Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 137,544
- 272,272
kiasi cha mshahara kwa rais yeyote duniani hutegemea na malengo halisi ya mgombea yaliyomsukuma kuomba kazi hiyo ! KWA MTU MWAMINIFU KABISA , IKULU NI MZIGO - JK NYERERE .
Huyo Mama ni mburula tu,hata hako kaelimu alikopata hakajamsaidia kitu.,Eti anamwuliza mwandishi 'wewe unaujua mshahara wa Obama?'Sijui hicho kiti amekikalia kwa vigezo gani.
Ndio Mamburula wetu hawa ndani ya Serikali inayothubutu kujiita eti, "Serikali sikivu" sijui huo usikivu ni kwenye lipi hasa.
Siwezi kutaja mshahara wa bosi wangu wala wa kwangu mwenyewe. Wewe unaujua mshahara wa Obama (Rais wa Marekani)? alihoji tena.
Huyo mama eti ndo alikuwa waziri wa sheria na katiba. Naye kwani ni dada msomi aka 'learned sister'? Teh teh teh....kaazi kweli kweli.
Eti 'wewe unaujua mshahara wa Obama'? Haya bana dada msomi. Nilishagachoka mie kuulizia huu mshahara wa rais maana mijitu ni mijinga kupita kiasi.
Kwa utaratibu huu,ccm ikiondoka madarakani kwa hiyari itakuwa ni muujiza wa karne!watu mnashangaa mishahara hawa jamaa hata nyama wanapewa bure nenda pale clock tower kwenye duka la nyama la kongwa..... ndio maana ile ranchi ya taifa haijiendeshi kifaid ni gari za STK tu zinapanga foleni pale kubeba nyama za mawaziri na wakubwa wengine.... yaan tumefika huku v8 zinabeba nyama kupeleka majumban mwa viongozi kwa mishahara hii hadi nyama nayo wanapewa bure tena kama siku za sikukuu mtanzania unayetaka kununua kwa cash pale hupati nyama ni oda za ofisi za serikali tu tena hawalipi!!!
Huo ni mshahara tu,Nahisi posho zao zikiwekwa hadharani hatutaamini
Ni mara tatu zaidi ya mshahara.