza? Kwani waliowabatiza walijibatiza? Kipo chanzo, wakaulize na kuhoji alafu waendelee na huduma zao.
 
Nimekuwa mfuatiliaji Mkubwa wa kongamano hili la jukwaa la kumhubiri Kristo(jkk) Kwa kifupi niseme naunga kabisa na haya maoni ya Baba Yangu askofu Sylvester gamanjwa...
Kama wewe ni ni mfuatiliaji mzuri wa vipindi vya redio wapo utapata kujifunza na kupata elimu kubwa juu ya hawa wanaojiita mitume na manabii.

Hawa akina mwamposa na akina Mzee Wa upako ni wezi Tu wa injili na inafaa kukemewa kama hivi ili wakristo wasipotee haiwezekani mafuta,chumvi,sabuni na maji ya upako vikamponya mtu huu ni uganga wa kienyeji LIVE.
Tena ningeomba Kwenye hili kongamano aletwe pia nguli wa injili mch Maghembe wa pale majumba sita Ukonga(gospel campaign center church) huyu Mzee Yuko fit Sana Kwenye kukemea usanii unaofanyika makanisani hasa Kwenye mambo ya maombezi.

Sikuzote jina la Yesu linajitosheleza hizi chumvi na maji vinatoka wapi? MUNGU hachanganywi na mambo ya uchawi ili aponye Bali Kwa lile jina lenye nguvu na mamlaka tulilopewa wanadamu(Yesu kristo)
 
Nimekuwa mfuatiliaji Mkubwa wa kongamano hili la jukwaa la kumhubiri Kristo(jkk) Kwa kifupi niseme naunga kabisa na haya maoni ya Baba Yangu askofu Sylvester gamanjwa...
Kama wewe ni ni mfuatiliaji mzuri wa vipindi vya redio wapo utapata kujifunza na kupata elimu kubwa juu ya hawa wanaojiita mitume na manabii.

Hawa akina mwamposa na akina Mzee Wa upako ni wezi Tu wa injili na inafaa kukemewa kama hivi ili wakristo wasipotee haiwezekani mafuta,chumvi,sabuni na maji ya upako vikamponya mtu huu ni uganga wa kienyeji LIVE.
Tena ningeomba Kwenye hili kongamano aletwe pia nguli wa injili mch Maghembe wa pale majumba sita Ukonga(gospel campaign center church) huyu Mzee Yuko fit Sana Kwenye kukemea usanii unaofanyika makanisani hasa Kwenye mambo ya maombezi.

Sikuzote jina la Yesu linajitosheleza hizi chumvi na maji vinatoka wapi? MUNGU hachanganywi na mambo ya uchawi ili aponye Bali Kwa lile jina lenye nguvu na mamlaka tulilopewa wanadamu(Yesu kristo)
Basi hujamuelewa baba yako. Hawapingi matumizi ya maji, chumvi n.k maana ipo biblical ila namna vinavyotumika na huduma za siku hizi hasa kuuzwa!

Hata sisi Wakatoliki tunatumia maji, chumvi, mafuta lakini haviuzwi! Huwezi kuuza upako! Unaweza kuuza zana za sala kama rozali, au biblia n.k lakini sio upako! Yesu mwenyewe alitumia tope kuponya lakini maandiko kama haya yanatumika vibaya mno! Wengine wanalishwa hadi majani!
 
Hao wote mi naita mbwa wote yanatufanyia mazingaombwe,mieleka,maigizo ya kuponya kwa kulitumia jina la Yesu Kristo vibaya.
 
