Msimamo wa Nyerere, Mareale UN ulikuwa mmoja

Ndikalawe

Inawezekana Mzee Peter Kisumo hakuwa mbali na ukweli. Nimetoa kipande kifuatacho kwenye Wikipedia:


http://http://en.wikipedia.org/wiki/Chaga_people

Hebu pima maelezo yake kisha utafsiri kama matukio haya yangeliwajengea uswahiba Nyerere na Marealle

Shukran


In 1952, the Chagga held an election to elect Mangi Mkuu, the "Paramount Chief", to look after their affairs and speak with colonial administrators on behalf of the Chagga.[2] Thomas Marealle of Marangu won the election, defeating divisional chiefs M. H. Abdiel Shangali of Hai and John Ndaskoi Maruma of Rombo. Another divisional chief, Petro Itosi Marealle of Vunjo, withdrew from consideration before the election.

Marealle consolidated power from the other three Chagga divisional chieftains, thus making the Chagga more powerful and in control of their own affairs. His capital was in Marangu.

But Marealle's downfall occurred during Tanganyika's struggle for independence, for two main reasons:First, He lost support among western educated people. When Chagga students at Makerere University criticized him in their college magazine, he publicly humbled them when they came home, in an "old" tribal way.[clarification needed] He placed his faith in Petro Njau, the elderly astute party organizer who had put him in. From 1958 Njau set himself the task of enlisting the support of the old conservatives and the clan elders. This was a spurious return to the great tribal past. But Mangi Mkuu believed and trusted implicitly in him, and in the exaggerated accounts of popularity which Njau reported.

Second, Mangi Mkuu crossed swords with T.A.N.U on his home ground of Kilimanjaro. He still supported the national aims of T.A.N.U for Tanganyika. He continued to support Julius Nyerere personally, as the national leader long after he had begun to deal summarily with local T.A.N.U critics at home, perhaps because these critics did not need to be taken seriously, since they were insignificantly unrepresentative of the people.

In 1957-58 the British Administration were belatedly trying to organize a council of Chiefs in Tanganyika as a delaying action against T.A.N.U, Mangi Mkuu wrote the governor asking that Nyerere himself should be invited to address the chiefs. The request was refused. It was not until 1959, when he was fighting for his political life, that Mangi Mkuu cut across Nyerere personally and cut across the national movement as such. In January 1959, by which time he was sharply on the defensive at home, Mangi Mkuu criticized Nyerere's visit to Moshi to hold an open-air TANU meeting in the town. A few months later he circularized the chiefs on the mountain, threatening to sack them if they supported TANU.

In the local field of Chaga politics, however the break came earlier. It did not come from TANU branches as such which, though they had started in 1955 on the mountain, had made little headway among the people. It came from Machame, from the chiefly rival whom Mangi Mkuu had supplanted in 1951. Chief Abdieli Shangali threw the weight of his authority behind his son-in-law, Solomon Eliufoo, and this was the decisive factor. Eliufoo, a commoner from one of the oldest clans in Machame, and a Lutheran-trained teacher, was abroad in the United States and Great Britain from 1953 to 1956. In 1957, he returned as a teacher and joined the TANU branch in Machame. In 1958, he entered politics; he became a nominated member of the Chagga Council, being nominated by Hai divisional council of which his father-in-law, Chief Abdieli Shangali, was chairman. The same year, he was elected member of the legislative council in Dar es Salaam on the TANU ticket.
Wickama,

..hapa nadhani national politics ziliingiliana na local politics.

..fuatilia kote ambako nime-highlight with red or black.

..Marealle alianza kwa kumshinda Shangali wa Machame ktk kuchagua Mangi Mkuu.

..baadaye Marealle akawa hana tatizo TANU au Mwalimu Nyerere.

..makala inasema " he[marealle] still supported the national aims of TANU for Tanganyika."

..tena wanaeleza kwamba alikuwa hata anam-support Mwalimu Nyerere "personally."

..mwaka 1957-58 Marealle aliandika barua kwa gavana akipendekeza Mwalimu Nyerere apewe nafasi ya kuhutubia Council of Chiefs. Hii council of Chiefs ilianzishwa na wakoloni kwa lengo la kupunguza kasi ya TANU. Marealle aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa hiyo Council.

..Pamoja na Marealle kuwa ktk council ya ma-chief, iliyoanzishwa na wakoloni, lakini bado tunaona anataka Mwalimu Nyerere apewe nafasi ya kuzungumza na machief na kuwasilisha hoja za TANU.

..Pia kuna taarifa kwamba hotuba ya Chief Marealle kule UN ilisisitiza matanio ya wa-Tanganyika kuwa huru.

..matatizo yalianza baada ya Abdieli Shangali,aliyeshindwa na Thomas Marealle ktk uchaguzi wa kumpata Mangi Mkuu,kuingia ktk siasa za TANU akim-support Solomon Eliufoo.

MY TAKE:

..Wamachame na Wamarangu wana matatizo yao ya kihistoria. Kuna kipindi jamii hizo mbili zilikuwa hata hazioleani.

..Kama TANU iliingia Uchagani kwa msaada wa familia ya Chief Shangali wa Machame,basi bila shaka kutakuwa na mgogoro na Chief Marealle wa Marangu.

..kwa mtizamo wangu tatizo halikuwa Uhuru wa Tanganyika, bali ni ule mgogoro wa Kihistoria kati ya Wamarangu na Wamachame.

