Mshahara wa dhambi ni mauti na majuto ni mjukuu

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,701
218,227
Ni maneno machache lakini yamebeba ujumbe mzito sana !

Hakika kwa yanayoendelea kwenye siasa za nchi yetu tangu uchaguzi mkuu , inahitaji roho ya paka kuyavumilia .

walioshinda wananyang'anywa hivi hivi macho makavu na Mungu ni shahidi ! kilombero waliokuwa wengi wamedhulumiwa , Tanga walioaminiwa na wananchi wameporwa haki yao , Dar es salaam inakaribia nusu mwaka tangu uchaguzi lakini wenye haki wanapigwa danadana , ya Zanzibar sina haja ya kuyarudia.

itoshe tu kusema mshahara wa dhambi ni mauti maana yote haya Mungu anayaona , nimeweka angalizo hili ili tusije kujuta siku za usoni kwa vile ilishasemwa na wahenga kwamba Majuto ni mjukuu .

NAKULILIA TANZANIA .
 
mungu ni wa maskini na mafukara ,,kama umenyimwa haki yako unaitafuta na kuipigania,,hakuna haki inayopatikana mezani,,,mwenye chakula hawezi kukiachia akapewe mwenye njaa,,,wanasemaga hivyo wenye maendeleo yao duniani
nawakilisha
 
Time will tell. kuna kizazi kinakuja, kizazi kinachowaangalia baba na kaka zao wakibet na kucheza pool...
HAKIKA IPO SIKU KITANUKA TU.
 
Mungu aliye hai atulinde sana .
Na msimamizi mkuu wa haki hapa nchini kila siku anaimba eti Muniombee kwa Mungu maana kazi hii ya kutenda haki ni ngumu sana. Mungu anayeomba tumuombee sijui ni huyuhuyu anayejulikana na wengi au huyu ni wake mwenyewe.
 
Ni maneno machache lakini yamebeba ujumbe mzito sana !

Hakika kwa yanayoendelea kwenye siasa za nchi yetu tangu uchaguzi mkuu , inahitaji roho ya paka kuyavumilia .

walioshinda wananyang'anywa hivi hivi macho makavu na Mungu ni shahidi ! kilombero waliokuwa wengi wamedhulumiwa , Tanga walioaminiwa na wananchi wameporwa haki yao , Dar es salaam inakaribia nusu mwaka tangu uchaguzi lakini wenye haki wanapigwa danadana , ya Zanzibar sina haja ya kuyarudia.

itoshe tu kusema mshahara wa dhambi ni mauti maana yote haya Mungu anayaona , nimeweka angalizo hili ili tusije kujuta siku za usoni kwa vile ilishasemwa na wahenga kwamba Majuto ni mjukuu .

NAKULILIA TANZANIA .
Mkuu kaa ukijua kuwa kuna msemo pia inasema hivi...HAKUNA MAREFU YASIYO NA NCHA...
 
Na msimamizi mkuu wa haki hapa nchini kila siku anaimba eti Muniombee kwa Mungu maana kazi hii ya kutenda haki ni ngumu sana. Mungu anayeomba tumuombee sijui ni huyuhuyu anayejulikana na wengi au huyu ni wake mwenyewe.
Ni mungu wa kumuwezesha kuwa na moyo wa chuma,hivyo neno huruma kwake nooooo
 
Kila kitu chochote kizuri unachokiona duniani kimesimama katika misingi ya ukweli na kujitoa (sacrifice) vivyo hivyo mambo yote yanayomsababishia binadamu matatizo na majuto yamesimama katika uongo uliofanywa na binadamu huyo huyo.
Hapa ni kuwa unavyochelewa kuutambua ukweli na kuufuata ndivyo matatizo yatakavyozidi kukuandama na wengine kufikia sehemu wakakiri hadharani kuwa hawajui ni kwa nini nchi wanazoongoza ni masikni kitu ambacho hata mtoto mdogo anakijua.
Hakuna laana kwa nchi kama kuwashindisha watu juani eti wanafanya uchaguzi pamoja na kutumia pesa nyingi wakati wewe unatumia dola na kuwambia kuwa 'hata mkichagua msindi tayari tunamjua'!
 
Kila kitu chochote kizuri unachokiona duniani kimesimama katika misingi ya ukweli na kujitoa (sacrifice) vivyo hivyo mambo yote yanayomsababishia binadamu matatizo na majuto yamesimama katika uongo uliofanywa na binadamu huyo huyo.
Hapa ni kuwa unavyochelewa kuutambua ukweli na kuufuata ndivyo matatizo yatakavyozidi kukuandama na wengine kufikia sehemu wakakiri hadharani kuwa hawajui ni kwa nini nchi wanazoongoza ni masikni kitu ambacho hata mtoto mdogo anakijua.
Hakuna laana kwa nchi kama kuwashindisha watu juani eti wanafanya uchaguzi pamoja na kutumia pesa nyingi wakati wewe unatumia dola na kuwambia kuwa 'hata mkichagua msindi tayari tunamjua'!
andiko lako limesababisha nibubujikwe na machozi !
 
Na msimamizi mkuu wa haki hapa nchini kila siku anaimba eti Muniombee kwa Mungu maana kazi hii ya kutenda haki ni ngumu sana. Mungu anayeomba tumuombee sijui ni huyuhuyu anayejulikana na wengi au huyu ni wake mwenyewe.
nawahurumia sana wanangu na wajukuu zangu maana hawana nchi nyingine zaidi ya hiii ambayo wamezaliwa ndani yake .
 
utukufu wa Mungu ni wa ajabu sana !
Mkuu hao wanao jiona wana makucha marefu,meno marefu na mikono yenye misuli minene hivyo kufanya lolote watakalo hapa duniani, mungu anawaangalia kwa jicho la kejeli sana na siku atakapo washushia kichapo wataishia kung'ata masikio kama mike tyson
 
Ni maneno machache lakini yamebeba ujumbe mzito sana !

Hakika kwa yanayoendelea kwenye siasa za nchi yetu tangu uchaguzi mkuu , inahitaji roho ya paka kuyavumilia .

walioshinda wananyang'anywa hivi hivi macho makavu na Mungu ni shahidi ! kilombero waliokuwa wengi wamedhulumiwa , Tanga walioaminiwa na wananchi wameporwa haki yao , Dar es salaam inakaribia nusu mwaka tangu uchaguzi lakini wenye haki wanapigwa danadana , ya Zanzibar sina haja ya kuyarudia.

itoshe tu kusema mshahara wa dhambi ni mauti maana yote haya Mungu anayaona , nimeweka angalizo hili ili tusije kujuta siku za usoni kwa vile ilishasemwa na wahenga kwamba Majuto ni mjukuu .

NAKULILIA TANZANIA .
Mkuu Mungu ni mwema na mwaminifu ipo cku tutashinda. Haya ni mambo ya kupita tu.
 
Sisi waafrica tumelaniwa hatufanyi kitu kikasonga mbele zaid ya wizi na kuneemesha familia zaoo
 
Halafu wakiwa kwenye nyumba za ibada utawasikia wakisema hivi MIMi NI SIRA WA NCHI HII NAOMBENI MMIOMBEE NIONGOZE VYEMA!!!, sa mi nashngaa inamaana huw 2nawaombea mabaya au MUNGU ndo anawapima kuhusu UONGOZI wao?!!
 
Back
Top Bottom