Msemakweli asakwa na polisi

Wakuu, hii habari msithubutu kuiamini hata kidogo. Chonde chonde wakuu.
 
KUNA ofisa mwenzetu wa polisi kituo cha Kijitonyama ametumwa na Yuauf Manji amkamate mwanasheria na Mwalimu wa Chuo Kikuu Huria, Kainerugaba Erick Msemakweli, kwa madai kwamba alimuomba rushwa ya Sh Milioni kumi.
BTW Yusuph Manji ana kituo cha Polisi?

Ama una maana alienda kufungua mashtaka ya kuombwa rushwa?

Hii nchi bana!
 
Na miye mwenzenu nilisema magazeti ambayo yanakubali kutekeleza amri hiyo ya mahakama yanakuwa ni washirika wa kumpa nguvu Manji ambazo hana. Huwezi kuzuia watu hata kufikiria. Amri za mahakama ambazo zimetolewa kwa ajili ya Manji ni wazi zinashambulia bila kupumzika uhuru wa maoni na uhuru wa habari pamoja na haki za wananchi kupata habari mbalimbali.
 

Hivi na wewe ni mtu wa kuongea mbele ya watu?
 

Hii ni kauli nzito sana, Mungu atunusuru, maana Watanzania ni wapole sana, tusiwafikishe mahala pa kufanya maamuzi mabaya. Kwa sasa polisi wamepumzika kuokota maiti za watu wanaouwawa na "wananchi wenye hasira kali" ama wale "wanaouwawa katika mapambano kati ya polisi na majambazi" kutokana na polisi kudhibiti uhalifu hadi pikipiki na polisi wanaanza kazi ya kushughulika na makosa ya barabarani na kufuatilia taarifa, lakini soon "wananchi wenye hasira" na "mapambano ya polisi" yatahamia kwa watuhumiwa wakubwa maana kina Msemakweli wako wengi na watakata tamaa na kina "Zombe" na "koplo Saad" wako wengi wanazuiwa kuwakamata kina "Manji", mwishowe wataamua kufanya watakavyo, kwa kuona wakubwa ndio wanaofaidi na wao na wazazi wao wakiteseka.
 
uko sahihi, habari hii c ya kweli. kiranja jiangalie!

Tupeni nyie ukweli wenyewe, maana hamjui ninayewaambia nimepataje habari. Musipotezee watu mda wa kujadili mambo ya maana. Subirini ifike siku hao akina Manji watakimbilia Dubai tutabanana hapa hapa na nyie
 

Mkuu kwa kweli lazima media zetu ziamue kuvunja hizi amri za ovyo za mahakama kwa kutumia kinga ya kikatiba. Maana katiba inatoa uhuru wa kutoa ambao unataka kupokwa na Manji kwa kutumia mahakama.
 
nikisema nchi ya wajinga watu wanakuwa wakali haya sasa huo ni ujanja?,na we unatumwa kijinga ukiulizwa kiapo na amri.sawa vumilia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…