abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
Written by administrator // 18/03/2011 // Kitaifa // 3 Comments
Salama Said,
JESHI la Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja linawashikilia watu 10, wanaosadikiwa kuwa ni majambazi ambao walikuwa kwenye maandalizi ya kutaka kupora katika hoteli ya kitalii ya My Blue, iliyoko Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini, Henry Mwibambe, alisema tukio hilo limetokea majira ya saa tisa usiku wa kuamkia jana, huko Nungwi ambapo hivi sasa matukio kama hayo yaliaza kupungua lakini sasa ameanza kujitokeza kwa kasi hasa huko Tanzania Bara.
Kamanda huyo aliwataja watuhumiwa wa ujambazi hao ni Andrew Henry Yussuf (24) mkazi wa Kigamboni Dar es Salaam, Abdullah Khatib Makota (33), mkazi wa Kiembesamaki, Khamis Msoma Masanja (31), mkazi wa Welezo, Faki Makame Faki (40) mkazi wa Kariakoo, Dar es Salaam.
Wengine ni Salum Seif Roto (30), mkazi wa Manzese Dar es Salaam, Lelo Michael Ringo (31),mkazi wa Tabata, Dar es Saalam, Said Juma Rashid (35) mkazi wa Magomeni Unguja, Msafiri Ali Mengi (25), mkazi wa Jangombe, Jeremia Joseph Michael (31), mkazi wa Dodoma na Khamis Kombo Juma (34) mkazi wa Tomondo Unguja.
Aidha Kaimu huyo alisema mmoja kati ya watuhumiwa hao alikamatwa akiwa amevaa sare za kamili za jeshi la polisi ambaye alikuwa katika kundi hilo la watuhumiwa hao.
Alisema mara baada ya majambazi hao kuingia katika hoteli hiyo walijaribu kuwapambana na walinzi wa hoteli hiyo kabla ya kikosi maalum cha kupambana na uhalifu kufika katika eneo hilo na kuanza kuchukua hatua za kupambana nao.
Kaimu kamanda huyo alisema hata hivyo katika kupambana na walinzi wa hoteli hiyo hakuna mtu aliyejeruhiwa hata mmoja, isipokuwa majambazi hao walitumia mapanga na kuwapiga mabapa walinzi hao kwa lengo la kuwatisha na kutaka watulie ili watimize azma yao hiyo ya uporaji.
Kaimu huyo ambaye ni Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai ya Mkoa huo, alisema Polisi walifanikiwa kuwakamata majambazi hao baada ya kupokea habari za uvamizi hu kutoka kwa wasamaria wema na dhana ya polisi jamii kufanya kazi.
Alisema baada ya polisi kuingia kwenye eneo la hoteli hiyo majambazi hao walijaribu kutoroka kwa kutumia gari yenye namba za uzajili Z 490 AV, Super Custom akuondesha kwa kasi.
Henry, alisema kukimbia kwao kwa kasi majambazi hao haikufanikiwa kwani waliwekewa kizuizi cha barabarani katika kituo cha polisi Nungwi ambapo kikosi cha kutuliza ghasia cha Mkoa huo kwa kushirikiana na polisi wa kituo hicho walifanikiwa kuwadhibiti na kuwaweka chini ya ulinzi mkali majambazi hao.
Alisema watuhumiwa hao wa ujambazi wamekamatwa wakiwa na silaha za jadi kama vile mpanga, ndondo, pamoja na koleo ya kuvunjia milango kwa lengo la kutaka kufanyia uhalifu wao.
Henry alisema watuhumiwa hao inasadikiwa kuwa ndio walioshiriki kuvamia hoteli ya kitalii ya Waridi iliyoko Pwani Mchangani Machi 17 mwaka huu majira ya usiku wa manane na kufanikiwa kuiba vitu kadhaa baada ya kuwafunga kamba walinzi wa hoteli hiyo na kutimiza azma yao.
Alisema kwamba watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani mara tu baada ya upelelezi kukamilika, huku Kaimu huyo akiwataka wananchi kushirikiana na Jeshi lake ili liweze kuvunja mtandao wa majambazi ambao umeanza kurudi upya hapa Zanzibar.
3 Comments on "Majambazi wakamatwa visiwani Zanzibar"
Salama Said,
JESHI la Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja linawashikilia watu 10, wanaosadikiwa kuwa ni majambazi ambao walikuwa kwenye maandalizi ya kutaka kupora katika hoteli ya kitalii ya My Blue, iliyoko Nungwi Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini, Henry Mwibambe, alisema tukio hilo limetokea majira ya saa tisa usiku wa kuamkia jana, huko Nungwi ambapo hivi sasa matukio kama hayo yaliaza kupungua lakini sasa ameanza kujitokeza kwa kasi hasa huko Tanzania Bara.
