Msikilize Lusinde akiuza sera za CHAMA CHA MAPINDUZI

Msikilize Lusinde akiuza sera za CHAMA CHA MAPINDUZI

Ni heri nikae choo cha kiswahili hata siku nzima kuliko kusikiliza utumbo wa Lusinde. Aiseeee, kumbe ndiyo ndiyo maana ccm walishindwa uchaguzi. Hivi waliokuw wanashangilia hotuba ni wameruuuuuu au ni wanamuziki w TOT?
 
Yaani inasikitisha kuna watanzania walikaa wakimshangilia hadi akamaliza.
Hii ni aibu.
 
kifaa cha ccm hicho, tena mjumbe wa halmashauri kuu!
sisi cuf na cdm tunamshukuru ametuongezea credt
 
huyu jamaa ashtakiwe!! amedhalilisha wanawake!!kwani mimba dhambi..eti wanunulie maembe mabovu, duh!!
 
WALIOKUWA WANASHANGILIA LAZIMA WATAKUWA WANAMUZIKI HAO tu...
Ni heri nikae choo cha kiswahili hata siku nzima kuliko kusikiliza utumbo wa Lusinde. Aiseeee, kumbe ndiyo ndiyo maana ccm walishindwa uchaguzi. Hivi waliokuw wanashangilia hotuba ni wameruuuuuu au ni wanamuziki w TOT?
 
hahahaahah Nimecheka kuisikia hii hotuba ya Mzee Lusinde Kudadeki kweli hii kali hata haijazimuliwa hata kidogo kama ni pombe itakuwa ni Gongo wacha weee.............. Luuuuuuuuuuusiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii ndeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Yesu na maria. Hayo ndio maneno ya kampeni ya kuomba kura? Duu yanatia aibu. Nilidhani nasoma matusi ya wale wa uwanja wa fisi manzese siamini yametoka kwenye kinywa cha mheshimiwa mbunge! Hakuna sera wala ahadi ni matusi tu hapo.
 
Yesu na maria. Hayo ndio maneno ya kampeni ya kuomba kura? Duu yanatia aibu. Nilidhani nasoma matusi ya wale wa uwanja wa fisi manzese siamini yametoka kwenye kinywa cha mheshimiwa mbunge! Hakuna sera wala ahadi ni matusi tu hapo.
 
Nimesikitishwa sana na speech ya Matusi ya Lusinde maana dhamira yangu inakataa hata kumwita Mheshimiwa!!!!!!!!!!
Alipokuwa anagombea ubunge mtera nilijua watanzania tumepata kifaa tumaini letu jipya. Kijana smart, msomi na very challenging, lakini sikujua kuwa Lusinde hafai hafai hafai hafai namna hii?!!!!! Usomi na uheshimiwa wote akaweka kando akaanza kubwabwaja matusi kama vile mbele yake hakukuwa na watoto na watu wanaomzidi umri!!!! Heshima gani hii tujifunze kwa chama kikongwe kama ccm!!! Naanza kuamini sasa kuwa ukimuona mtu mzima analia ujue mambo ni magumu. Chadema kinawakosesha usingizi ccm. Lakini kosa si la chadema bali ni la ccm wenyewe. Waungwana waliwaambia kuwa chama ili kirudi kwenye mstari kinahitajika kufanyiwa overhauling. Lakini asiyesikia la mkuu................ cha ajabu hasira zote chadema. Jirekebisheni tu hata bila kuwataja chadema wananchi watakiamini chama. Mzee Butiku kaongea na wengine wameongea lakini hamuwasikii kuwa ccm kinaelekea kufa. Bila kujitakasa na dhambi ya miaka mingi hamtatoka wananchi wameshaamka. Poleni kwa kutukana.

USHAURI KWA CHADEMA:
1. Mfungulieni mashtaka Lusinde maana ushahidi upo tena very valid.
2. Acheni ccm watukane nyie elezeni mapungufu yao kama ufisadi, ubabe, kulindana, ahadi nyingi zisizotekelezeka nk.
3. Anzisheni vyombo vya habari kama TV ili kuwafikia wananchi wengi. Propaganda dhidi yenu ni kubwa
4. Vijijini mwamko bado si mkubwa sana. na huko ndo mtaji wa ccm. wale wakiamka ccm hawawezi kutoka.