..Kuna habari za kuanzishwa kwa Chama cha Siasa cha Wachagga na tetesi kwamba Mwalimu Nyerere alikuwa akikiunga mkono chama hicho,lakini baada ya kutimiza malengo yake akakitupa mkono.

cc Nguruvi3, Mag3, Kudi Shauri, Jasusi, Abunuas, Kishimbe wa Kishimbe, ilboru1995, Pasco
 
Wamachame na Wamarangu wana matatizo yao ya kihistoria. Kuna kipindi jamii hizo mbili zilikuwa hata hazioleani.

..Kama TANU iliingia Uchagani kwa msaada wa familia ya Chief Shangali wa Machame,basi bila shaka kutakuwa na mgogoro na Chief Marealle wa Marangu.

..kwa mtizamo wangu tatizo halikuwa Uhuru wa Tanganyika, bali ni ule mgogoro wa Kihistoria kati ya Wamarangu na Wamachame.

..Kuna habari za kuanzishwa kwa Chama cha Siasa cha Wachagga na tetesi kwamba Mwalimu Nyerere alikuwa akikiunga mkono chama hicho,lakini baada ya kutimiza malengo yake akakitupa mkono
joka,

Nisaidie kitu, Tunajua Nyerere alikwenda UN kwa tiketi ya TANU kuwatetea watanganyika kudai uhuru. Sasa, huyu Marealle alikwenda UN kudai nini kwa tiketi ya nani na agenda yake ilikuwa kwa maslahi ya kina nani tofauti na wale waliotetewa na JKN? Hapohapo tunaambiwa alikuwa anam-support Nyerere kisha strangely akapiga marufuku mikutano ya TANU mjini Moshi 1959?
 
Last edited by a moderator:
JokaKuu
Hili la Marealle na Nyerere kwa kadri ninavyolifahamu na kupitia machapisho linapotoshwa


Tofauti yao ilikuwa muda wa Tanganyika kujitawala na wala si kupinga uhuru.

Kutokana na mgogoro wa kihistoria uliousema ambao bado upo kichini chini wapo watu wanatumia fursa hiyo na kusema Marealle alipinga uhuru.

Hapa kuna tatizo lingine linajitokeza na hili lipo kwa Nyerere na viongozi wetu wengine.
Confusion yote hii ni kwasababu Mwalimu hakuandika ''Memoir' yeye mwenyewe na hivyo kutoa nafasi ya ''inasemekana'.


Nadhani unaona jinsi mzee wetu Mohamed Said anavyopotosha sehemu ya umma kwa hisia zake kwa vile hakuna kumbu kumbu rasmi zaidi ya masimulizi ya second and third party.

Kuhusu mzee Kisumo, nadhani muda umefika apunzike.

Siku za karibuni amejivunjia heshima yake sana kiasi kwamba ile credibility aliyoijenga miaka mingi imekuwa eroded vibaya sana.
 
Last edited by a moderator:
Kwa wale mnao changia hii thread i have to give you one thing to note kuhusu uhusiano wa Nyerere na siasa za Tanzania, na kwa nini kimantiki Nyerere asingeweza kupatana na either Mangi Marealle au Shaghali.

Point yenyewe ni hii. Wakati Nyerere anajanjaruka (ujanja wenyewe alipewa na wazungu), uchaggani watu walikuwa wameshajacharuka kabla yake. KWa sababu gani nasema hivyo. Wachagga teyari walikuwa na elimu na maarifa ya kutosha kuongoza serikali bila kuhitaji msaada wa mtu yeyote. Uchagani mifumo ya kiserekali ilikuwepo muda tangu na tangu. For your information, mifumo ya kiserekali imetokana na jamii zenye mifumo ya kilimo huko ulaya au asia. Jamii nyingi zilizookana na mifumo hii ya kijamii hata kwenye biashara ni wazuri popote pale duniani. Hivi ni vitu ambavyo vlilkuwepo uchaggani na maeneo ya jirani mpaka kwa wakikuyu. Organised agricultrure ndo imepelekea organised business tuliyo nayo leo.

Sasa swali linakuja hivi. Nyerere alikuwa anauwezo gani wakuongoza bila msaada wa watu makabila mengine? Alichokifanya Nyerere ni kukimbilia kwa waswahili, akajifanya yeye mswahili, na waswahili wanavyopenda sifa basi wakamtukuza kweli naye akapata kichwa. Waswahili wakitakakumzidi ujanja anakimbilia kwa wachagga, akiona wachagga wanataka kumzidi ujanja anakimbilia kwa waswahili. Hivyo hivyo ndivyo alivyoyafanyia makabila mengine kama wahaya. He was like an imaginary character kitu ambacho somehow kilimsaidia. Lakini laiti Nyerere angeenda na Uzanaki wake kulikuwa hakuna jinsi angeweza kukubalika au kufanya mambo aliyoyafanya.

Kwenye duru za siasa za ulimwengu wa leo, Nyerere kwa sasa namfananisha sana na Mch Mtikila. They are both like 'one man show'. Siasa za Nyerere, hata Mtikila, na kidogo Zitto alikuwa anaelekea huko, zilikuwa hazina interest yoyote ya kumtoa mwafrica kwenye umaskini bali kumtoa mwafrica kwenye kuonewa au kutawaliwa. Mwafrica wa leo anahitaji elimu, maarifa ya kisayansi na technologia ya viwanda. Mwafikra wa leo anahitaji mapinduzi ya kifikra ya kutokudhani kwamba kuna binadamu superior kuliko mwingine bali mwenye kujua kwamba mambo yote yanawezekana chini ya juua. Haya yote yanawezekana kwa kuwa na jamii imara yenye misingi bora ya kifamilia, kimalezi, kazi nk.

