Mtatiro afichua kilichomfanya ajiunge na CUF

Mtatiro afichua kilichomfanya ajiunge na CUF

Kama wewe ni mnafiki hutadumu katika Chama cha CUF ,hakuna kauli mbadala zaidi ya hiyo ,na zaidi mnafiki huyo huwa anahama kwa vishindo ,na hata wanachama mwanachama wa kweli hatoki kwenye CUF na kama wa kweli akitoka basi ujue tarudi.
 
sizani kama kuna mtu anaweza kurudisha kadi ya cdm kwa ccm au cuf huyu mtatilo aliyempa cheti pale udsm apelekwe mahakamani hastaili kuitwa eti mtu mwenye digrii huyu ndo anasababisha watu wengi kunifananisha mimi na watu wenye digrii ingawa elimu yangu ni std 7 pale vingunguti 'a' pr' school kwa ujinga wao
 
Mtatiro namkubali, wakati tupo Udsm tulikuwa tunaenda kulichimbisha wote pale bodi ya mikopo(tirdo) hadi nikapata boom..bravo jm
 
Mtatiro nimesoma nae Ifakara High school namtambua vema kama kilanja wa chakula alivyokuwa na roho mbaya, tukaenda nae UDSM namfahamu uwezo wake mdogo sana anaweza lopoka kama hapa ka-print kadi ya CDM hii inaonekana ni mpya kabisa yaani huyo mwanachama wa chadema alijiunga asubuhi... tena hata hakuikuja kadi jioni akairudisha CUF... shame on you Mtatiro, na nimemuona mdogo wako Malima CUF umempa shavu gani?

huyu jamaa wa CUF aliyeshika kadi ya CDM haamini alichoambulia...sisi tunaotokea maeneo ya uvuvi ni sawa na kutupa kokolo/wavu kwa nguvu sana na matokeo yake unapata samaki mmoja na ambaye hafai kuliwa, huyo ni sawa na ndg aliyepotea njia
 
Kujiunga kwake CUF ilikuwa ni wrong choice at a wrong time!

Aliingia CUF wakati Cuf ilikuwa imeshachakachuliwa na watu walikuwa tayari wameshaichoka.

Mtaji wao wa kisiasa huku Tanzania bara uliokuwa mikoa ya Tabora, Lindi, Mtwara na Tanga, kwa sasa karibu wote umeliwa na CHADEMA mara baada ya uchaguzi wa 2010.
 
2015 ni lipumba tena jamani?
Kweli kwa kuwa chama hakina mwingine!!!!
 
Ingawa sijui ana nafasi gani katika CUF lakini naajiuliza ilikuwa ni lazima ahutubie? Na kama ilikuwa ni lazima, hiyo ndiyo hotuba ailiyojiandaa kuwaeleza watu waliokusanyika hapo? Na kama ndiyo hotuba aliyojiandaa kuitoaa, ina tija gani kwa hao waliokuwepo, kwa chama chake na kwa taifa? Na tangu aingie chama kinachomfaa amefanya nini kusaidia taifa hili liondokane na matatizo ya ufisadi, mfumko wa bei, maisha ya shida ya Watanzania? Kukataa kwake kupewa nyumba na magari, kunalisaidia vipi taifa na hata majirani zake anaoishi nao ama wale wanaompa lift kama wapo? Narudia tena kujiuliza maswali yangu ya hapo juu.
 
Naibu katibu mkuu wa CUF chama cha wanachi Mh.Julius Mtatiro,amebainisha kwamba nchi inakuwa na viongozi mafisadi wengi kwa kuwa wengi hawana nia ya kuongoza ili kumkomboa mtanzanaia bali kukomboa matumbo yao.