Kazi njema
 
kwa kweli ndugu yangu hii uliyosema ni kweli kabisa..! unajua sio kwamba viongozi hawajui matusi..! sio kwamba viongozi hawafahamu lugha mbaya..! lakini kama kiongozi tena ambaye ameaminiwa na wananchi kupewa jukumu kubwa la kuwa wakilisha tena sio sehemu ya muhimu kama bungeni..! hata mkiwa watu watatu tuu..! na ukachaguliwa kiongozi..! inabidi uwe na uchaguzi wa neno lipi uliongee wapi..! laa sivyo wewe unakua hufai kuwa kiongozi..! hata watu walio kua wanatetea haki za watu huko zamani kwenye historia mfano Martin Luther king jr. ambao walikua na reason kabisa ya kutoa maneno machafu..! sio kwamba walikua hawajui maneno machafu ya kutumia..! lakini kwa sababu walikua viongozi wanao jua nini maana ya kua viongozi..! walijua ni maneno yapi ya kuyatumia na wakati gani..!

picha aliyo ionyesha huyu kiongozi..! kwa kweli hata mimi ninasita sana kumuita kiongozi..! maana hata ukiangalia hii clip mwishoni kuna watoto wa shule ya msingi nadhani kama sikosei wanaonekana wanashika midomo kushangaa kwamba "hivi huyu ni mtu mzima kweli..!? ukiambia analingana na baba angu..!? na hivi ni kweli ninayasikia haya kutoka kwa mtu kama huyu..?" yani tuna kipa kizazi kijacho mfano ambao ni utata mtupu..! mtoto kama yule anapata shida kujua afanye nini..!? nyumbani mzee anamwambia matusi ni dhambi halafu akija anakutana na mtu wa heshima anatoa matusi halafu akirudi nyumbani unategemea atajisikiaje akimkuta baba yake anamshabikia lusinde..? si atapata utata mkubwa sana....?

jamani uongozi sio huu..! mimi siandiki haya kushabikia chama chochote ila nadhani hata wale watoto wameona kua hiki sio chama..! sasa kama mtoto anaweza kun'gamua suala kama hili hivi mtu mzima unaposhindwa wewe si ni kama kichaa tu..!? kwa sababu ninaamini kua vichaa wanauelewa uliopo chini kidogo ukilinganisha na watoto..! jamani mimi nadhani huyu hafai kua kiongozi hata wa familia yake..! sisemi hivi kumdhalilisha ila unadhani watoto wake wanajifunza nini hapa kutoka kwa baba yao (kama ameoa)..?

nilimsikiliza juzi wakati anahojiwa clouds.. kitu alichosema mwisho baada ya kuulizwa na kibonde kua "kama mwerevu... kichaa akikuvua nguo na kukimbia nazo utamfukuza au utakaa..?" lusinde alijibu kua "utakaa"

jibu hili lilimfunga mwenyewe na kumuonesha kwamba sio muerevu hata kidogo kwasababu alisema kua aliyaongea yale maneno ili kuwajibu chadema ambao walikua wanawatukana... sasa kama chadema wamekutukana wewe kama mwerevu unawatukana pia au utakaa..! yeye aliwatukana pia so hapo hajaonesha uerevu wowote na yeye amekua kichaa.. hata hivyo ni kama tu chadema nao walitoa maneno machafu kama aliyo yatoa

inasikitisha sana...!
 
Kweli CCM mna sera nzuri, lakini hazina tija kwa Mtanzania wa leo wala yule wa kesho
Hotuba ya Livingstone Lusinde Katika Maandishi Kutoka Wavuti


Mh mwenyekiti wa chama, waheshimiwa viongozi wenzangu na wanachama wenzangu, nataka nianze kutofautiana hapahapa jukwaani na wenzangu, habari ya sisi kutukanwa halafu tunasema sisi hatutukani hatufanyi kazi ya kanisa hapa, kudadadeeekimatusi yakija nitatukana hoja zikija nitasema, potelea mbali

CCM oyeeeee.......oyeeee!

Niseme nisiseme.....semaaaaaa!