Kuna watu wanapenda kukaa na kuzungumza vitu hata wasivyo vielewa vizuri kuhusu wachagga. Waacheni Wachagga wenyewe wajieleze. Wanabaki kuzusha tu uzushi na hadithi zisizo za kweli. Ukiwauliza nia yao sidhani hata kama wanajua, zaidi ya stereotype mind. Ila ukweli utakuja dhihirika tu. Wachagga ni wapiganaji katika nyanja zote za maisha, hilo halina cha ubishi, na wameiipigania sana na kuitumikia sana hili taifa tangu kabla na hata baada ya uhuru, ni kwamba majina yao hayako kwenye rekodi kwa sababu they did not need it. Ila kwa sababu waswahili wanapenda kulalamikalalamika na kujikweza kweza hata kama ni kwa jambo dogo tu, basi makelele mengi kweli utasikia. Wao ndo wamejipa hati miliki ya nchi hii, kila kitu wao, ndo maana huyu mwingine anadhani uraihisi ni kupeana kula kwao, kila kitu bagamoyo.
 
Kuna watu wanapenda kukaa na kuzungumza vitu hata wasivyo vielewa vizuri kuhusu wachagga. Waacheni Wachagga wenyewe wajieleze. Wanabaki kuzusha tu uzushi na hadithi zisizo za kweli. Ukiwauliza nia yao sidhani hata kama wanajua, zaidi ya stereotype mind. Ila ukweli utakuja dhihirika tu. Wachagga ni wapiganaji katika nyanja zote za maisha, hilo halina cha ubishi, na wameiipigania sana na kuitumikia sana hili taifa tangu kabla na hata baada ya uhuru, ni kwamba majina yao hayako kwenye rekodi kwa sababu they did not need it. Ila kwa sababu waswahili wanapenda kulalamikalalamika na kujikweza kweza hata kama ni kwa jambo dogo tu, basi makelele mengi kweli utasikia. Wao ndo wamejipa hati miliki ya nchi hii, kila kitu wao, ndo maana huyu mwingine anadhani uraihisi ni kupeana kula kwao, kila kitu bagamoyo.

Nara;
Uhalisia wa maneno ni kuwa wachagga wako very organised kuanzia na family tasks hadi society wanayokaa. Ikiharibika ni huko baadae lakini sio huko walikotoka. Matunda ya kuwa organised yanaonekana sana kuwa haipo familia ya kichaga inamwachia mtoto kuwa "zoba zoba haeleweki". Kwa sababu hii mpaka kesho ni vigumu ukakuta vijana wa kichagga kwenye orodha ya "stow away" waliorudishwa toka ughaibuni au wabebaji wa madawa. Ni malezi. Zingatia kuwa wachagga ni makabila na dini tofauti. Wachagga ni testimony kuwa issue ya maendeleo sio uDINI ni BIDII binafsi.

URAIS. Binafsi naamini kuweka aina yoyote ya kizuizi (cha wazi au kificho) ili kwamba mtu mwenye kutambulika kama MCHAGA asiwe kiongozi wa nchi itakuwa ubaguzi wa kiJINAI na ni kinyume cha katiba ya nchi hii. Hakuna aliyechagua kuzaliwa kwenye kabila lake. Lakini mtu kama anatoka jamii ya kichagga akijenga imani kuwa SISI TUNAZUIWA KUWA MARAIS pia ni tatizo kubwa kwa nchi yetu kwa vile huenda tutakosa mzalendo tena mwenye kipaji na tija na maono ya kusaidia nchi. Hii ni hofu ambayo lazima tuivunje ili vijana wetu wa KICHAGGA, KIHAYA, NA KINYAKYUSA waitupilie mbali na kuacha kuishi na MYTHS. We need their talents and energies.

Tufanye nini?

1. Mimi nadhani ni muhimu sana vijana wa kichagga wakachapa kazi kama walivyo sasa bila hofu yoyote moyoni ya kubaguliwa wala unyonge

2. Ipo haja ya vijana wa kichagga kuwa kwenye safu za CCM kama wanachama na viongozi (why not?)kwa vile wengi wao wana vipaji vizuri na ni wachapa kazi wazuri lazima Mbele ya Safari mmoja wao atajawakilisha chama hicho kugombea urais, after all patience is the key. Kuna timu za premier league (UK au Bongo) hazijawahi pata ubingwa tangu ligi ianze lakini hazijatangaza kuchoka. Ni Kweli au uongo? (why the haste?)

3. Issues za kina Nyerere/Marealle/Abdulwahid/Bibi Titi huwa naziona kama ni za wakati HUO. Walichoweza sawa, walichoshindwa pia sawa. Hatutawarudishia uhai ili warekebishe dosari zao hata kama tukishinda tunawasema kwenye studio/websites zote duniani. Sisi Tu-focus nguvu zetu kwenye mahitaji yetu ya leo na kuweka mikakati ya kesho
 
joka,

Nisaidie kitu, Tunajua Nyerere alikwenda UN kwa tiketi ya TANU kuwatetea watanganyika kudai uhuru. Sasa, huyu Marealle alikwenda UN kudai nini kwa tiketi ya nani na agenda yake ilikuwa kwa maslahi ya kina nani tofauti na wale waliotetewa na JKN? Hapohapo tunaambiwa alikuwa anam-support Nyerere kisha strangely akapiga marufuku mikutano ya TANU mjini Moshi 1959?
Wickama,

..sina uhakika Chief Marealle alitumwa na nani.

..huenda alikwenda UN kuzungumza kwa niaba ya Machifu wenzake wa Tanganyika.

