Mshahara wa Rais kaa la moto

Mshahara wa Rais kaa la moto

Rafiki KOKUTONA ndio maana hawataki Watanzania tuijue mishahara yao. Muajiri wao ni Watanzania halafu mishahara wanajipangia waajiriwa tena kwa siri halafu hawataki muajiri wao ajue mishahara waliyojipangia!!!! Wakati huo huo hawataki kuongeza mishahara ya Walimu na Madaktari kwa kisingizio Serikali haina pesa!!! Ila pesa ya kujilipa wenyewe mishahara minene siku zote haikosekani!!! Eti ni kosa kutangaza mshahara wa wanene hadharani!!! Walifungie tena Mwananchi kwa kuvunja sharia ya kuanika mishahara ya wanene hadharani.

Wamekosa utu na huruma kabisa kwa wananchi na walipa kodi. Angalia mishahara yao ilivyo mikubwa na wanaipokea bila aibu kabisa il hali haikatwi kodo lakini bado wanamkandamiza mtumishi ambaye hafikii haata theluthi ya mishahara yao kwa kumkata kodi kubwa eti PAYE, wao PAYE wanakatwa wapi?

Bado wameongeza kodi kibao zisizo na kichwa wala miguu...unajua nini BAK wao machungu hawayasikii sbb kila kitu wanapewa tu hawana machungu yoyote ya kutafuta kwa jasho. Lakini ole nakwambia muda wao utafika watakapoinamisha vichwa vyao kwa aibu. Siku Mungu atakapoamua kusimama na kuanika uovu huu hadaharani.

 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
siri ni KIFO tu mshahara kuwa siri huo ni uwizi na ubabaishaji weka kitu hadharani bwana eboo.
 
Asikitike nini wakati yeye ni mwizi wa mbao mufindi? Kelele zoote anazopiga anataka wajue amerudi kuisaidia CCM. Kisha nao wampe tenda.

Siku zao zinahesabika..kabla hawajaiona aibu miguuni mwao

 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mshahara mdogo sana ukizingatia misaafa anayotoa kwa Makundi mbalimbali nyakati zote hass za sikukuu Acheni wivu khaaa
 
Mshahara mdogo sana ukizingatia misaafa anayotoa kwa Makundi mbalimbali nyakati zote hass za sikukuu Acheni wivu khaaa

Misaada ingekuwa inatangazwa na ufanye hesabu ya percent anayotoa katika pato lake nakuhakikishia hata kumi bora hachomozi!!!
Watu wametoa nyumba wanakaa yatima itakuwa mbuzi mchele na.mafuta??????!!!!!!

Aliyekutuma kakuelekeza la 1A wewe umekuja la 7B
 
Kwa level ya tanzania vs china wale wataalamu wa uwiano watupe hiyo ratio kwa kuwa china ipo top tena kutoka juu na bongo ipo top twenty kutoka chini ila mshahara wa kikwete naona magumashi kwa xi ping
 
Hiyo sheria ya kutotangaza mshahara wa watumishi kuwa siri ni namba ngapi na ilitungwa mwaka gani? Kama Magufuli anataja sheria zote za barabara, kwanini na huyo waziri wa Utumishi asituambie ni sheria ya lini badala ya kuogopesha tu watu!
 
32,000,000*12*10=3,840,000,000
Mshahara wa Rais baada ya kumaliza awamu yake ya miaka 10, hakatwi kodi hata senti moja.
 
32,000,000*12*10=3,840,000,000
Mshahara wa Rais baada ya kumaliza awamu yake ya miaka 10, hakatwi kodi hata senti moja.
Mkuu nilitaka nianzishe thread,lakini nadhani tunaweza kujadili hapa.


Nilitaka tu nijuwe vigezo vyetu kwa mishahara ya viongozi wetu.Kwasababu tumeona viongozi wetu wanalipwa zaidi ya viongozi wa nchi tajiri ambazo zinatufadhili kwa kila namna hata bajeti zetu!Haya ni maajbu ya dunia.

Sitaki kuwa negative,ila nataka details zenye kuconvince,ya kwamba kwanini maisha ya viongozi wetu hayareflect maisha ya wananchi wanaowaongoza!