Unajua kuna wabunge wa chadema maji marefu unawalea sana, wewe ndio uliowachanja chale mpaka matakoni leo wanakutukana, nataka niwaambieni wenzetu wanajifanya wanajua kutukana hapa mwisho! ndio maana nimekuja kuwapasha kwamba hoja nyingine za kipuuzi wanazozisema chadema wanajitukana mpaka wao wenyewe, kuja kusema hapa kwamba mgombea wa ccm katoboa sikio kwa hiyo ni shoga maana yake na baba yake slaa nae ni shoga maana nae katoboa sikio kudadadeeeki CCM oyeeee....oyeeeee


Nataka niwaambie ndugu zangu msindanywe, msidanganywe na rangi utamu wa chai sukari, wale waliojazana katika chadema wote karibu nusu baba zao wametoboa masikio kwa hiyo na wao mashoga? Niwaambie nisiwaambie. . . .waambie! mbunge wa arusha mjini juzi alikua mahabusu na si tunajua kule mahabusu alifanywa nini, lakini hatutaki kusema

tuwalambe tusiwalambe.....walambeee!

Ndungu zangu nataka niwaambieni kwa habari ya lugha chafu wote sisi tunazo wala msifikiri hatujui sisi hatuna, tunajua Lema alikua mahabusu amepata bwana kule tunajua, na kuna wanaume wengine wameolewa sisi tunawafahamu, nataka kuwasihi sana, kwenye uchaguzi, kwenye uchaguzi tunajenga hoja za msingi lakini wakileta maneno ya honyo na hapa yapo, kudadadeeeki

nataka niwasihi sana, hakuna mtu asiye na makosa duniani, leo dr slaa anapita kuwasema wenzake wakati yeye upadri ulimshinda kanisa likamfukuza kwa kutia mimba wanakwaya

Sioi oyeeee! Oyeeee!

Mi nawafahamu wale, unajua tukiendelea kuwachekea hivi tukiendelea kuwambeleza hivi itafika mahali watatuchokoa machoni bora tule nao sahani moja, kuna
*****
mwingine yuko mle, kuna ***** mwingine yuko mle anajiita campain manager wa chadema, ukoo wa nyerere, baba yake mzazi wa nyerere akiitwa buhito alikua akitoboa masikio, alikua shoga? anajitukana mpaka mwenyewe kwa sababu ya akili mbovu, kutoboa masikio sio ushoga, masai wanatoboa, wagogo wanatoboa, wameru zamani walikua wanatoboa, wa-wakurya wanatoboa, wakamba wanatoboa, ye hajui historia anakuja hapa (huku kabana pua) ng'wee ng'wee ng'weeee, mbona ye ameliwa si hatusemi

ccm oyeee, oyeeeee
wanaokipenda chama mikono juuu!

(sauti ya kike kwa mbaali inasikika - wamekwisha!)

subiri niwaambie, hoja zinazojengwa hapa ni hoja za kipumbavu, kuna watu wanakuja kujenga hoja ya kitoto, kwamba msimchague sioi kwa sababu alizaliwa kenya, sio raia wa tanzania, mtu akizaliwa kwenye ndege anakua raia wa nchi gani? Acheni ushamba nyie, Suala la mtu kuzaliwa na suala na uraia ni vitu viwili tofauti, uchungu unapompata mwanamke anazalia hapohapo hawezi kusubiri, kuna wengine wamezaliwa kwenye mabasi mbona hatuwaiti raia wa basi, washamba wakubwa nyie, hiyo mnaona ni hoja ya kupita mnazungumza, halafu nyingine wanapita wamebana pua, msimchague sioi kwa sababu baba yake alikua mbunge, baba yake atarudi lini? Baba yake anarudi?

Ngojeni niwaeleze, na bahati nzuri najua walipo ntakua napiga hapa afu napiga palepale, kudadadeeeki . . .

CCM oyeee .....oyeeeee!
Msikubali kudanganywa ndugu zangu maswala ya mtoto kufata kazi ya baba yake, katika tanzania ni kitu cha kawaida, tunao wanajeshi na watoto zao wanajeshi uongo kweli?....kweliiiiii! tunao madereva na watoto wao madereva uongo kweli?.....kweliiii, tunao wapiga debe na watoto zao wapiga debe uongo kweli . . . kweliiii! kuna ajabu gani kwa sioi piga makofi kwake.

Niwaulize nisiwaulize.....ulizaaaaaaa! Marehemu sumari angekua daktari na mtoto wake daktari CHADEMA wangegoma kunywa dawa (sauti ya kimbea kwa mbali inajibu . . . . wathubutu!), washamba nyie!

ccm oyee. . . oyeeee! Niwalambe nisiwalambe. . . . walambeee!

Ndio maana tunataka tuwaambie chama cha mapinduzi ndiyo chenye makamanda wa ukweli sio nyie makamanda feki, Jakaya Kikwete mwenyekiti wa ccm kazi yake zamani alikua mwanajeshi uongo kweli?..... kweliiii, kapteni komba alikua mwanajeshi uongo kweli? .......kweliiii! lakini wanavaa nguo za kijani halafu washamba ambao hata mgambo hawajapita wanavaa makombati.

ccm oyeee.....oyeeee!