..kuna mahali Nyerere ananukuliwa aki-endorse hotuba aliyotoa Marealle huko UN. hapa nakushauri utafute maandiko wa mwanahistoria John Illife.

..sasa kwa msingi huo utaona kwamba Chief Marealle hakuwa na ajenda tofauti na Mwalimu Nyerere au TANU.

..kwa mtizamo wangu, Mwalimu Nyerere na Chief Marealle, walipishana baada ya Mwalimu kuanza kuwa karibu na maadui wa kisiasa[za uchagani] wa Marealle.
 
Last edited by a moderator:
Wickama,

..nadhani kuna wa-Tanganyika wengine zaidi ya Japhet Kirilo, Chief Marealle, na Mwalimu Nyerere, ambao walipata kuwasilisha petition mbalimbali dhidi ya Waingereza before the UN.
 
Last edited by a moderator:
Mnawawaza sana wachaga .....shame on u all ....hata mfanye mfanyavyo waliotangulia wametangulia tuu... Ukweli ni kwamba hata nyie mnaowaponda wachaga mnataman mngezaliwa wao....waacheni wenzenu wale maisha walijua elimu mapema wakat babu zetu wakiwasisitizia baba zetu kuchunga ng'ombe na kulima kwa jembe la mkono....wachaga kwenye kila sekta wako na ni ukweli usiojipinga kuwa wao kwa asili mia kuubwa wameichangamsha tz wakipeana tough na wahaya na wanyakyusa...fika kilimanjaro migomban magorofa kibao sio sisi had tuje dar ndio tuone majumba ya kifahar au wengne tunaishia kuziona kwenye bongo movies
 
Wickama,

..hapa nadhani national politics ziliingiliana na local politics.

..fuatilia kote ambako nime-highlight with red or black.

..Marealle alianza kwa kumshinda Shangali wa Machame ktk kuchagua Mangi Mkuu.

..baadaye Marealle akawa hana tatizo TANU au Mwalimu Nyerere.

..makala inasema " he[marealle] still supported the national aims of TANU for Tanganyika."

..tena wanaeleza kwamba alikuwa hata anam-support Mwalimu Nyerere "personally."

..mwaka 1957-58 Marealle aliandika barua kwa gavana akipendekeza Mwalimu Nyerere apewe nafasi ya kuhutubia Council of Chiefs. Hii council of Chiefs ilianzishwa na wakoloni kwa lengo la kupunguza kasi ya TANU. Marealle aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa hiyo Council.

..Pamoja na Marealle kuwa ktk council ya ma-chief, iliyoanzishwa na wakoloni, lakini bado tunaona anataka Mwalimu Nyerere apewe nafasi ya kuzungumza na machief na kuwasilisha hoja za TANU.

..Pia kuna taarifa kwamba hotuba ya Chief Marealle kule UN ilisisitiza matanio ya wa-Tanganyika kuwa huru.

..matatizo yalianza baada ya Abdieli Shangali,aliyeshindwa na Thomas Marealle ktk uchaguzi wa kumpata Mangi Mkuu,kuingia ktk siasa za TANU akim-support Solomon Eliufoo.

MY TAKE:

..Wamachame na Wamarangu wana matatizo yao ya kihistoria. Kuna kipindi jamii hizo mbili zilikuwa hata hazioleani.

..Kama TANU iliingia Uchagani kwa msaada wa familia ya Chief Shangali wa Machame,basi bila shaka kutakuwa na mgogoro na Chief Marealle wa Marangu.

..kwa mtizamo wangu tatizo halikuwa Uhuru wa Tanganyika, bali ni ule mgogoro wa Kihistoria kati ya Wamarangu na Wamachame.

..Kuna habari za kuanzishwa kwa Chama cha Siasa cha Wachagga na tetesi kwamba Mwalimu Nyerere alikuwa akikiunga mkono chama hicho,lakini baada ya kutimiza malengo yake akakitupa mkono.

cc Nguruvi3, Mag3, Kudi Shauri, Jasusi, Abunuas, Kishimbe wa Kishimbe, ilboru1995, Pasco


Ukichunguza historia ni vigumu kuona ni wapi machame imekuwa na mgogoro wa kihistoria na wamarangu. Machame ilipata matatizo na kibosho miaka ya mwisho ya 1880 ambapo Mangi Sina, mtawala wa Kibosho (ambaye yeye mwenyewe alikulia Machame) aliunda zengwe na kuuwa wamachame kadhaa kule Kibosho na kutumia fursa hiyo kuivamia Machame na kusababisha uharibifu na maafa makubwa. Tokea wakati huo wamachame na wakibosho walikuwa na uhasama wa kufa mtu. Kitendo alichokifanya Mangi Sina kilisababisha Kibosho kuingia kwenye mgogoro na Mangi Mandara wa Moshi (rafiki wa Mangi wa Machame) akisaidiwa na Mangi Marealle wa Marangu (kwa kumlazimisha) ambapo waliishambulia Kibosho kwa nguvu zote ingawa hata hivyo walishindwa vibaya.

