Msemaji wa Singida FG: Nadhani Watanzania mshaitambua Yanga B ni timu gani

Frank Wanjiru

JF-Expert Member
Apr 12, 2012
21,841
38,736
Baada ya kikosi cha Simba Sc, kuruhusu kichapo cha mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya mtani wake Yanga Sc, Afisa Habari wa Singida Fountain Gate, Hussein Massanza ameibuka na kusema kuwa ni rasmi kuwa watanzania na wanasoka watakuwa wameitambua Yanga B kwenye soka la ‘bongo’ ni timu gani.

Massanza amesema kuwa kumekuwa na kauli nyingi zinazosema kuwa Singida FG ni Yanga B kila wanapopoteza mchezo dhidi ya Yanga hivyo ameeleza kuwa kwa kuwa Simba nayo imepoteza mchezao kwa goli nyingi ambazo wao kama Singida hawajahi kufungwa na Yanga hivyo basi Simba ndiyo Yanga B.

“Sasa nadhani Yanga B mmeiona, sisi huwa tunasingiziwa tu, maana tukipoteza mchezo dhidi ya Yanga tunaitwa Yanga B, je hawa waliopoteza kwa idadi ya goli 5-1 tuwaite vipi?,” amesema Massanza.

Cc: Hussein Massanza
 
Hao Yanga si juzi tu tumetoka kuwafunga 5-2 kule Tanga.

Au tuliwafunga ngapi?
 
Baada ya kikosi cha Simba Sc, kuruhusu kichapo cha mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya mtani wake Yanga Sc, Afisa Habari wa Singida Fountain Gate, Hussein Massanza ameibuka na kusema kuwa ni rasmi kuwa watanzania na wanasoka watakua wameitambua Yanga B kwenye soka la ‘bongo’ ni timu gani.

Massanza amesema kuwa kumekuwa na kauli nyingi zinazosema kuwa Singida FG ni Yanga B kila wanapopoteza mchezo dhidi ya Yanga hivyo ameeleza kuwa kwa kuwa Simba nayo imepoteza mchezao kwa goli nyingi ambazo wao kama Singida hawajahi kufungwa na Yanga hivyo basi Simba ndiyo Yanga B.

“Sasa nadhani Yanga B mmeiona, sisi huwa tunasingiziwa tu, maana tukipoteza mchezo dhidi ya Yanga tunaitwa Yanga B, je hawa waliopoteza kwa idadi ya goli 5-1 tuwaite vipi?,” amesema Massanza.

Cc: Hussein Massanza
Amesema kweli na watasema yote. BADO TUNASUBIRI WASEME WALINUNULIWA PIA NA YANGA, maana Yanga kila akishinda kanunua mechi.
 
Hao Yanga si juzi tu tumetoka kuwafunga 5-2 kule Tanga.

Au tuliwafunga ngapi?
IMG-20231105-WA0028.jpg
 
Back
Top Bottom