Hao wote mi naita mbwa wote yanatufanyia mazingaombwe,mieleka,maigizo ya kuponya kwa kulitumia jina la Yesu Kristo vibaya.
Tutawatambua kwa matunda yao. Muda utaongea
 
Wakuu,

Nahisi wengi hawajafuatilia kwa karibu "vita" inayoendelea kwenye makanisa ya kiroho. Hivi karibuni Askofu Kakobe, Mtume Fenenard (yule wa Agape) na Askofu Gamanywa waliunda umoja wao na kuuita Jukwaa la kumuhubiri Kristo na siku ya uzinduzi waliponda mno huduma za sasa hasa manabii ikiwemo kuuzwa kwa mafuta na maji ya upako.

Kakobe alifikia hatua kuitaka serikali kukusanya kodi kwa manabii wanaouza maji na mafuta ya upako maana ni biashara kabisa na kinyume cha maandiko

Nimefatilia matamko ya hilo jukwaa la kumuhubiri Kristo nikaona video ambayo walikuwa wakifafanua kusudi la jukwaa hilo na pia waliweka sauti za watu walioibuka kuwajibu na kujibu hoja zao (nenda YouTube utakuta mengi zaidi).

Leo nimeona limeitishwa kongamano la huduma zote tano likiongozwa na akina Askofu Gwajima, Mwingira na wahudhuriaji wengi akiwemo akina Mwamposa n.k

Hili kongamano lilishasemwa kuandaliwa kuwajibu akina Kakobe ( ukisikiliza majibu ya akina Kakobe) na kweli limefanyika.

Ni dhahiri kuna mgawanyiko mkubwa, si kawaida kuona mtu kama Askofu Gwajima akiwa kinyume na mtu anayemwita baba yake kiroho yaani Kakobe.

Kwanza kama Roho ni yule yule hawezi kufunulia watu wake mafunuo yanayopingana. Huku kupingana ni dalili dhahiri ya kazi ya yule mwovu.

Mimi ni Mkatoliki na sipo hapa kupinga imani za wengine zaidi nawaombea umoja kama jinsi kila misa lazima tuombee umoja wa kanisa. Umoja wa Kanisa ni moja ya sala ambayo Kristo aliombea kanisa lake.

Maandiko yanasema nyinyi ni chumvi na chumvi ikiishiwa utamu itakolezwa na nini? Kama mnashindwa kuambiana ukweli kama Paulo alivyomkosoa Petro wazi nani awasuluhishe? Kiburi cha kiroho?

Itakuwa aibu mtapokuja kusuluhishwa na wanasiasa, tumieni umoja wenu rasmi unaotambuliwa na serikali kuainisha ukweli juu ya huduma zenye utata na mueleze ukweli ili watu wataoamua kwenda huko waende wakijua kweli.

Hizi link zitawasaidia wanaotaka kufatilia zaidi huu mtifuano mkali.







Kwani hao ni Dhehebu moja hadi useme kuna mgawanyiko?

Kanisa lilishagawanyika kitambo baada ya kutekwa na warumi na kuanzisha ukatoliki!
 
Basi hujamuelewa baba yako. Hawapingi matumizi ya maji, chumvi n.k maana ipo biblical ila namna vinavyotumika na huduma za siku hizi hasa kuuzwa!

Hata sisi Wakatoliki tunatumia maji, chumvi, mafuta lakini haviuzwi! Huwezi kuuza upako! Unaweza kuuza zana za sala kama rozali, au biblia n.k lakini sio upako! Yesu mwenyewe alitumia tope kuponya lakini maandiko kama haya yanatumika vibaya mno! Wengine wanalishwa hadi majani!
Akina mwamposa ameingia mkataba na kampuni ya maji(Canadian water) ambayo yanauzwa kwa jumapili sio chini ya carton 150-200.
Ukienda Kwa Nicolas suguye huyu ndiye mwizi Mkuu kwelikweli maana badala ya kuhubiri watu wamjue MUNGU na kutubu yeye sikuzote anahubiri jinsi wachawi wanavyologa,mizimu ya ukoo na familia,madhabahu ya kichawi na kiganga..... Kwenye makanisa Yao neno Yesu kristo limehadimika vinywani mwao
 
Back
Top Bottom