Mshukiwa wa ubakaji ajinyonga India

Mshukiwa wa ubakaji ajinyonga India

mwekundu

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2013
Posts
22,477
Reaction score
21,039
Mshukiwa wa ubakaji ajinyonga India
Mshukiwa katika kesi ya ubakaji wa msichana mmoja wa chuo kikuu ambaye baadaye alifariki nchini India, amepatikana amefariki gerezani. Haya yamethibitishwa na wakili wake.

Polisi wanasema kuwa Ram Singh, alijinyonga akiwa ndani ya gereza la Tihar mjini Delhi's Tihar, lakini mawakili wa utetezi wanadai kuwa huenda alinyongwa.
Taarifa zinazohusiana

afya

Ram Singh, aliyekua na umri wa miaka 33, alikuwa mmoja wa washukiwa katika kesi ya ubakaji wanaozuiliwa na polisi kwa madai ya mauaji ya msichana waliyembaka.

Wote walikanusha madai hayo.

Shambulizi dhidi ya mwanafunzi huo, lililofanyika Disemba mwaka jana, lilizua mjadala mkali nchini India kuhusu wanawake wanavyodhulumiwa.

Jela la Tahir ambako washukiwa wa ubakaji wanazuiliwa

Kesi ya mshukiwa wa sita inaendeshwa katika mahakama ya watoto.

Mwandishi wa BBC Sanjoy Majumder,mjini Delhi,anasema kuwa kifo cha bwana Singh kinakuja kama aibu kubwa kwa maafisa ambao wanakabiliwa na shinikizo kubwa kuhusu kesi hiyo.

Msemaji wa jela hiyo Sunil Gupta, aliambia BBC kuwa Ram Singh alijinyonga kwa banketi usiku wa kuamkia leo.
SoURCE ;BBC
 
India unyanyasaji wa wanawake ni too much! Huyu bwana kakwepa kesi kiaina!
 
Police said the suspect hanged himself around 5am this morning in his prison cell...but his lawyer and parents are claiming he was murdered.
"Ram did not kill himself. He had no reason to. He was murdered," his fathersaid.
"This is not a suicide. He was kept in isolation, with at least four special guards posted outside his cell. We suspect foul play" his lawyer said
33 year old Ram Singh was the driver of the New Delhi bus on which a 23 year old student was gang raped and fatally beaten on December 16 2012. The woman later died from injuries sustained from the attack. Six suspects were arrested and if convicted, could face the death penalty. (Read the original story HERE)
 
Back
Top Bottom