Msingi wa Amani bado ni Haki

Wateule

JF-Expert Member
Sep 17, 2010
390
368
Amani na usalama wa raia hautokuja kupatikana kama nchi inaendeshwa kijanjajanja. Msingi wa amani ya kweli unabaki kuwa HAKI. Kubadilisha IGP na kuamini kwamba huyo ndio mwenye mbinu za kupambana na uhalifu, ukiwemo wa kuua askari, ni kujidanganya. Tatizo awamu hii ni kwamba nchi inaendeshwa kiupendeleo au kama wengine walivyoita "double standard" na kibabe. Cha kusikitisha askari wetu ndio wamekuwa wanatumika kuendeleza ubabe huo huku mkuu akiendeleza "double standard" (mfano, issue ya Bashite).

Katika mazingira kama haya, nasikitika kusema kwamba tutaendelea kushuhudia na kusikia matukio ya ajabu kila wakati....matukio ambayo yanakusudia kulipa visasi, kuleta hali ya sintofaham, na kukomoana. Dawa sio IGP mpya, dawa ni kwa serikali kusimamia HAKI na kutoa HAKI. Isitoshe mpaka sasa kazi kubwa inayofanywa na rais wetu tena kwa uweledi mkubwa ni kuteua na kutengua tu.
 
Amani na usalama wa raia hautokuja kupatikana kama nchi inaendeshwa kijanjajanja. Msingi wa amani ya kweli unabaki kuwa HAKI. Kubadilisha IGP na kuamini kwamba huyo ndio mwenye mbinu za kupambana na uhalifu, ukiwemo wa kuua askari, ni kujidanganya. Tatizo awamu hii ni kwamba nchi inaendeshwa kiupendeleo au kama wengine walivyoita "double standard" na kibabe. Cha kusikitisha askari wetu ndio wamekuwa wanatumika kuendeleza ubabe huo huku mkuu akiendeleza "double standard" (mfano, issue ya Bashite).

Katika mazingira kama haya, nasikitika kusema kwamba tutaendelea kushuhudia na kusikia matukio ya ajabu kila wakati....matukio ambayo yanakusudia kulipa visasi, kuleta hali ya sintofaham, na kukomoana. Dawa sio IGP mpya, dawa ni kwa serikali kusimamia HAKI na kutoa HAKI. Isitoshe mpaka sasa kazi kubwa inayofanywa na rais wetu tena kwa uweledi mkubwa ni kuteua na kutengua tu.
Wateule, mimi nakubaliana na wewe.
Ni haki, haki, haki, haki

Ukiondoa hilo amani huwa ni ndoto za mchana!
 
Back
Top Bottom