Tunawasikia watawala wakiomba watanzania tutunze amani yetu. wakati hadi sasa hatujapata majibu sahihi ya watu kutekwa

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,843
31,054
Kuna "contradiction" ya hili neno amani namna inavyotafsiriwa na hawa watawala wetu, wakati mambo yanayoendelea hapa nchini, mara Kwa mara tunawasikia watawala wakirudia msemo huu wa kuwaomba watanzania tutunze amani yetu tuliyojaaliwa na Mungu Kwa nguvu zote, wakitolea mifano wa nchi nyingine hata za jirani, kuwa amani huko nchini kwao imetoweka.

Hivi hiyo amani Gani iliyopo hapa nchini wanayoongelea hao watawala wetu, wakati hapa nchini, tayari amani ishatoweka Kwa watu kutekwa na baadaye kuuawa kama ilivyotokea Kwa kiongozi wa CHADEMA,Ali Kibao kuuawa kinyama na huyo Rais wetu, hataki kuunda Tume huru ya kuchunguza kifo hicho chenye utata mkubwa??

Hivi amani Gani wanayoongelea hawa watawala wetu, wakati Rais wetu hataki kuunda Tume huru ya kuchunguza, kutekwa viongozi wa CHADEMA, akina Soka, ambao mpaka sasa hawajulikani walipo?

Kwa hiyo Kwa tafsiri yangu, tayari amani hapa nchini, ishatoweka na tunapaswa nchi yetu tuwekwe kundi Moja na hizo nchi ambazo amani kwao ilishatoweka kitambo!

Iwapo tu nchi yetu itakuwa inataka amani hiyo irejee, basi Rais wetu anapaswa aunde Tume huru haraka iwezekanavyo ya kuchunguza matukio haya Ili watu hao wafahamike na kuburuzwa Kwenye vyombo vya sheria na tuwajue ni kina nani hao wanaohusika na matukio hayo ya kikatili sana

Vile vile ni lazima, Waziri wa Mambo ya ndani, Yusuph Masauni na mwenzake, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camilius Wambura, wajiuzulu mara moja Kwa kushindwa kuwalinda raia na Mali zao, ambao ni wajibu namba Moja ya majukumu yao.

Niwaambie hao viongozi niliowataja kuwa kulinda amani ya nchi yetu hakutokani na Jeshi la Polisi, kufanya doria katika Jiji hili la kibiashara la Dar, Kwa kurandaranda Kwa askari hao kuwa na silaha za kivita na magari ya washawasha, Bali tunawataka wao watulinde na hao watu wanaotambulika kuwa ni watu wasiojulikana Ili wasituteke tena na kutuua kinyama na hapo hapo, hao Jeshi la Polisi, pamoja na vifaa vyao vya kisaasa walivyo navyo waendelee tu kutuambia kuwa hao watu wasiojulikana, wameshindwa kuwabaini ni wakina nani??😳

Soma Pia:
 
Watu wasiojulikana ni haohao polisi na inawezekana waliopotea hao viongozi wa chadema ikawa wamewaua ndiyo maana wametumia nguvu kubwa kuzuia maandamano sababu hawana uwezo tena wa kuwarudisha waliowateka na kuwaua.kutokana na tukio la kibao limethibitisha pasipo na shaka wanaojiita wasiojulikana ndiyo haohao wanaozuia watu kuandamana
 
Watu wasiojulikana ni haohao polisi na inawezekana waliopotea hao viongozi wa chadema ikawa wamewaua ndiyo maana wametumia nguvu kubwa kuzuia maandamano sababu hawana uwezo tena wa kuwarudisha waliowateka na kuwaua.kutokana na tukio la kibao limethibitisha pasipo na shaka wanaojiita wasiojulikana ndiyo haohao wanaozuia watu kuandamana
Ni kweli kabisa unachoongelea.

Huwa najiuliza hivi ni Nini kinachomshinda Rais wetu kuunda Tume huru ya kuchunguza hiki kifo Cha Mzee wetu Ali Kibao na haya matukio ya hao waliotekwa na hao watu tunaoambiwa kuwa ni watu wasiojulikana??

Kama sio wao "manjago" kuwa ni wahusika wakuu wa matukio yote haya, kumbe ni nani waliofanya vitendo hivyo vya kinyama??😎
 
Kwa hiyo Kwa tafsiri yangu, tayari amani hapa nchini, ishatoweka na tunapaswa nchi yetu tuwekwe kundi Moja na hizo nchi ambazo amani kwao ilishatoweka kitambo!
Mkuu Mystery, despite all the odds, Tanzania bado ni kisiwa cha amani licha ya hayo matukio machache ya uteiaji, upotevu na mauaji ambayo ni isolated cases za hapa na pale.