Inaaminika kihistoria kwamba baadaye Mangi Marealle aliunda urafiki na Mangi Shangali wa Machame, ili yeye (kwa kuunda urafiki na wakoloni wa kijerumani baada ya kufariki kwa Mangi Mandara) awe mkuu kule mashariki ya uchagani na Machame irudi tena kwenye historia yake ya kuwa nguvu kubwa magharibi mwa uchagani (baada ya kifo cha Mangi Sina mwaka 1897). Hata hivyo urafiki huu haukudumu muda mrefu sana na usingeweza kurejesha uchagani kwenye miaka yake ya zamani. Wakoloni wa Kijerumani walikuwa wameshashika hatamu kwa hiyo utawala wa kimila usingekuwa na nguvu tena waliyoiotea ndoto. Shangali alijiuzulu umangi mwaka 1900 na kaka yake aliyeshika nafasi kule Machame hakufahamiana sana na Marealle. Marealle alifariki mwaka 1911 na utawala wa Marangu uliofuata haukuwa maarufu kwa wakoloni na hivyo kupoteza nguvu ya ukaribu aliyokuwa nayo Mangi Marealle. Kibaya zaidi wakoloni wa kijerumani waling'olewa mara baada ya vita kuu ya kwanza na Uingereza ikachukua nafasi yao Tanganyika mwaka 1917.

Inawezekana sera waliyokuja nayo waingereza ndiyo ingeweza kuzaa uhasama kule uchagani. Mwaka ule tu walioingia rasmi Tanganyika, wakaingizwa kwenye zengwe lililopikwa kwa ufundi kule uchagani na hata kuamua kuwakamata watawala wote wa kichaga na kuwapeleka rumande sehemu mbalimbali kwenye mwambao wa Kenya. Hata hivyo yaliyotokea baada ya hapo ndipo wakagundua ule ulikuwa ni ujanja wa kisiasa ambao ulijikita zaidi Machame. Shangali alirudi tena kwenye umangi kule Machame kupitia zengwe hilo. Waingereza wakapiga presha kwamba Shangali asiendelee kutawala wakihisi zengwe. Hata hivyo makubaliano yalifikiwa kwamba ataachia madaraka mmoja wa watoto wake wakubwa atakapokuwa amekua na kuwa tayari kutawala. Hatimaye 1922 Shangali alistaafu rasmi siasa na mtoto wake Abdiel akatawala mahali pake. Kwa kuona Machame imekuwa na mizengwe mingi ya kisiasa, waingereza waliamua kumvuta kwa karibu Mangi Abdiel ili kumdhibiti na hata kudhibiti Machame. Wakamfanya awe ndiyo mwakilishi na msemaji wao kule uchagani, nafasi ambayo baadhi ya wazee hasa kule Vunjo waliona alikuwa nayo Marealle kwa Wajerumani na hivyo mtoto wake aliyekuwa akitawala, yaani, Petro Itosi, aliistahili. Hii ilileta maneno na minong'no mingi huku wakimtuhumu Mangi Abdieli wa Machame kuwa kibaraka wa wakoloni. Maneno hayo yalisababisha mwaka 1930 Waingereza waitishe uchaguzi wa mwakilishi wa wakoloni kwa wazawa atakayekuwa kiongozi wa watawala wote wa kichaga. Ili kufuta minong'ono, waliwapendekeza Mangi Abdiel wa Machame na Mangi kijana wa Marangu, Petro Itosi, wagombee hizo nafasi. Matokeo ya uchaguzi yaliyofanywa kwenye baraza la watawala wa jadi kule uchagani yalionyesha kuwa Petro Itosi alishinda kwa zaidi ya 99% ya kura zote. Kutokana na matokeo hayo kuwa kinyume kabisa na walichokitaka wakoloni, walidai uchaguzi ulivurugika na hivyo matokeo kuwa batili. Sintomfahamu hiyo iliendelea mpaka mwaka 1946 walipoamua kuunda watawala wa majimbo kule uchagani na kuigawa uchagani yote kwenye majimbo matatu tu, yaani Hai (iliyokuwa na asilimia karibu 50 ya uchagani yote) wakampa mtu wao, Abdieli Shangali wa Machame; Vunjo ikawa chini ya Mangi Petro Itosi wa Marangu; na Rombo iliyokuwa chini ya Mangi Selengia Kinabo wa Rombo Mkuu.

Haya matukio ndiyo yanaweza kudhaniwa kusababisha uhasama kuwepo kati ya Machame na Marangu, ambapo walionekana kama wapinzani (rivals) kwenye kinyang'anyiro cha kuwa juu ya watawala wote wa kichaga. Pamoja na kuteua watawala hao wa majimbo, inaonekana wakoloni waliendelea kumfanya (isivyo rasmi) Mangi abdieli Shangali kuwa ndiyo kama mkubwa wa wengine na mwakilishi wa wakoloni kule uchagani. Walimteua kuwa mtanganyika wa kwanza kuwakilisha wazawa kwenye baraza la kutunga sheria na mwaka 1947 alialikwa Uingereza na Mfalme wa Uingereza kupewa nishani ya MBE. Mambo haya yalizidisha chuki na chokochoko zilizidi hasa kutokea Marangu na baadhi ya wapinzani wa siku nyingi wa kisiasa kule Hai ambao hawakumpenda Mangi Abdieli. Kwa kuona Mangi Petro Itosi asingeweza kukabili mikakati hiyo, walimshawishi mtoto wa kaka yake, Thomas Marealle agombee nafasi ya cheo walichokipendekeza cha Mangi mkuu wa uchagani. Hii sokomoko yote ndiyo imekuwa ikionyesha historia ambayo inawezekana imekuja kutafsiriwa kuwa wamachame wamekuwa na uhasama wa kihistoria na wamarangu. Lakini usaili wa wamachame kihistoria unaonyesha hawadhani kama Marangu imekuwa na nguvu ya kihistoria ya kuwa mahasimu wao wa kisiasa (yaani rivals).
 
joka,

Nisaidie kitu, Tunajua Nyerere alikwenda UN kwa tiketi ya TANU kuwatetea watanganyika kudai uhuru. Sasa, huyu Marealle alikwenda UN kudai nini kwa tiketi ya nani na agenda yake ilikuwa kwa maslahi ya kina nani tofauti na wale waliotetewa na JKN? Hapohapo tunaambiwa alikuwa anam-support Nyerere kisha strangely akapiga marufuku mikutano ya TANU mjini Moshi 1959?

