Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,770
- 59,118
Juzi kuna mtu (mwanamke) alikua analalamika jinsi mume wake alivyosababisha mpaka akabadilika na kua tofauti kabisa na alivyokua mwanzo....wapo waliounga mkono...waliotoa pole pia kushauri.Tatizo ni kwamba ile mada ilikua inatetea wanawake na kuponda wanaume.Sasa je wanaume wao ndo hawakutwi na situation kama hizo!?!Wangapi wanakua walevi baada ya muda ndani ya ndoa?! Wangapi wanakua na hasira za haraka ambazo hazikuwako mwanzo?! Wangapi wanakimbia nyumba zao walizozipenda mwanzo!!?!Mwangapi wanakua wachachu (bitter) tofauti na kabla ya ndoa??!!Na nyie wadada/wamama hua mnawafanya nini mpaka wababa/kaka zetu wanabadilika na kua hivi?!Na inapotokea hua mnafanya jitihada gani kuwasaidia warudie hali zao za kawaida kabla ya kuanza kulalamika fulana kawa mlevi mara sijui mkorofi?!Samahanini kwa maswali mengi ila jamani kuweni waungwana kwa wenzi wenu.Kama hutaki abadilike katika hali ambayo ni chanya kuelekea hasi jitahidi usiwe kisababishi cha yeye kua hivi!!Na ikitokea kua responsible na tafuta suluhisho badala ya kulalamika!!!