Nchi matajiri ziko makini kuhusu matumizi ya viongozi na yasiyo ya maana ambayo huyaita "pork barrels"

Ninachotaka hapa si malumbano ya kwanini ilitakiwa iwe siri,kama alivyosema mama Kombani ambaye nimeshtushwa na uwezo wake wa kufikiri!

Kwasababu anajuwa kuwa mambo yemekuwa wazi,alichotakiwa kufanya ni kueleza sababu ambazo zitahalalisha ama kujustify mishahara hiyo mikubwa kuliko ya viongozi wa nchi tajiri ambao michango yao mdiyo hiyohiyo inayotumika kuwalipa viongozi wetu akiwemo rais!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Wamekosa utu na huruma kabisa kwa wananchi na walipa kodi. Angalia mishahara yao ilivyo mikubwa na wanaipokea bila aibu kabisa il hali haikatwi kodo lakini bado wanamkandamiza mtumishi ambaye hafikii haata theluthi ya mishahara yao kwa kumkata kodi kubwa eti PAYE, wao PAYE wanakatwa wapi?

Bado wameongeza kodi kibao zisizo na kichwa wala miguu...unajua nini BAK wao machungu hawayasikii sbb kila kitu wanapewa tu hawana machungu yoyote ya kutafuta kwa jasho. Lakini ole nakwambia muda wao utafika watakapoinamisha vichwa vyao kwa aibu. Siku Mungu atakapoamua kusimama na kuanika uovu huu hadaharani.


Viongozi kama hao kamwe hawatataka mabadilko,kwasababu wengi wao kilichowapelekea ndo hicho(siyo kuelimisha,kuwatumikia wananchi na kuwafumbua macho),na wanajuwa wakiwafumbua macho wananchi,basi maslahi yao yatakuwa hayana maana na hawatafanya hivyo,bali kuendelea na shughuli ambazo wana maslahi nazo...Mfano kuhonga kanga na pilao,kuleta machafuko kwa kuhubiri chuki za kidini na kikabila,mauwaji,kweka fedha akaunti za nje,kuhakikisha wananchi hawajui haki zao na pia hawaeleimiki na kufahamu haki za uraia!

Mfano hata hapa JF,hawataki hoja zijadiliwe tena,kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa kwenye hilo kwasababu kuna watu wanajibu upumbavu wao,wanaanzisha thread za kipumbavu na watu wana jibu,nadhani wanaofanya hivyo ni wale wanaotaka kujionyesha kwamba wanauwezo wa kupambana na maadui wa chadema na kutaka kuonyesha udhaifu wa mleta hoja,lakini the best weapon fo a fool is to ignore him.

Sisemi kwamba msijibu kila posti za hao watu,ila kama ni zakijinga kama aliyoitoa,msijibu!hata akianzisha thread ya kijinga,ignore it.!kuijibu ni faida kwake kwasababu hata mkimtukana,yeye anajuwa ni "the truth pain",licha ya kwamba si kweli.Kuwa mwanachadema makini,si kujibu hoja za fools!Ni kuunga mkono hoja zenye akili,kuelimisha,na kurespond kwenye hoja ambazo utaweza kuwaelimisha wananchi kwenye process ya kurespond,ama kusaidia kwenye udadavuaji pale inapotokea kuna mwenye honest question nk.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu haingii akilini kuona Kikwete analipwa mshahara mkubwa ukilinganisha na viongozi wa China, Urusi, India n.k. Hawa viongozi ndio wanakuwa mstari wa mbele pale huduma mbali mbali muhimu nchini zinavyolegalega kwa kudai kwamba nchi yetu ni maskini hivyo Serikali haina uwezo wa kifedha kuhakikisha huduma hizo muhimu zinapatikana katika hali ya kuridhisha kwa Watanzania walio wengi. Inapokuja kwenye mishahara yao umaskini wa Tanzania wanausahau kabisa na hivyo kujipangia mishahara mikubwa tena kwa siri ambayo inawazidi hata viongozi wa nchi tajiri duniani kama China, Urusi na UK.