Mh. Mtatiro aliamua kuweka wazi kile alichokiweka moyoni kwa muda mrefu kwamba kabla ya kujiunga na chama chochote cha siasa alifuatwa na vyama vyote vikubwa vya siasa hapa nchini wakimsahawishi ajiunge kwenye vyama vyao,lakini alivutiwa sana na ilani/itikadi , sera ya CUF kama alivyo tanabaishawa na Prof.Lipumba (mwanyekiti wa CUF ) ambaye ambaye alifanya mazungumzo nae, amabaye Mtatiro ansema yeye alikuwa tofauti na viongozi wa vyama vingine ambao walimuahidi,nyumba,gari,fedha na vyeo.”Hii haikuwa interest yangu mimi niliangalia chama gani chenye siasa za kweli na kinawatetea watanzania bila fix” alieleza Mtatiro.

mtatiro.jpg
Naibu Katibu mkuu wa CUF mh.Mtatiro akihutumia wananchi Ndungumbi,Makanya,Kinondoni

Mtatiro pia ameonya tabia ya viongozi wa Chadema ya kununua viongozi wa CUF kwa fedha nyingi kama wanavyofanya CCM.Mtatiro alisema kwamba tabia hii ianjenga viongozi wachumia tumbo na wasio na nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi ambao wengi wanakuwa mafisadi na wachumia matumbo.”Prof.Lipumba aliniambia -karibu CUF, hili ndilo neno ninalolikumbuka kwa kweli yeye ndiye aliyekuwa kiongozi pekee wa chama cha siasa ambaye hakujinadi kwa kutumia fedha.Kiufupi mimi huwezi kuninunua kama inavyofanyika kwa wengine kwani najitambua”aliongeza mh.Mtatiro

Naibu katibu mkuu huyo wa CUF aliendelea kutanabisha kwamba wanaushahidi wa sauti wa namna viongozi hao wa Chadema walivyokuwa wakihangaika kuwarubuni viongozi wa CUF mikoa ya kusuni kwa kutumia ahadi za kuwapatia fedha pale watakapohama CUF na kuhamia Chadema wakati wa ziara yao ya mikoa ya kusini hivi karibuni.

Mh.Mtatiro alitanabaisha hayo juzi kwenye mkutano wa hadahara uliofanyika uliofanyika kata ya Ndugumbi Kinondoni ambapo kada muhimu wa CCM alihamia CUF na kushusaha bendera ya CCM kwenye tawi lake na kupandisha bendera ya CUF na kuunda tawi la CUF Mkombozi.

Teh teh ,ningekuwa mtatiro nisingeongelea FIX kwani juzi tu wali weka Mchungaji feki. Nigekuwa mtatiro nisingesema suala la kununuliwa kwa CUF na CDM tena kwa kuongezea Kama CCM. kwani anathibitisha kuwa wao wanauzwa.Na CDM si pekee anayekwenda nunua,CCM alishatangulia.

Ila hakusema ukweli kuwa waliokuja CDM si wachumia tumbo, Kwani hadi sasa Prof Safari kaonyesha Thamani yake.
 
Mtatiro nimesoma nae Ifakara High school namtambua vema kama kilanja wa chakula alivyokuwa na roho mbaya, tukaenda nae UDSM namfahamu uwezo wake mdogo sana anaweza lopoka kama hapa ka-print kadi ya CDM hii inaonekana ni mpya kabisa yaani huyo mwanachama wa chadema alijiunga asubuhi... tena hata hakuikuja kadi jioni akairudisha CUF... shame on you Mtatiro, na nimemuona mdogo wako Malima CUF umempa shavu gani?

kweli jF ni hatari,kuna watu wan allergy na vitu fake.Hiyo kadi ni moja tuu,na hiaonyeshwi hadharani,inaweza kuwa ni upande mmoja tuu umepiga color copy
 
Naibu katibu mkuu wa CUF chama cha wanachi Mh.Julius Mtatiro,amebainisha kwamba nchi inakuwa na viongozi mafisadi wengi kwa kuwa wengi hawana nia ya kuongoza ili kumkomboa mtanzanaia bali kukomboa matumbo yao.

