PreGE2025 Mtazamo Wangu Kuhusu No Reform No Election

PreGE2025 Mtazamo Wangu Kuhusu No Reform No Election

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

ERTUGRUL BEY

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
11,622
Reaction score
21,689
Screenshot_20250426_102254_Google.jpg


Ni mara chache sana huwa naandika kuhusu Siasa,na niweke wazi huu ni mtazamo wangu kama ambavyo nawe unaweza kuwa na mtazamo wako

Binafsi naona hii movement ingesubiri kwanza kwasababu moja kubwa,ni hivi majuzi tu Mheshimiwa Tundu Lissu ndio amechukua madaraka ya Uenyekiti wa Chama cha Chadema,hivyo basi angehitaji kwanza kujipanga na kuunganisha nguvu ya chama hasa ukichukua bado kuna majeraha kadhaa baada ya uchaguzi

Hii kwanza ingempa fursa ya kuweka mambo sawa ndani ya Chama pamoja na kutengeneza mazingira mazuri ambayo yatakuwa rafiki kwa kila mwana chadema ,kuwa familiar na sera na malengo ya Chama pamoja na kuwa na mipango thabiti katika kuchukua dola ya nchi hii

Chama kuwa imara ni pamoja na kutengeneza mifumo mizuri ya kupata pesa ambazo zitawezesha Chama kufanya shughuli zake za siasa bila kikwazo chochote kile,na hii inawezekana tu pale Kiongozi Mkuu atakapo unganisha nguvu ya Viongozi pamoja na Wanachama wake

Sasa kabla hilo halijafanyika tayar Chama kimeingia katika mapambano mengine ambayo yanahitaji nguvu ya pamoja na umakini mkubwa sana

Kuonyesha kwamba bado Chama kingehitaji kujijengea misingi ya kukiimarisha kabla ya kwenda kwenye hatua ya pili ya No Reform No Election,ni kuibuka kwa kundi linalo jiita G55

Hili ni kundi moja ambalo limethubutu kupaza sauti na kujitoa mhanga lakini naamini nyuma yake kuna watu kama hao wengi ambao naamini kabisa wanaunga mkono ajenda ya G55

Kama Chadema kingeweka ajenda ya NRE pembeni kwanza na kujikita kuimarisha chama kwa maana ya kutoa tofauti zote na majeraha baada ya uchaguzi ingekuwa ni move nzuri sana kuelekea katika mapambano makubwa zaidi

Lakini kama Chadema kingeamua kushiriki Uchaguzi pamoja na changamo nyingi,bado kingepata viti kadhaa serikali za mitaa na viti vya ubunge na hivyo kuwa na sauti katika kuchagiza uwepo wake na uhamasishaji wake kisiasa

Lakini kwakupata viti bungeni kungesaidia kwanza kuwa na ushawishi kama Chama kwakuwa sauti yake itasikika zaidi na pili wangepata ruzuku ambayo ingewawezesha kusaidia harakati zake za kuimarisha shughuli za Chama

Nachelea kusema kwamba kwa siasa za nchi hii Chadema haitaweza kuzuia Uchaguzi na badala yake kitakuwa kimejichimbia kaburi lake lenyewe

Na wananchi wa nchi hii sio wajasiri kama wa nchi ya jirani,lau wangekuwa wajasiri wangeweza kuleta mabadiliko ya maandamamo yasiyo na ukomo lakini sio wananchi wa Tanzania hii ninayo ijua

Mda Utaongea

Ni hayo tu!
 
Hakuna kitu kama hicho mkuu.huwezi kuwa na timu ya mpira bila kushiriki ligi ukajiona una timu.mazingira ya timu kucheza hayapo sasa timu ya nini??Kinachitakiwa ni kila mtanzania kujua kuwa tumetekwa na sisi wananchii wote wa Tanzania ndio tuna shida sio chadema.
 
Mtazamo wako unaheshimiwa ila hili jipu lilishaiva kitambo tangu 30yrs ago, kuahirisha mambo ni hulka ya mtu mweusi kufikiria kila kitu kiwe kesho, hii itabadilisha attitude, wacha tuone tunalamba mtori nyama zipo chini! Nchi ilishakosa wafanya maamuzi, kila mtu anaogopa so anapoibuka mtu wa kusonga mbele tuache asonge!
 