Halafu katika washamba hakuna mshamba kama dokta slaa, anavaa kombati kuuubwa akitembea kama kajinyea vile (anapata shangwe kutoka kwa wanaomsikiliza, sorry to say this hapa hata mke wangu alicheka, nikamtazama kwa hasira hadi akaogopa!)

Nipige Nisipigeee?.........Pigaaaaaaa aaaaa
Bendera ya CCM ina rangi ganiiiiiiiiiiiiii?............ .......Kijaniiiiiiiiiiiiii.
Ukipanda mahindi yanaota na rangi ganiiiiiiiiiiiii?............K ijaniiiiiiiiiiiiii.
Ukipanda mpunga unaota na rangi ganiiiiiiiiiiiiii?............ .Kijaniiiiiiiiiiiiiiii
Migomba yote ina rangi ganiiiiiiiiiii?............... ............Kijaniiiiiiiii.
Piga makofi na vigelegele kwa chama cha mapinduzi.

Nataka niwaambie kama CHADEMA, kama viongozi wa CHADEMA ni vichaa wa kurogwa, mie ni kichaa wa kuzaliwa, kudadadeeeki!tarehe moja, dk slaa juzi, (anaguna) yaani katika watu washamba nimewashangaa dk slaa, anakakaa kwenye tv anasema eti ''ooooh hapa isipochaguliwa chadema patachimbika'' kama ni fujo itaanzia arumeru, kwa nini isingeanzia kwa mke wake? Ngoja niwaambie ndugu zangu, alichokua anakisema slaa, alichokua anatutishia vita slaa mimi namwambia anatishia kujamba wakati anaharisha.

ccm oyeee....oyeeee!. wangapi mtampa kura kura sioi, mikono juu....(watu wananyanyua mikono), hatufanyi kazi ya kanisa hapa! hapa tumekuja kuwaambia kwa suala la kutishana hakuna mtu anayeogopa, wote si tumeaga na nataka niwaambie slaa yule anavimba macho ya watu, lakini kama slaa ana ubavu nipeni mi tuweke ulingo hapa, ngumi moja naua yule, nikikusanya yule nipige mkono mmoja mnakuja kuokota yule, akiona watu wamejaa (anabana pua) ng'weng'weng'wee ng'weng'weng'wee upadri umemshinda ataweza serikali? thubutuu!

Nataka niwaambie, ndugu zangu wa arumeru, suala la uchaguzi mdogo sio suala la kudanganywa, wanakuja CDM hapa wanakudanganyeni, kwamba watapora mashamba ya wazungu wawagawieni, muasisi wa chama cha CDM ndugu mtei ana shamba hapa heka 700 mbona hawampori wawagawie? wangeanza kwanza la mtei, sio kuwadanganya wananchi, kama wanawapenda kweli wa meru wamwambie mzee mtei chukua shamba lako rudisha kwa watu wa meru(sauti ile ya kike. . . hatudanganyiki)

ccm oyeee.....oyeeee!
Niwachane nisiwachane?......wachaneee!

Vijana wenzangu, CDM inawapa pesa za kunywa viroba, mnalewa viroba na bangi mnazomea wazee wenu, halafu wenzenu wanapita na helikopta wanawaona machizi

niseme nisiseme.....semaaa!

Kokote duniani askari wanaoteka nchi ni askari wa miguu wacha wao waruke juu si tunateka nchi, wao wanaruka na helicopter si tunachukua jimbo asubuhi, kudadadeeki, mnakuja mnadanganywa hapa eti ooh chadema, sijui ooh nasari ataleta ajira na soko, ajira atazitoa wapi? Watu hawana shukrani anasimama hapa dk slaa anatukana ccm, hawajafanya kitu, hawajafanya kitu, shule alizosoma yeye zimejengwa na baba yake? shule zimejengwa na serikali ya chama cha mapinduzi, watu wanajiita wamesoma chuo kikuu (chuo hicho) kimejengwa na serikali ya chama cha mapinduzi, nionesheni hapa chuo walichojenga CDM. . . hakunaaa!

ccm oyeee....oyeeee!