Mh. Mtatiro aliamua kuweka wazi kile alichokiweka moyoni kwa muda mrefu kwamba kabla ya kujiunga na chama chochote cha siasa alifuatwa na vyama vyote vikubwa vya siasa hapa nchini wakimsahawishi ajiunge kwenye vyama vyao,lakini alivutiwa sana na ilani/itikadi , sera ya CUF kama alivyo tanabaishawa na Prof.Lipumba (mwanyekiti wa CUF ) ambaye ambaye alifanya mazungumzo nae, amabaye Mtatiro ansema yeye alikuwa tofauti na viongozi wa vyama vingine ambao walimuahidi,nyumba,gari,fedha na vyeo.”Hii haikuwa interest yangu mimi niliangalia chama gani chenye siasa za kweli na kinawatetea watanzania bila fix” alieleza Mtatiro.

mtatiro.jpg
Naibu Katibu mkuu wa CUF mh.Mtatiro akihutumia wananchi Ndungumbi,Makanya,Kinondoni

Mtatiro pia ameonya tabia ya viongozi wa Chadema ya kununua viongozi wa CUF kwa fedha nyingi kama wanavyofanya CCM.Mtatiro alisema kwamba tabia hii ianjenga viongozi wachumia tumbo na wasio na nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi ambao wengi wanakuwa mafisadi na wachumia matumbo.”Prof.Lipumba aliniambia -karibu CUF, hili ndilo neno ninalolikumbuka kwa kweli yeye ndiye aliyekuwa kiongozi pekee wa chama cha siasa ambaye hakujinadi kwa kutumia fedha.Kiufupi mimi huwezi kuninunua kama inavyofanyika kwa wengine kwani najitambua”aliongeza mh.Mtatiro

Naibu katibu mkuu huyo wa CUF aliendelea kutanabisha kwamba wanaushahidi wa sauti wa namna viongozi hao wa Chadema walivyokuwa wakihangaika kuwarubuni viongozi wa CUF mikoa ya kusuni kwa kutumia ahadi za kuwapatia fedha pale watakapohama CUF na kuhamia Chadema wakati wa ziara yao ya mikoa ya kusini hivi karibuni.

Mh.Mtatiro alitanabaisha hayo juzi kwenye mkutano wa hadahara uliofanyika uliofanyika kata ya Ndugumbi Kinondoni ambapo kada muhimu wa CCM alihamia CUF na kushusaha bendera ya CCM kwenye tawi lake na kupandisha bendera ya CUF na kuunda tawi la CUF Mkombozi.
AKSANTE *Mh kumbe hata ninyi mlinunuliwa na CHAMA CHA MABWEPANDE sasa mbona unasema hununuliki wakati umo kwenye mtumbwi uliolipiwa?Angalia uLIkokwenda NDOANI UNGESEMA UNA ANGALIA NAMNA YA KUJINASUA HAPO TUNGE KUSIKILIZA NA KUKUSAIDIA.
 
Alikurupuka CDM haiwezi kununua mtu kutoka CUF labda aamue kujiunga nayo kwa ridhaa yake mwenyewe, maana muungano wa chama hiki na magamba huko zenji kimeiua hapa bara, rejea hata matokeo ya uchaguzi mdogo wa Igunga CDM haikusimamisha mtu mara ya kwanza, lakini kwenye by-election moto wake ulionekana, na mpaka sasa unaendelea maana ushindi wa kufoji wa Kafumu ulitenguliwa na mahakama.

kwa jinsi navyoijua cdm kutoa pesa kwa kununua viongozi si swala geni acha unafiki we unategemea kanda ya kusini cdm ikienda mikono mitupu nani atafika kukisikiliza na cdm haioni shida kumnunua kiongozi wa cuf iliaeneze cdm kusini bahati nzuri watu wa kusini waelewa hawana mpango na mafisadi wanyuma ya pazia
 
bado amelala huyo, akiamka atakuta CDM wameshachukua nchi. Ataungana na CCM kuendeleza kelele zake.
 
kwa jinsi navyoijua cdm kutoa pesa kwa kununua viongozi si swala geni acha unafiki we unategemea kanda ya kusini cdm ikienda mikono mitupu nani atafika kukisikiliza na cdm haioni shida kumnunua kiongozi wa cuf iliaeneze cdm kusini bahati nzuri watu wa kusini waelewa hawana mpango na mafisadi wanyuma ya pazia
No comment inawezekana ukawa na evidence, ni nani waliyemnunua na kiasi gani? weka uthibitisho in law oral evidence is not conclusive inatakiwa kuwa corroborated na documentary evidence or other evidence
 
Back
Top Bottom