View attachment 3316077

Ni mara chache sana huwa naandika kuhusu Siasa,na niweke wazi huu ni mtazamo wangu kama ambavyo nawe unaweza kuwa na mtazamo wako

Binafsi naona hii movement ingesubiri kwanza kwasababu moja kubwa,ni hivi majuzi tu Mheshimiwa Tundu Lissu ndio amechukua madaraka ya Uenyekiti wa Chama cha Chadema,hivyo basi angehitaji kwanza kujipanga na kuunganisha nguvu ya chama hasa ukichukua bado kuna majeraha kadhaa baada ya uchaguzi

Hii kwanza ingempa fursa ya kuweka mambo sawa ndani ya Chama pamoja na kutengeneza mazingira mazuri ambayo yatakuwa rafiki kwa kila mwana chadema ,kuwa familiar na sera na malengo ya Chama pamoja na kuwa na mipango thabiti katika kuchukua dola ya nchi hii

Chama kuwa imara ni pamoja na kutengeneza mifumo mizuri ya kupata pesa ambazo zitawezesha Chama kufanya shughuli zake za siasa bila kikwazo chochote kile,na hii inawezekana tu pale Kiongozi Mkuu atakapo unganisha nguvu ya Viongozi pamoja na Wanachama wake

Sasa kabla hilo halijafanyika tayar Chama kimeingia katika mapambano mengine ambayo yanahitaji nguvu ya pamoja na umakini mkubwa sana

Kuonyesha kwamba bado Chama kingehitaji kujijengea misingi ya kukiimarisha kabla ya kwenda kwenye hatua ya pili ya No Reform No Election,ni kuibuka kwa kundi linalo jiita G55

Hili ni kundi moja ambalo limethubutu kupaza sauti na kujitoa mhanga lakini naamini nyuma yake kuna watu kama hao wengi ambao naamini kabisa wanaunga mkono ajenda ya G55

Kama Chadema kingeweka ajenda ya NRE pembeni kwanza na kujikita kuimarisha chama kwa maana ya kutoa tofauti zote na majeraha baada ya uchaguzi ingekuwa ni move nzuri sana kuelekea katika mapambano makubwa zaidi

Lakini kama Chadema kingeamua kushiriki Uchaguzi pamoja na changamo nyingi,bado kingepata viti kadhaa serikali za mitaa na viti vya ubunge na hivyo kuwa na sauti katika kuchagiza uwepo wake na uhamasishaji wake kisiasa

Lakini kwakupata viti bungeni kungesaidia kwanza kuwa na ushawishi kama Chama kwakuwa sauti yake itasikika zaidi na pili wangepata ruzuku ambayo ingewawezesha kusaidia harakati zake za kuimarisha shughuli za Chama

Nachelea kusema kwamba kwa siasa za nchi hii Chadema haitaweza kuzuia Uchaguzi na badala yake kitakuwa kimejichimbia kaburi lake lenyewe

Na wananchi wa nchi hii sio wajasiri kama wa nchi ya jirani,lau wangekuwa wajasiri wangeweza kuleta mabadiliko ya maandamamo yasiyo na ukomo lakini sio wananchi wa Tanzania hii ninayo ijua

Mda Utaongea

Ni hayo tu!
TAKATAKA
 
nawaza tu napiga kakura kangu kamoja, alafu jamaa ana mbegi wa kura.

mbali na hivyo waziwazi wanakuambia mshindi wala hatokani na hizo kura mlizopiga

#NoReformsNoElection
Nimeipenda hii🤣🤣

Halafu mapema kabla kura hazijaanza kupigwa kuna box tayar limejaa kura😂😂
 
Hakuna kitu kama hicho mkuu.huwezi kuwa na timu ya mpira bila kushiriki ligi ukajiona una timu.mazingira ya timu kucheza hayapo sasa timu ya nini??Kinachitakiwa ni kila mtanzania kujua kuwa tumetekwa na sisi wananchii wote wa Tanzania ndio tuna shida sio chadema.
Hakuna mabadiliko bila kujitoa muhanga. Kama ni kushiriki chaguzi za kihuni, cdm imeshashiriki sana. Sasa ni wakati wa kutumia mbinu nyi gine. Kama maelezo yako ya kushiriki uchaguzi ni sahihi, mbona walishiriki juzi wa SM na bado ukanajisiwa? Au ww nadharia zako zinajiegemeza kwenye uhalisia gani?
 
Back
Top Bottom