Mtaji wa CCM unapo back fire

Mtaji wa CCM unapo back fire

DARKMAN

Senior Member
Joined
Aug 23, 2012
Posts
122
Reaction score
86
Kwa muda mrefu CCM imekuwa ikitumia 'ujinga' kama tatizo la kimkakati la kuendelea kubaki madarakani. Ni ukweli usiopingika kuwa sababu ya ujinga unaotokana na umasikini kukithiri katika sehemu kubwa ya jamii, hata wakati wa kampeni za uchaguzi CCM imekuwa ikifanya jitihada za makusudi kutengeneza ajenda na propaganda ambazo ni wajinga tu wanaoweza kumeza. CCM imekuwa ikinufaika sana na hali ya ujinga na umasikini uliokithiri katika jamii. CCM imekuwa ikikwepa kwa juhudi zote kampeni kuongozwa na hoja (issues based), ndio maana inakataa mijadala katika kushindanisha wagombea.

Sasa CCM imekuja na mpango wa kusafirisha gas kutoka mtwara kwenda DSM, wapinzani wamewalisha wananchi propaganda za aina ileile kama ambazo CCM huwa wanazitumia. Ukisikiliza hoja zinazotolewa na wananchi huko mtwara ndio utajuwa kweli kazi ipo. Mtu anasema kwanini hawakusafirisha maji kutoka kidatu hadi DSM halafu hiyo mitambo ya umeme ikajengwa DSM, Kwa mjinga hii ina mantiki sana. Sasa eti CCM saa hizi ndio inataka wananchi wa mtwara watumie akili kufikiri ili waone mantiki ya serikali katika kusafirisha gas,too late subirini watu wafe tu kwa sababu ni mbegu mliyoipanda. kama mngetaka jamii ambayo inayoweza kujenga hoja mngeitengeneza.

Kama CCM wangejishugulisha kutoa ujinga katika jamii, hili bomba la gas wala tusingebishana kuhusu kulijenga labda tungebishania mikataba yake imekaaje na itawanufaishaje wananchi
 
2005 ccm ilitumia ubaguzi kwa kumdhalilisha waziri mkuu mstaafu,salim ahmed salim kwa kusema ni muarabu,ccm hiyo hiyo 2012 imemteua mwarabu mweusi(msomali)abdurahamani kinana.kinana ni mmoja wa wamiliki wa kampuni yenye tender ndani ya bomba la gesi mtwara dar,ccm chini ya kikwete imempa kazi kinana kuendeleza na kulinda wizi wa rasilimali ya nchi.serikali ya ccm chini ya kikwete inatumia polisi kukandamiza demokrasia kwa kuzuia mikutano mingi ya chadema kwa kisingizio cha kutokuwa na polisi wa kutosha.lakini wanaposisitiza kuwa wataendelea na mikutano yao idadi kubwa ya polisi inasambazwa kwa kuzuia mikutano yao.
Sasa litakalotokea tanzania ni umwagaji mwingi wa damu hadi kufikia 2015 sababu serikari chafu ya ccm haisikilizi wananchi bali inawalinda wachache wao wezi wa mali ya taifa letu,tumeona polisi wakiuwa raia kuanzia arusha,tabora,morogoro,mbeya ,songea na hakuna aliyechukuliwa hatua yeyote kwa mauwaji hayo.wananchi sasa wameanza kujibu mapigo kwa kuua askari,na kuna taafifa kuwa sasa ni jino kwa jino raia wakiuwawa na polisi mchana raia watauwa polisi usiku sasa amani iko wapi kama si ubaguzi uaolelewa na serikari ya ccm?
Mod ukiifuta hii habari nitakuwa nairidisha kila kukicha kwa watu mbalimbali mpaka ujumbe huu uenezwe kwa wapenda amani kote tanzania
 
Back
Top Bottom