Kwa vile yanafanywa na watu wasiojulikana, ili kuyakomesha matukio haya ni kwanza tuwajue hawa wasiojulikana kama ni wasiojulikana kweli au ni 'wasiojulikana' Shambulio la Lissu: Wajue wasiojulikana watakaojulikana na 'Wasiojulikana' ambao kamwe, hawatajulikana

Kuna watu wanawadhania wasiojulikana hawa ni wale 'jama zetu', tumewashauri TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!

Kwa vile serikali yetu imeshindwa kuwabaini, tumetoa wito WanaJF, je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi?

Serikali yetu imekomaa kuwa inaweza!, thiamine tuipe muda wa kutosha.

Ila kiukweli amani tunaitunza na kuilinda kama mboni ya jicho letu ndio maana tunatumia gharama kubwa sana kwenye prevention ya kuzuia fujo kuliko watu kuja kuigharimia kwa machozi, jasho na damu.
P
 
Tanzania bado ni kisiwa cha amani despite hayo matukio machache ya isolated cases za hapa na pale.

Kiukweli amani tunaitunza na kuilinda kama mboni ya jicho letu ndio maana tunatumia gharama kubwa sana kwenye prevention ya kuzuia fujo kuliko watu kuja kuigharimia kwa machozi, jasho na damu.
P
Paskali, hivi amani Gani tunayoilinda, wakati watu wetu wanaendelea kutekwa na hawa watawala wetu, hawataki kuchukua hatua madhubuti za kukomesha unyama huo??

Tumemwambia Rais Samia aunde Tume huru ya uchunguzi, Ili wahalifu hao wafahamike, lakini Cha ajabu inaelekea Rais Samia, hataki kuunda Tume hiyo huru!

Hivi unapata tafsiri Gani hapo Paskali??😳
 
Paskali, hivi amani Gani tunayoilinda, wakati watu wetu wanaendelea kutekwa na hawa watawala wetu, hawataki kuchukua hatua madhubuti za kukomesha unyama huo??

Tumemwambia Rais Samia aunde Tume huru ya uchunguzi, Ili wahalifu hao wafahamike, lakini Cha ajabu inaelekea Rais Samia, hataki kuunda Tume hiyo huru!

Hivi unapata tafsiri Gani hapo Paskali??😳
Kuna vitu mtu mwenye akili timamu wala hujiuluzi ni nani!, utaundaje tume kujichunguza kitu unachokijua?!.

Sisi watu wa kusaidia tunaendelea kumsaidia huyu Mama, ili kumuepushia na bakra za karma za matendo maovu ya watu wake kwa kumtumia mtangulizi wake kama shamba darasa, kama ni kushauri, tumeshauri sana tuu
Mwisho wa siku anayewajibishwa na karma ni mamlaka ya mwisho yenye uwezo wa kufanya kitu lakini haikufanya!.
P
P.
 
Wanatufanya watoto sana majuha na mazezeta
Huyu Mama ninamshangaa sana.

Yeye anatuhimiza watanzania tulinde amani, wakati huo huo vyombo vyake vya ulinzi na usalama ndiyo "Main suspects" wa kadhia yote hiyo ya utekaji na uuwaji.

Tunamwambia aunde Tume huru ya uchunguzi, anashikwa na "kigugumizi" kuunda Tume hiyo😳

Hivi huyu Mama anataka tumueleweje??
 
Sisi tayari tumekamilika kuwa species tofauti..ukitaka kujiridhisha mtafute askari polisi aliyestaafu ..huwa wanakuwa na hali mbaya sana kisaikolojia!
Hiyo ni laana inayotokana na kuwatesa wananchi wasio na hatia
 
Mabeberu ndio wale wanaosema tukiwapoteza polisi musiwatafute makofi kwa CCM?.
Inashangaza Kwa huyo Mwenyekiti wa UVCCCM, wa Mkoa wa Kagera, aliyetoa kauli ya uvunjifu wa amani kama hiyo, hajakamatwa Hadi leo, lakini CHADEMA wanaotaka kufanya maombolezo ya kiongozi wao aliyeuawa kinyama na viongozi wao kina Soka ambao Hadi leo hawajapatikana na kujulikana wako wapi, ndipo majeshi yanajitokeza na silaha za moto na kuwaambia CHADEMA kuwa hawaruhusiwi kufanya maandamano hayo!😳
 
Wanaposema tutunze Amani wanajua kuwa wao ndiyo wanaiharibu. Sisi tuitunze ili Kama vile walipomuuwa Mzee kibao wawe salama.
 
Back
Top Bottom