Wanatuletea sera ya jogoo, nataka mkatae sera ya CDM ni sera ya jogoo, Jogoo katika makuku maongo hakuna kama jogoo, Jogoo linapokua linamtaka kuku mwenzake linadanganya linamwambia nitakushonea gauni reeefu mpaka huku (anainama huku akizunguka kuonyesha mfano wa jogoo, watu wanalipuka kwa kicheko)

Niseme nisiseme. . . .semaaaa!

Kataeni uongo wa jogoo, linaahidi kushona gauni refu wakati lenyewe likiinama hata chupi halina, waongo wakubwa tunawajua, na hivyo viroba mnavyokunywa vijana, viroba mnavyokunywa vijana mwisho tarehe moja, wataondoka watakuacheni mmetukana wazee wenu, mmewapiga mawe wazee wenu, na mimi nataka niwaambie vijana wa CDM utaonekana kichaa ukionekana unazomea rangi ya kijani maana utakuta mti una rangi gani....kijani! unaanza uhuuuu watu wanasema huyu chizi, mchezaji aliyeumia ni mchezaji wa timu ya ccm tunaweka mchezaji wa ccm, suruali yangu nyeusi imetoboka siwezi kuweka kiraka cheupe kama nina akili nzuri, inabidi niweke cha rangi gani? Kijaniii! Hata hilo mnataka mtu atoke dodoma kuja kuwaambia? Kama huoni kwa macho papasa kwa mkono utapa majibu.

Ccm oyeeeee.....oyeeeee!


Niwaambie nisiwaambie hawa.....waambie!...ngoja niwaambie watu wa CDM nyie

nikakutana na kijana mmoja akanichekesha sana, ananiambia mwanaume mzima, basi kati ya watu ambao hawajui kiswahili mbowe hajui kiswahili, mbowe anasimama anasema nina uchungu mkubwa, bibilia inasema hivi wanawake mtazaa kwa uchungu, wanaume watakula kwa jasho uongo kweli...kweliiii! kama mbowe anauchungu ana mimba?....vicheko

ccm oyeeee.....oyeeee!

Nataka niwaambie, kipindi hiki ni kipindi cha lala salama, ukiona mtu anasikia kichefufu, ukiona mtu anatema mate, ukimuona mtu anaichukia ccm ujue tayari tumeshamtia mimba, ndio maana unawaona saa hizi wanapiga kelele, unaona kina slaa wanapiga kilele, wameshapigwa mimba, mbowe pigwa mimba, nasari pigwa mimba....mayoweee

Tarehe moja wanaenda kujifungua mtoto anaitwa sioi, piga makofii. Kichefuchefu chote kitawaisha utawaona ooh tulikua pamoja tulikua pamoja kudadadeeki.

Niwachane nisiwachane?.....wachane!

we ukiona unapita mwanaccm humsemeshi mtu anakufanyia hivi (anaonesha V, ishara ya CDM) ujue ana mimba ya mapacha, mnunulie udongo, mnunulie maembe mabovu, mnunulie vitu vya uchachu tarehe moja anajifungua sioi anakwenda bungeni na wao mimba wanazaa hapohapo.

Tuwapime wenye mimba tusiwapime....tuwapimeeee
Tuwapime wenye mimba tusiwapime....tuwapimeeee

nitakuuliza swali, nitakuuliza swali, atakaempigia kura sioi anyoshe mkono kama hakunyosha jua ana mimba

ccm oyeeee....oyeeee!


Source: "Kudadadeki, matusi yakija nitatukana, hoja zikija nitasema..." - L. Lusinde - wavuti.com*
 
Kweli CCM mna sera nzuri, lakini hazina tija kwa Mtanzania wa leo wala yule wa kesho

Umeona eeeh! sijui Rejao,ritz,mafilili huwa wakisoma hii wanajiskiaje?
 
Huu ndio ujumbe muruwa kwa ccm

"The hand writing on the wall" (or "the handwriting on the wall" or "the writing is on the wall" or "Mene Mene"), an idiom, is a portent of doom or misfortune. It originates from the Biblical book of Daniel chapter 5 in which the fingers of a supernatural hand write a mysterious message in the presence ofBelshazzar, king of Babylon, who is meanwhile drinking at a major feast. It is revealed by Daniel that the writing foretells the demise of the Babylonian Empire and the story concludes with the Persians capturing Babylon. The phrase "the writing is on the wall" is now a popular idiom for "something bad is about to happen.
 
CCM wanajivunia na wanamwita LUSINDE kuwa ni JEMBE la CCM.
 
Back
Top Bottom