Wanajua fika kwamba hakuna justification yoyote ya wao kujipangia mishahara mikubwa kiasi hiki tena ikiwa haitozwi kodi na huku gharama zao za kila siku pamoja na familia zao zote zinabebwa na walipa kodi.

Hawana vigezo vyovyote walivyovitumia ambavyo wanaweza kuviweka hadharani ili kuthibitisha kwanini waliamua mshahara wa Kikwete uwe shilingi 32 million na Pinda milioni 26 kwa mwezi badala ya shilingi milioni 5/6 kwa mwezi. Na kwa kuwa hakuna vigezo hivyo ndiyo maana hawataki kabisa hili swala lijadiliwe kwa kina na wanatumia ubabe kutishia hata vyombo vya habari kwamba kuutaja mshahara wa mfanyakazi wa Serikali hadharani ni kosa.

Tatizo pia ni kwamba Viongozi hawa hata siku moja hawawezi kuwapa fursa waandishi wa habari ili wawaulize maswali kama haya, "Je unastahili kupata mshahara wa shilingi 32/26 milioni kwa mwezi huku ukiwa hukatwi kodi wakati Mwalimu anayepata mshahara wa shilingi laki 4 anakatwa kodi?" "Je kungekuwa na tofauti gani katika maisha yako kama mshahara wako ungekuwa ni shilingi milioni 5 kwa mwezi na pesa nyingine kutumika katika kuboresha huduma muhimu nchini kama vile afya, elimu, upatikanaji wa maji safi n.k."



Mkuu nilitaka nianzishe thread,lakini nadhani tunaweza kujadili hapa.


Nilitaka tu nijuwe vigezo vyetu kwa mishahara ya viongozi wetu.Kwasababu tumeona viongozi wetu wanalipwa zaidi ya viongozi wa nchi tajiri ambazo zinatufadhili kwa kila namna hata bajeti zetu.ahsys ni mssjsbu ys dunia.

Sitaki kuwa negative,ila nataka detailas zenye kuconvinve,ya kwamba kwanini maisha ya viongozi wetu hayareflect maisha ya wananchi wanaowaongoza!

Nchi matajiri ziko makini kuhusu matumizi ya viongozi na yasiyo ya maana ambayo huyaita "pork barrels"

Ninachotaka hapa si malumbano ya kwanini ilitakiwa iwe siri,kama alivyosema mama Kombani ambaye nimeshtushwa na uwezo wake wa kufikiri!

Kwasababu amjuwa kuwa mambo yemkuwa wazi,alichotakiwa kufanya ni kueleza sababu ambazo zitahalalisha ama kujustify mishahara hiyo mikubwa kuliko ya viongozi wa nchi tajiri ambao michango yao mdiyo hiyohiyo inayotumika kuwalipa viongozi wetu akiwemo rais!
 
Hiyo sheria ya kutotangaza mshahara wa watumishi kuwa siri ni namba ngapi na ilitungwa mwaka gani? Kama Magufuli anataja sheria zote za barabara, kwanini na huyo waziri wa Utumishi asituambie ni sheria ya lini badala ya kuogopesha tu watu!

Huyo Mama ni mburula tu,hata hako kaelimu alikopata hakajamsaidia kitu.,Eti anamwuliza mwandishi 'wewe unaujua mshahara wa Obama?'Sijui hicho kiti amekikalia kwa vigezo gani.
 
Hawa wanasiasa ndio maana watafanya kila kitu waliwezalo,ili mradi aingie ikulu..mtu anavuta pay ndefu alafu bado anaishi maisha ya zero cost jamani
 
KOKUTONA wabonaki waitu? Ija nikugambile ebigambo.

Btw huyo jamaa mropokaji achana naye ana laana ya kula rambirambi ya mjane wa Mwangosi!

Hivi ile rambirambi aliyokula huyu jamaa hajarudisha mpaka leo ! Eee M/Mungu , mwingi wa rehma uliyewakataa watenda dhulma wote wa enzi zile , tunakuomba umkatae na huyu aliyemdhulumu mjane na wanawe , Amina .
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom