MTANZANIA yakemewa bungeni

Mkuu shukran kwa kuscan hii habari, nimeisoma yote neno kwa neno. A lot of parliamentary boilerplate, but a lot of meaningful heated debate too.

1. Ndugai kwa kwenda kwenye kimjadala kisicho mizani na kujibishana na Tundu Lissu kama Naibu Spika, bila ya kuwa na uwakilishi rasmi wa CCM, na hivyo kutoa picha kwamba anawakilisha CCM, amedhalilisha bunge kuliko gazeti lolote linavyoweza kufanya.

2.Ndugai anajichanganya kwa kusema bunge linadhalilishwa, halafu hapo hapo kusema anajua kuna uhuru wa vyombo vya habari. Hivi huyu mwanasheria? Kama unajua kuna uhuru wa vyombo vya habari, na bado unasema bunge limedhalilishwa, inabidi uonyeshe kwamba bunge limedhalilishwa kwa kadiri ya kupita kiwango cha kawaida cha kubanwa na vyombo vya habari ili kulihasibu, hakuonyesha hili.

3. Habari nzima haionyeshi Ndugai kutaja specifics za udhalilishaji wa gazeti na kuzikanusha. Bunge si dini kusema haliwezi kusemwa. Hata hizo dini zinasemwa, mitume wanasemwa.

4. Kuna some very serious allegations ambazo nchi yoyote makini zingefanyiwa kazi. Mbunge amesema bungeni kwamba wabunge wa CCM wanawaambia wabunge wa upinzani kwamba wanapigiwa simu za vitisho kupitisha bajeti. Hili ilikuwa si suala la kusema tu, hili lilikuwa suala la kuliforce bunge kufanya uchunguzi na kuandika ripoti, nani anatoa vitisho hivi? Kwa maslahi ya nani? Kama kuna mtu anadhalilisha bunge basi ni huyu anayetoa vitisho kwa wabunge, lakini mbona hatusikii huyu kufuatiliwa ? Ndugai anabaki kutoa kanuni rejareja kushutumu magazeti tu?
 
Alipotoka Rostam hilo gazeti limebadili mwelekeo....ndio lilikuwa nambari one kuitukana cdm na dr. slaa wakati wa uchaguzi hiyo yote hawakuiona sio? wanakuja kuona la leo!!!!! Na bado.
 
Ukitaka kujua hii nchi viongozi wake ni viraza ndo kama hiyo Just imagine Badge imeshatangazwa then mtu anakurupuka tu eti serikali imeongeza bil 95 watanzania tujiulize hizo Hela zimetoka wapi?
 
huyu kilaza anatetea kibarua chake hakuna jingine
ni vema akagawa kipato anachopata kumhudumia mkewe aliyemtelekeza badala ya kuwapiga waandishi wanaoandika ukweli

hafu anaonekana kwao ni vilaza sana, tupen cv za huyu jamaa usikute ni kama ile ya jk!
 
Ni kweli wabunge hasa wa magamba ni nguvu ya soda, kwani hakuna maslahi yeyote ya wananchi wanayoyasimamia zaidi ya matumbo yao, ndo maana kila hoja kwao ni ndiyoooooooooooooooooooo. lakini sku zao zinahesabika wala si mbali sana
 
Leo asubuhi baada ya kipindi cha maswali Naibu Spika aliwasomea wabunge kichwa cha habari cha gazeti lililotoka leo ambalo ni MTANZANIA lenye kichwa kisemacho WABUNGE NGUVU YA SODA.

Ndugai alikerwa na habari hiyo kwamba inalidhalilisha bunge japo waandishi wanatumia uhuru wao wa kuhabarisha.

Alisema Bunge ni taasisi inayoheshimiwa na hivyo kuna haja ya kudhibiti uandishi wa aina ile.

Lakini akaongeza kwamba waandishi wanalipinga bunge kwa sababu wabunge wenyewe ndiyo wa kwanza kulipinga bunge lao badala ya kulitetea.

Binafsi sikutaka kusimuliwa nikalikimbilia gazeti hilo na nimeli-scan ili thinkers mjadili.

Scan iko katika page tatu na hivyo kuna document tatu za kudownload yaani Ndugai-01, Ndugai-02 na Ndugai-03.

Nimesita kwanza kuonyesha maoni au hisia zangu ili nisii-bias hii post ili ihukumiwe kwa haki humu JF.

Kazi kwenu.

Ni ajabu, sasa wabunge wanataka hata wakifanya madudu wasisemwe au wasifiwe tu. Mwambie Ndugai, enzi hizo zimepita za Mfalme kutembea uchi watu wakashindwa kumwambia mpaka mtoto mdogo aseme kuwa "mfalme yuko uchi"!! Heshima unajipa wewe mwenyewe. Mbona mwalimu anaheshimika hata huko kaburini. Alijijengea heshima. Bunge (Wabunge wa CCM hawana sifa hiyo) litasemwa tu. Pale mtakapo fanya vizuri mtaandikwa vizuri, pale mtakapofanya vibaya mtaandikwa vibaya.
 