Inaonekana hapa Nyerere aliwakilisha Chama ..Wakati Marealle aliwakilisha ..Native authorities ..chiefs au Sasa Mameya .......inaonekana Nyerere akiwa fix Kina Marealle ...ambaye alimuunga mkono lakini baada ya Uhuru Akawapa native leaders ( chiefs ) wengi uongozi Kama Kina Chief Mkwawa ,Cheef fundikira ,kunambi etc kazi ....a kamtosa Marealle ...plus INAJENGWA propaganda inayoendelea kuwatesa watu hadi Leo kuwa Hawakutaka Uhuru ..au walitaka KUJITENGA .......
ni muhimu Sasa Wakati umefika ukweli UWE wazi ili Jamii zingine NAZO zipumue
 
Inaonekana hapa Nyerere aliwakilisha Chama ..Wakati Marealle aliwakilisha ..Native authorities ..chiefs au Sasa Mameya .......inaonekana Nyerere akiwa fix Kina Marealle ...ambaye alimuunga mkono lakini baada ya Uhuru Akawapa native leaders ( chiefs ) wengi uongozi Kama Kina Chief Mkwawa ,Cheef fundikira ,kunambi etc kazi ....a kamtosa Marealle ...plus INAJENGWA propaganda inayoendelea kuwatesa watu hadi Leo kuwa Hawakutaka Uhuru ..au walitaka KUJITENGA .......
ni muhimu Sasa Wakati umefika ukweli UWE wazi ili Jamii zingine NAZO zipumue

Hapa tutajadili mengi sana ila ukweli wazungu walimtaka Merrealle kwa sera zake na ndiyo maana wakampa mafasi ya ukuu wa machifu kwani walijua angekuwa bepari tofauti na sera za Nyerere kwani wazungu walishamjua Nyerere kuwa ni right wing conservatives ila bahati mbaya walishachelewa kwani wakakuta tayari Nyerere ana nguvu kuliko melleale walijiitahid kumpigania Melleale lakini waap kwani Nyerere nae alikuwa mjanja, msomi na tayari alisha jua lengo la Melleale na wazungu wake na ndiyo maana alipopata uhuru tu akampeleka hukohuko(UN) akae nao na yeye(Nyerere) akafanya mission yake hapa nyumbani

Mimi sidha kama kunakitu kipya cha kuandika kuhusu hii historia kwan hata hayo maelezo ya mtoa mada kaanza kana kwamba anaishu nyeti iliyotofauti ambayo hata mallecture hawaijui lakini maelezo yake yenyewe mepesi tu juu ya chuki za machifu wa kichaga

Nothinng is hidden hapa na wala msitumie nguuvu kuuubwa kupambana na ukweli kwani always ukweli ukweli huwa unajipigania.

Mellealeku kumsemea Nyerere ama Nyerere ku recomend speech ya Melleale hai justfy kuwa hawakuwa wahasimu, kwenye politics tunasema thats politics na always if you cant fight him just join him so hatujui who? joined who?.

Thats it
 
Alichosema Kisumo ndicho sahihi!. Mjerumani alikuwa akitumia utawala wa direct rule, Muingereza ndio akaleta indirect rule ya devide and rule!. Wagawanye uwatawale kwa kuanzisha utawala wa uchifu!. Machifu walifanywa wajione wao ndio bora zaidi, na mkuu wa machifu wote Tanzania alikuwa ni Mangi Mkuu, Thomas Marealle!.

Ni ukweli usiopingika watu wa koo hizi za kichifu walipendelewa ikiwemo kupewa nyumba na Malkia kule London!. Hawa walikuwa ni vibaraka wa wazungu!, walinuona mkoloni ni bora zaidi kuliko mtu mweusi!. Mpaka leo, mpaka kesho makabila anajisikia fahari sana kuishi kuzungu, kuvaa kuzungu, kutembea kizungu, kuongea kuzungu na kutokana na kuupenda uzungu, baadhi ya wanawake wa wetu hupenda kujibadili ili wafanane na wazungu, kuvaa mawigi na nywele za bandia za kizungu, kubadili rangi kwa kujichubua wawe kama wazungu, kujikondesha kuwa na shape kama wazungu, masikini dada zetu hawajui, kuwa hata ladha hubadilika na kuwa ya kizungu!.

Mpaka leo mpaka kesho, nazijua baadhi ya familia zenye uwezo, wanawake wao wanakwenda kujifungulia London!.

Nimebahatika kusoma na one of them toka ukoo wa Mangi Mkuu, hawa jamaa ni mayai kweli kweli!. Tulipomaliza tuu form four, mwenzetu huyoo London!. Nilipopata fursa ya kuja Uingereza, nilimtembelea, life ilikuwa safi!, jamaa wana nyumba ya ukoo London ila yeye na mkewe walipanga nyumba nzima jirani!. Maisha ni ya kudeka deka tangu Tanzania hadi London!.

Tangu tulipoachana Bongo hadi tunakutana London ilipita yapata miaka 10!. Tulipafanya tathmini ya pamoja kati ya miaka 10 ya bongo, mimi nina nini, na miaka 10 ya London mwenzangu ana nini!, akatamani kurudi bongo na mimi nikamuunga mkono. Miaka miwili baadae alirudi na familia yake ila its very unfortunatelly maisha ya bongo yalimshinda!, family ilisambaratika for sometimes, ila kutokana na kuona familia bora, family ili take controll, familia ikatengamaa na jamaa akaona bora arudi kuishi London, huko amezoea zaidi na maisha anayaweza kuliko maisha ya huku!.