Kamanda huyo aliwataja watuhumiwa wa ujambazi hao ni Andrew Henry Yussuf (24) mkazi wa Kigamboni Dar es Salaam, Abdullah Khatib Makota (33), mkazi wa Kiembesamaki, Khamis Msoma Masanja (31), mkazi wa Welezo, Faki Makame Faki (40) mkazi wa Kariakoo, Dar es Salaam.
Wengine ni Salum Seif Roto (30), mkazi wa Manzese Dar es Salaam, Lelo Michael Ringo (31),mkazi wa Tabata, Dar es Saalam, Said Juma Rashid (35) mkazi wa Magomeni Unguja, Msafiri Ali Mengi (25), mkazi wa Jangombe, Jeremia Joseph Michael (31), mkazi wa Dodoma na Khamis Kombo Juma (34) mkazi wa Tomondo Unguja.
Aidha Kaimu huyo alisema mmoja kati ya watuhumiwa hao alikamatwa akiwa amevaa sare za kamili za jeshi la polisi ambaye alikuwa katika kundi hilo la watuhumiwa hao.
Alisema mara baada ya majambazi hao kuingia katika hoteli hiyo walijaribu kuwapambana na walinzi wa hoteli hiyo kabla ya kikosi maalum cha kupambana na uhalifu kufika katika eneo hilo na kuanza kuchukua hatua za kupambana nao.
Kaimu kamanda huyo alisema hata hivyo katika kupambana na walinzi wa hoteli hiyo hakuna mtu aliyejeruhiwa hata mmoja, isipokuwa majambazi hao walitumia mapanga na kuwapiga mabapa walinzi hao kwa lengo la kuwatisha na kutaka watulie ili watimize azma yao hiyo ya uporaji.
Kaimu huyo ambaye ni Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai ya Mkoa huo, alisema Polisi walifanikiwa kuwakamata majambazi hao baada ya kupokea habari za uvamizi hu kutoka kwa wasamaria wema na dhana ya polisi jamii kufanya kazi.
Alisema baada ya polisi kuingia kwenye eneo la hoteli hiyo majambazi hao walijaribu kutoroka kwa kutumia gari yenye namba za uzajili Z 490 AV, Super Custom akuondesha kwa kasi.
Henry, alisema kukimbia kwao kwa kasi majambazi hao haikufanikiwa kwani waliwekewa kizuizi cha barabarani katika kituo cha polisi Nungwi ambapo kikosi cha kutuliza ghasia cha Mkoa huo kwa kushirikiana na polisi wa kituo hicho walifanikiwa kuwadhibiti na kuwaweka chini ya ulinzi mkali majambazi hao.
Alisema watuhumiwa hao wa ujambazi wamekamatwa wakiwa na silaha za jadi kama vile mpanga, ndondo, pamoja na koleo ya kuvunjia milango kwa lengo la kutaka kufanyia uhalifu wao.
Henry alisema watuhumiwa hao inasadikiwa kuwa ndio walioshiriki kuvamia hoteli ya kitalii ya Waridi iliyoko Pwani Mchangani Machi 17 mwaka huu majira ya usiku wa manane na kufanikiwa kuiba vitu kadhaa baada ya kuwafunga kamba walinzi wa hoteli hiyo na kutimiza azma yao.
Alisema kwamba watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani mara tu baada ya upelelezi kukamilika, huku Kaimu huyo akiwataka wananchi kushirikiana na Jeshi lake ili liweze kuvunja mtandao wa majambazi ambao umeanza kurudi upya hapa Zanzibar.
3 Comments on "Majambazi wakamatwa visiwani Zanzibar"
utomvu 18/03/2011 kwa 7:15 um · Jibu
Hio ndo faida ya muungano tukisima muungano hauna faida kwa znz tunaonekana aaa tunataka kuvunja udugu, udugu udugu gani huo nakuvamiwa namijitu isiojua hata dini, vunja muungano weka pasport khalass.
asumani 18/03/2011 kwa 7:35 um · Jibu
Nani wa kulaumiwa?
makame silima 18/03/2011 kwa 8:45 um · Jibu
Haya yote yalikuwa hakuna Zanzibar, lakini tulipo ungana na wadudu hawa ndipo walipotuambukiza maradhi haya ya Ujambazi,Uhasharati wakujiuza mili na utapeli ambao udanganyifu huu umo hata ktk Muungano. Waungana na Juma Kecho unambiwa Umeungana na Yussf.
Na kuhusu Ujambazi mimi nazani hata huyu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini, Henry Mwibambe ni mmoja ktk hawa Majambazi,Zanzibar na Andrew wapi na wapi kama hili si jambazi la Tanganyika?.na nazani huyu Andrew Henry Yussuf nindugu yake wadamu.
Vunja Muungano turudishe hazi na mila zetu Wzanzibar tukisherewa watatupoteza hawa kitu utamaduni na ustarabu mwiko kwao.
Vitu tungane na watu matapeli wasio tekeleza makubaliano.