Mtambuzi mie, nishageuka Simba Mzee mchezewa sharubu...!

Mtambuzi mie, nishageuka Simba Mzee mchezewa sharubu...!

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,441
03_01_89346b.jpg


Ama kweli siku hazigandi, alijiimbia Lady JD.
Nikikumbuka miaka ile nikiwa kijana shababi mwenye siha nzuri, kipindi hicho, mkate wa Boflo kwa mpemba ulikuwa unauzwa hela kumi. Wakati huo sijakutana na Mama Ngina, wala hawa wanangu King'asti na Asnam hawajulikani duniani nilitesa sana na vibinti.

Nakumbuka wakati huo mabinti walikuwa wanatokelezea na magauni yao ya vitambaa vya Polister, Criplin au Chirmen walivyonunua kwa washihiri, wakati huo vitambaa vilikuwa vinapimwa kwa kipimo maarufu cha ZIRAA.

Nilikuwa kama Helikopter ndege isiyochagua mahali pa kutua. mambo yangu yalikuwa bambam na vijisenti mfukoni havikuwa vya kujibana, yaani nilikuwa nikimhonga mwanamke shilingi kumi atatangaza mtaa mzima. "Baba ana pesa yule kama njugu...!" Atasema kwa mashoga zake, kumbe ndio alikuwa ananipigia upatu, mabinti kuniwania.....

Sasa kiko wapi?

Mtambuzi nishageuka Simba Mzee aliyeshiba mizoga, vitoweo vinanichezea sharubu, mwenyewe nimebaki kuvikodolea macho. Nitoe wapi nguvu ya kuhimili sarakasi za mabinti wa siku hizi ambao wanataka kugeuzwa geuzwa kama samaki kikaangoni.

Kwa bahati mbaya sana mazingira ya kazi yangu achilia mbali hapa kazini kwangu kazi ninayofanya hunikutanisha na vimwana walioumbwa wakaumbika, na kujipamba na lebasi za ulimbwende pamoja na makochokocho chungu mzima. Ukichanganya na vivazi wanavyovaa, Oh mai.........! Utashangazwa na uumbaji wa Mwenye enzi Mungu.

Kutokana na macho yangu kukaa kihayawani. Ama kweli macho ya muasherati yana hila mbaya, hivi sasa nina bahati mbaya ya kusingiziwa na mabinti kuwa nawatongoza. Yaani nikizungumza na binti yeyote hapa kazini au popote pale huishia kunisingizia eti nimemtongoza...!

Hivi sasa hapa kazini kuna vita baridi miongoni mwa mabinti wakitupiana vijembe. Si mnawajua wanawake kwa mipasho...! Hivi majuzi wawili wametiana vidole vya macho, lahaula, kesi imefika kwa Meneja Rasilimali Watu. Mara simu hiyo napigiwa, mie huyo kwa Meneja Rasilimali Watu, nikijua tunaenda kuzungumzia mambo ya mafunzo kazini. He! Nafika, nakutana na mabinti wametumbuliana macho kama kuku mitetea inayogombea Koo (Jogoo).

Kesi iko Kilingeni.......

Hivi hawa mabinti wananitafutiani...?

Salaam hizi ziwafikie wapendwa wote wanaonitakia mema.... Raiza, Paloma, Zion Daughter, Asnam, Kipipi, King'asti, Lisa, Nivea, cacico, Elizabeth Dominic, charminglady, lara 1, Mrembo by Nature, vivian, Lusile, Jeska, Binti.com, Remmy, sweetlady, FirstLady1, FirstLady, MwanajamiiOne, Husninyo, Mamndenyi, mwaJ, Swts, Madame B, MadameX, Angel Msoffe, snowhite, gfsonwin, Preta, Nyamayao, marejesho, Asprin, Mwita Maranya, SnowBall, Roulette, jouneGwalu, HorsePower, Mungi, Erickb52, Don Mangi, Thomas Odera, Kipaji Halisi, Mentor, Kiranga, Nyani Ngabu, Bujibuji, Arushaone, Mzee mwenzangu Babu DC Dark City
 
ahahahahahhahahhahahhahhaahhah
sheemeeeejiiiih!
sasa hizo sahrubu zako si zina dhahabu!
natamanije sasa ningekuwa huyo meneja mjasiria watu!
na mi ningetaka nizichezee sharubu!
 
ahahahahahhahahhahahhahhaahhah
sheemeeeejiiiih!
sasa hizo sahrubu zako si zina dhahabu!
natamanije sasa ningekuwa huyo meneja mjasiria watu!
na mi ningetaka nizichezee sharubu!

Acha ushambenga na wewe....., sasa ndio unashadadia...? LOL

Sasa shemeji hivi FP yuko wapi? unajua nawadai nyie...?
 
Last edited by a moderator:
Kwa bahati mbaya sana mazingira ya kazi yangu achilia mbali hapa kazini kwangu kazi ninayofanya hunikutanisha na vimwana walioumbwa wakaumbika, na kujipamba na lebasi za ulimbwende pamoja na makochokocho chungu mzima. Ukichanganya na vivazi wanavyovaa, Oh mai.........! Utashangazwa na uumbaji wa Mwenye enzi Mungu.