Back to Mangi Mkuu, aliside na wakoloni kuwa Watanganyika bado hatiko tayari kujitawala mpaka labda baada ya miaka 15-20!. Akapendekeza kwa vile Kilimajaro ilikuwa juu kimaendeleo, watoe uhuru kwa majimbo kwa Kilimanjaro kupewa uhuru wake kwanza, maeneo mengine yakishaendelea nayo ndio yapewa uhuru hadi Tanganyika yote iishe!.

Chief Marealle ali undermine juhudi zozote za Tanganyika kujiwala, Nyerere baada ya kulijua hili, ali team na wale Waswahili masikini wenzake na wale wazee wa Gerezani, tukapata uhuru!. From there alifutilia mbali uchifu, Mangi Mkuu Mareale akamind sana, akahamia London!. Nyerere aliwawasideline baadhi ya makabila kwenye urais!. Never will this country be ruled na rais kutoka baadhi ya makabila!. Laana ya Nyerere itatushukia!.

Poleni!
Merry X-mass
Pasco
Tumkumbuke Nyerere.
Pasco
 
Tuhuma nyingine, iliyowahi kutolewa na watu wangine, ni kwamba ktk hotuba yake ya June 17,1958 UN Chifu alisema anataka Kilimanjaro ijitenge na nchi ya Tanganyika, huu ni uongu mtupu!

UKWELI HUU HAPA:
Alichoeleza Chifu UN jinsi kwamba yeye na Machifu wengine wa Kanda ya Kaskazini walivyoanzisha chama chao ( Northern Province Chief's Convention) 1956 na jinsi machifu wote Tanganyika walivyoanzisha Chama chao (Territorial Chief's Convention 1957)

Chief alisema madhumuni ya kuanzisha vyama hivyo ilikuwa ni kuwafanya machifu wakutane, washirikiane na watatue matatizo yanayowakabili kwa pamoja. Alise sasa machifu wanaweza kuongea kwa sauti moja katk ngazi ya wilaya, mkoa na nchi nzima. Aliyeanzisha hoja ya kuanzisha vyama hivi (hatua ya kwanza ya kuondoa ukabila nchini alikuwa Chifu Thomas Marealle.
Kama angetaka Kilimanjaro ijitenge asingeanzisha vyama vya kuunganisha machifu wote wa nchi nzima na asingepeleka misaada mingi kwa makabila mengine kama alivyofanya.

Kwa mfano alipeleka misaada kwa Wagogo 1956 wakati wa njaa kubwa Dodoma na aliwahi kupeleka misaada Lindi na Usukuma pia kwa Chifu Majebele.

Kisumo atazamwe upya, pia achunguzwe kwann anasambaza mabaya juu ya Chifu Marealle, lazima kuna conflict of Interest, na wote wanaowasema vibaya wachaga angali kuna mazuri waliyoyafanya katika kuleta usawa kwa Tanganyika yote.
Hakika mkuu shukrani sana.
Paramount chief mariale alikua na wazo zuri sna hapa kuwaunganisha watanganyika wote pamoja pamoja na kusaidia machifu wenzake wa sehemu tajwa.
 
Rejea kusoma post yangu Mkuu...hakuna mahala nimetoa tuhuma za kuwalaumu watu wa kanda nyingine na kuwafananisha na madafu kama unavyotaka kuwaaminisha wewe... instead nimekemea propaganda za kijinga za CCM zinazoendekeza ukabila na ukanda wakati kaskazini kuna watu wazuri tu wanaoweza kuisaidia nchi hii ikapiga maendeleo ya haraka...kwani wewe ni zao la walioshindwa kuuzwa hata kwa dinari moja enzi za biashara zile za kuuza watu? pole ndugu...
Kuna shida mahali kichwani mwako
 
Alichosema Kisumo ndicho sahihi!. Mjerumani alikuwa akitumia utawala wa direct rule, Muingereza ndio akaleta indirect rule ya devide and rule!. Wagawanye uwatawale kwa kuanzisha utawala wa uchifu!. Machifu walifanywa wajione wao ndio bora zaidi, na mkuu wa machifu wote Tanzania alikuwa ni Mangi Mkuu, Thomas Marealle!.

Ni ukweli usiopingika watu wa koo hizi za kichifu walipendelewa ikiwemo kupewa nyumba na Malkia kule London!. Hawa walikuwa ni vibaraka wa wazungu!, walinuona mkoloni ni bora zaidi kuliko mtu mweusi!. Mpaka leo, mpaka kesho makabila anajisikia fahari sana kuishi kuzungu, kuvaa kuzungu, kutembea kizungu, kuongea kuzungu na kutokana na kuupenda uzungu, baadhi ya wanawake wa wetu hupenda kujibadili ili wafanane na wazungu, kuvaa mawigi na nywele za bandia za kizungu, kubadili rangi kwa kujichubua wawe kama wazungu, kujikondesha kuwa na shape kama wazungu, masikini dada zetu hawajui, kuwa hata ladha hubadilika na kuwa ya kizungu!.

Mpaka leo mpaka kesho, nazijua baadhi ya familia zenye uwezo, wanawake wao wanakwenda kujifungulia London!.

