Dr. Said
Senior Member
- Nov 16, 2010
- 112
- 501
Hello ndugu.Habari zenu jamani.
Kwanza nikiri kwamba naandika post hii huku kichwa kinaniuma. Toka nimepata hii pesa (600k nimeuza mali, 400k nimekopa) nimeumiza sana kichwa biashara gani ntafanya ili niendeshe maisha?
Kiukweli sitafuti faida ya haraka haraka, nataka tu nipate chochote ili nilipe kodi na kum-support mzazi mwenzangu maana nimesota sana baada ya kupoteza kazi.
Niliwaza biashara hizi (zifuatazo) lakini nikaacha hayo mawazo kwa sababu zifuatazo.
Saloon - flemu, vifaa, furniture. Nikaona pesa haitoshi.
Mobile money - flemu, leseni, float. Pesa haitoshi.
Mgahawa - flemu, (viti na meza), vyombo. Na nikizangatia hakuna biashara inayolipa ndani ya siku chache za mwanzo nikaona pesa haitoshi. Nitakula msingi.
Biashara ambayo naiwaza sasa hivi ni kunnua simu, hata nikianza na tatu kisha niziuze tu mtaani. Kama kuna mtu ashawai fanya hivi naomba mawazo yenu. Na risk zake ni zipi ?
Lakini kama idea yangu si nzuri, naombeni mnishauri idea nzuri maana kichwa kinauma sana.
Huhitaji mtaji (au mtaji mkubwa) kuanzisha biashara.
Bali unahitaji taaluma ya kusoma matatizo ya soko pamoja na namna ya kutatua matatizo hayo.
Baada ya hapo unatakiwa kuweza ku test soko lako bila ya kupoteza pesa nyingi.
Kama soko linalipa, unajikita katika hilo soko na kujenga biashara. Kama hali lipi unaenda kwenye soko jengine.
Unaweza kuangalia video hii kujifunza zaidi:
View: https://youtu.be/oN9ZQWzAoxk?si=e8zdoasxhitqg6fU
Vile vile tunayo kozi ya bure mtandaoni tunafundiaha yote hayo.
Kama utapenda kujisajili unaweza kwenda hapa Wazo Fasta