Bunge ni chobo cha heshima. Lakini heshima inajengwa na waliomo ndani. Ni majadiliano ya tija, maamuzi ya tija nk yanayolipa bunge heshima yake. sasa kama wasikilizaji wanaona halina sifa hizo jamani watu wasiseme. Nadhani Bunge liwe na uvumilivu wa kukosolewa. Nguvu ya soda, ni kukamia kufanya kitu halali baadaye ukaacha kukifanya bila sababu zisizo za msingi. Sidhani kama bunge lilidhalilshwa, ni jinsi mwandishi alivyotoa tathmini yake. Na hili si dharau.
 
kaka! ndugai anapwaya sana kwenye hicho kiti! yani ccm walikosa mtu kabisa? mibinafsi hanifurahish kabisa! anavijembe sana! kama jana baada yawaziri mkuu kuongelea suala a arusha! yeye alimalizia kwakutupia kijembe! wanaboa sana!
MUNGU atusaidie 2015 tuwaondoe kabisa!
 
Tatizo la ndugai ni la jamíi kubwa.... pale anapyaya sana.. Aliyemwambia bunge linaheshimiwa nani utaheshimu vp watu au chombo kilichokosa mwelekeo, hakina tija, yaan ni sehemu ya wasanii tu... Semeni wenyewe wabunge wa bunge hili wanatofauti na Comedian wowote mlio wahi kuwaona.
 
waache ujinga, sasa kama ni nguvu ya soda inamaana wasiambiwe!

A dressed person if told by others that he is half naked he want care much, but a naked person if told by any person that he/she is naked for sure he/she will be angry because his/her assumption is that your shout is attracting attention of many viewers and that is his/her main worry. GOOD JOB MTANZANIA WE MISSED YOUR SERVICE FOR SO LONG!
 
Ndungai ni dodoki or sorry ni lapulapu (mhe.Ndungai usiseme na mm nimetumia uhuru wng vibaya).

WaTZ wengi wamepiga kelele juu ya gazeti hili na mengine yanayotoka NEW HABARI kuwa yanakiuka maadili but Serikali ikafumba macho, na kukimbilia kubamiza magazeti makini kama MWANAHALISI.

MTANZANIA lilifika mahali likaitwa "toilet paper" kwa kuandika hovyo. Kutukana wapambanaji na kutetea mafisadi. Mzee Mengi aliwahi kulipeleka mahakamani na likamwomba radhi mara mbili.

Lakini cha ajabu eti serikali ilikuwa haioni yote hayo inakuja kuona hili la bunge. Yani wakitukanwa Wananchi kimya, lakini ikiguswa serikali nongwa'?
Ama kweli KUNYA ANYE KUKU, AKINYA BATA KAHARISHA.

Kweli Ndungai ameonesha kiwango cha juu kabisha cha fikra chakavu.

Lakini wao wenyewe si ndio wamewafumbia macho haya makaratasi ya NEW HABARI kwa kumwogopa R.A.
Sasa wanaona athari zake eeeh.!!
Ama kweli mbwa akikuzoea sana anaingia nawe hata msikitini.
 
Unajua sasa na furahi sana Mtanzania linpogeika GAMBA lazima waambiwe ukweli hawa ,wemezoea sifa za kupika sasa wanachota aibu walizilimbikiza,walizoea kushangiliwa sasa wanachekwa kwa upumbavu waliouficha, eti sasa wasiambiwe ukweli?
 
Penye ukweli uongo hujitenga kilichozungumzwa na MTANZANIA ndio realy situation zama za kufichana ukweli zshapita.Ndugai kwa sasa anapwaya saana bora ata Anna Makinda anaonesha kajifunza na ukongwe unamsaidia ila uyo jamaaa mmmmmm kama Vuvuzela vle ila tym wil tel
 
Magamba walizoea kusifiwa na magazeti ya RA hata pale ambapo hawakustahili kusifiwa. Nami nime note kuwa magazeti ya new habari corporation yamebadili Stance. Ndugai na wenzake nafikiri haiwakeri hiyo habari ya nguvu ya soda bali trend ya gazeti hilo. Kikubwa wao wapprove otherwise sio kulitisha gazeti. Foka yote kuhusu wizara ya usafirishaji imeishia wapi!!


Naungana na wewe mkuu. Si uongo kuwa waandishi wetu wa habari wengi sio professioanal, hata kama wamesomea DSJ wengi wako below minimum requirements. Lakini the fact is, kuna sheria inayotakiwa kudhibiti magazeti, hiyo ndio inayotakiwa kecheck mwenendo wa magazeti na ya waandishi. Bunge kazi yake ni kutunga sheria zinazodhibiti mwenendo wa magazeti, kuanza kulikemea gazeti bungeni wakati kuna sheria na idara zimeundwa kwa kazi hiyo, haiingii akili.

By the way bunge linaonesha kuwa ni somekind of place where people will do all the talking and all the talking will result to nothing. Ndio maana mwandishi aliita ni nguvu ya soda.
 
Back
Top Bottom