Nimebahatika kusoma na one of them toka ukoo wa Mangi Mkuu, hawa jamaa ni mayai kweli kweli!. Tulipomaliza tuu form four, mwenzetu huyoo London!. Nilipopata fursa ya kuja Uingereza, nilimtembelea, life ilikuwa safi!, jamaa wana nyumba ya ukoo London ila yeye na mkewe walipanga nyumba nzima jirani!. Maisha ni ya kudeka deka tangu Tanzania hadi London!.

Tangu tulipoachana Bongo hadi tunakutana London ilipita yapata miaka 10!. Tulipafanya tathmini ya pamoja kati ya miaka 10 ya bongo, mimi nina nini, na miaka 10 ya London mwenzangu ana nini!, akatamani kurudi bongo na mimi nikamuunga mkono. Miaka miwili baadae alirudi na familia yake ila its very unfortunatelly maisha ya bongo yalimshinda!, family ilisambaratika for sometimes, ila kutokana na kuona familia bora, family ili take controll, familia ikatengamaa na jamaa akaona bora arudi kuishi London, huko amezoea zaidi na maisha anayaweza kuliko maisha ya huku!.

Back to Mangi Mkuu, aliside na wakoloni kuwa Watanganyika bado hatiko tayari kujitawala mpaka labda baada ya miaka 15-20!. Akapendekeza kwa vile Kilimajaro ilikuwa juu kimaendeleo, watoe uhuru kwa majimbo kwa Kilimanjaro kupewa uhuru wake kwanza, maeneo mengine yakishaendelea nayo ndio yapewa uhuru hadi Tanganyika yote iishe!.

Chief Marealle ali undermine juhudi zozote za Tanganyika kujiwala, Nyerere baada ya kulijua hili, ali team na wale Waswahili masikini wenzake na wale wazee wa Gerezani, tukapata uhuru!. From there alifutilia mbali uchifu, Mangi Mkuu Mareale akamind sana, akahamia London!. Nyerere aliwawasideline baadhi ya makabila kwenye urais!. Never will this country be ruled na rais kutoka baadhi ya makabila!. Laana ya Nyerere itatushukia!.

Poleni!
Merry X-mass
Pasco
Asante
 
Hapa tutajadili mengi sana ila ukweli wazungu walimtaka Merrealle kwa sera zake na ndiyo maana wakampa mafasi ya ukuu wa machifu kwani walijua angekuwa bepari tofauti na sera za Nyerere kwani wazungu walishamjua Nyerere kuwa ni right wing conservatives ila bahati mbaya walishachelewa kwani wakakuta tayari Nyerere ana nguvu kuliko melleale walijiitahid kumpigania Melleale lakini waap kwani Nyerere nae alikuwa mjanja, msomi na tayari alisha jua lengo la Melleale na wazungu wake na ndiyo maana alipopata uhuru tu akampeleka hukohuko(UN) akae nao na yeye(Nyerere) akafanya mission yake hapa nyumbani

Mimi sidha kama kunakitu kipya cha kuandika kuhusu hii historia kwan hata hayo maelezo ya mtoa mada kaanza kana kwamba anaishu nyeti iliyotofauti ambayo hata mallecture hawaijui lakini maelezo yake yenyewe mepesi tu juu ya chuki za machifu wa kichaga

Nothinng is hidden hapa na wala msitumie nguuvu kuuubwa kupambana na ukweli kwani always ukweli ukweli huwa unajipigania.

Mellealeku kumsemea Nyerere ama Nyerere ku recomend speech ya Melleale hai justfy kuwa hawakuwa wahasimu, kwenye politics tunasema thats politics na always if you cant fight him just join him so hatujui who? joined who?.

Thats it
Waingereza mwanzoni waliwa avoid walutheri weusi kwa sababu ya uhasama wao na Wajerumani during WW I. Walijaribu kueneza uprotestanti wa kwao Tanganyika (uanglikana kwanza na pili u presbyterian). Sometimes kidogo wali import watu hao kutoka makoloni jirani na Tanganyika. Baadae wakaona wa shirikiane na walutheri weusi baada ya kuanza kuwa na mahusiano mazuri kidogo na wajerumani. Vile vile walijenga ushirikiano huu kama njia ya kudhibiti ukatoliki ambao ulikuwa una anza kuwa na nguvu Tanganyika. Lakini walikua wamechelewa kidogo.

Nyerere alikuwa mjanja, lakini pia alisaidiwa na kushauriwa na ma Jesuit.

Na hisi vile vile machifu wa kiprotestanti huenda pia walikua na ukaribu na freemasons wa kiingereza. Nyerere huenda alikuwa ana juana na hao freemasons lakini alikuwa mtiifu zaidi kwa ma Jesuits.
 
Ukiwa na chick vision bila kujaribu kuwaza mbali utasema marealle alikuwa against JK kudai uhuru.

Marealle alikuwa anataka nchi iwe stable kwanza ndio tupewe uhuru. Miundombini kama mashule na hospitali watanzania wajielewe na kuthamini uhuru. Sasa alisems atleast nchi nzima ukiendelea kama KLM by then ndio tupewe uhuru. Wakafanya jumping conclusion na kusema mangi alijuwa anataka uhuru wa KLM pekee.

Wakaanza propaganda na kuwalisha watu huo uongo.bado sijajua dhumun hasa la kutengeneza uzandiki huo. No wonder kuna watu wana hate wachaga vibaya.ndio impact yake hiyo.

Tukimsema marealle kwenye hizo harakati vibaya je nafasi yA JOSEPH KYILIRO itakuwa wapi
Kidogo Kama naelewa nia ya marealle.sababu tangu tupate uhuru bado tupo palepale

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom