mapenzi hasara
Senior Member
- Feb 28, 2020
- 102
- 275
Nami nikaona mti mkubwa Sana unaotoa nuru upande mmoja na upande mwingine wa mti kuna Giza totoro.
Nami nikaona wamiliki wa mti huu wakiwaonesha wanakijiji upande mmoja wa nuru na kuwaficha upande mwingine wa Giza.
Nami nikaona upande wa Nuru wa mti ukizidiwa na Giza kuanza kutanda katika kijiji husika.
Wanakijiji wanapojaribu kuukata ule mti wanatishwa na wamiliki, Kwa kuwaua na kuwashtaki Kwa kuwapa kesi zisizowahusu.
Nikaona Giza likitanda na hatimae upande wa mwanga ukapotea mara wanakijiji wakihangaika kupata mwanga Kwa miaka kadhaa bila mafanikio huku maamuzi yote yakifanywa bila kushirikishwa wanakijiji.
Nikaona wanakijiji wako kimya wakiwa wamefunga midomo wamekaa katika Giza totoro, wanakijiji wamekosa tumaini nalo limepotea kabisa wakiwa wanalia mbele za Mungu juu Giza katika kijiji.
Nami nikaona wingu likifunguka mwanga mkali kutoka mawinguni ukilipiga ule mti mkubwa utoao kiza kinene, nao mwanga ukalishinda kiza na kukausha kabisa ule.
Nami nikaona mti ukikauka wamiliki wakikimbia na kukana umiliki wa mti ule, nikaona mti ukiondoka taraibu baada ya kumaishwa na mwanga kutoka mawinguni.
Mwisho nikaona wanakijiji wanavyofurahia kuondoka kwa ule mti na kuna kwa mwanga.
Nami nikaona wamiliki wa mti huu wakiwaonesha wanakijiji upande mmoja wa nuru na kuwaficha upande mwingine wa Giza.
Nami nikaona upande wa Nuru wa mti ukizidiwa na Giza kuanza kutanda katika kijiji husika.
Wanakijiji wanapojaribu kuukata ule mti wanatishwa na wamiliki, Kwa kuwaua na kuwashtaki Kwa kuwapa kesi zisizowahusu.
Nikaona Giza likitanda na hatimae upande wa mwanga ukapotea mara wanakijiji wakihangaika kupata mwanga Kwa miaka kadhaa bila mafanikio huku maamuzi yote yakifanywa bila kushirikishwa wanakijiji.
Nikaona wanakijiji wako kimya wakiwa wamefunga midomo wamekaa katika Giza totoro, wanakijiji wamekosa tumaini nalo limepotea kabisa wakiwa wanalia mbele za Mungu juu Giza katika kijiji.
Nami nikaona wingu likifunguka mwanga mkali kutoka mawinguni ukilipiga ule mti mkubwa utoao kiza kinene, nao mwanga ukalishinda kiza na kukausha kabisa ule.
Nami nikaona mti ukikauka wamiliki wakikimbia na kukana umiliki wa mti ule, nikaona mti ukiondoka taraibu baada ya kumaishwa na mwanga kutoka mawinguni.
Mwisho nikaona wanakijiji wanavyofurahia kuondoka kwa ule mti na kuna kwa mwanga.