Kutokana na macho yangu kukaa kihayawani. Ama kweli macho ya muasherati yana hila mbaya, hivi sasa nina bahati mbaya ya kusingiziwa na mabinti kuwa nawatongoza. Yaani nikizungumza na binti yeyote hapa kazini au popote pale huishia kunisingizia eti nimemtongoza...!
Mtambuzi.........pole sana kwa kusingiziwa!!!
 
Last edited by a moderator:
Mtambuzi mzee mwenzangu, pole sana! Najaribu kupiga picha kwa umri wako huo, umesimama mbele ya meneja rasilimali watu eti unasuluhishwa ugomvi, kisa vimwana wanataka kutoana macho kwa ajili yako!!! Nashindwa kupata picha sijui meneja wako atakuwa anafikiria nini kichwani mwake kuhusu wewe. Hatahisi kuwa ng'ombe hazeeki maini au pengine ndo yale ya usemi wa mababu kuwa wewe ndiye "Simba mwenda pole ..."?!
 
Kuna jamaa yangu aliniambia uitaka kuwakamata kuku wakusanye mahali pamoja ndo inakuwa raisi kuwakamat!naanza kuangalia ninani wakwanza kumkopi na wakatikati na wamwisho mimi nitaunganisha dot nitajua watz is wat!
CC Madame B nisaidie kwa tungo hii tata!! ila Mtambuzi unajua sima mzee anasubiria kisimani lazima kudu waje kunywa maji alafu unakamata kiulaini!!
gfsonwin, Paloma
 
hizo sharubu zako zilete nizipake Hina Mtambuzi hawatazishikashika tena just curious ulikuwa unashikwa sharubu za wapi vile!!!SHIKAMOO MTAMBUZI HERI YA PASAKA .
 
Last edited by a moderator:
Kuna jamaa yangu aliniambia uitaka kuwakamata kuku wakusanye mahali pamoja ndo inakuwa raisi kuwakamat!naanza kuangalia ninani wakwanza kumkopi na wakatikati na wamwisho mimi nitaunganisha dot nitajua watz is wat!
CC Madame B nisaidie kwa tungo hii tata!! ila Mtambuzi unajua sima mzee anasubiria kisimani lazima kudu waje kunywa maji alafu unakamata kiulaini!!
gfsonwin, Paloma
KakaKiiza shikamoo!!!
sijui nibadilishe lense nitumie mbonyeo.....maana naona wa kwanza kuwa mentioned ni Raiza,......... gfsonwin ni wa 31..............wakati Mtambuzi ametag watu hamsini!!!
hakyanani hizi ndio hasara za kusoma senti kayumba................ngoja nirudie mtihani wa fomfoo!!!
 
Last edited by a moderator:
KakaKiiza shikamoo!!!
sijui nibadilishe lense nitumie mbonyeo.....maana naona wa kwanza kuwa mentioned ni Raiza,......... gfsonwin ni wa 31..............wakati Mtambuzi ametag watu hamsini!!!
hakyanani hizi ndio hasara za kusoma senti kayumba................ngoja nirudie mtihani wa fomfoo!!!
Wakwanza geresha wapili hadi wa8 unaweza kupata jibu na katikati unachukua banchi la wati 10 pia halafu mwisho unaanzia wakwanza kutoka mwisho hadi wa 12 pia kutoka mwisho ukiunganisha unapata script!
 
hizo sharubu zako zilete nizipake Hina Mtambuzi hawatazishikashika tena just curious ulikuwa unashikwa sharubu za wapi vile!!!SHIKAMOO MTAMBUZI HERI YA PASAKA .
Zikipakwa hina si ndio zitawavutia, hebu niepushie hilo balaa we Nivea...
 
Last edited by a moderator:
Hahahaahahahaahaaaaaaaa!!!!!!
Umepatikana ndugu yangu Loh!
macho yamekutoka utafikiri mjusi kabanwa na mlango,
Wakati unawatania ulifikiri na wao watajua ni utani
Alafu Mtambizi inaonyesha wewe mtaalamu wa kuwakamata ihali umri umeenda.
Hakikisha hugeuzwi geuzwi kama samaki kwenye kikaango maana unaweza teguka kiuno ukaanza kutembea kiupogo upogo kama gari imekatika cental Bolt.
 
Sasa kiko wapi?

Mtambuzi nishageuka Simba Mzee aliyeshiba mizoga, vitoweo vinanichezea sharubu, mwenyewe nimebaki kuvikodolea macho. Nitoe wapi nguvu ya kuhiminili sarakasi za mabinti wa siku hizi ambao wanataka kugeuzwa geuzwa kama samaki kikaangoni.

Mkuu ngombe hazeeki maini! wachape nao tu!:msela:
 
Wakwanza geresha wapili hadi wa8 unaweza kupata jibu na katikati unachukua banchi la wati 10 pia halafu mwisho unaanzia wakwanza kutoka mwisho hadi wa 12 pia kutoka mwisho ukiunganisha unapata script!

You dont make any sense!!! unahitaji kurudia mtihani pia wa fomfoo!

next kweshen - unapata script gani KakaKiiza?!?!
 
Back
Top Bottom